MICHAKATO

Levis Rocky Ndekeno

This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Pages

Thursday, September 18, 2014

Ndekeno Production

Sunday, September 14, 2014

BAPTIST DAY (Sept 2014)



REMNANT CHRISTIAN CENTRE src=

Monday, September 8, 2014

Ndekeno Production



REMNANT CHRISTIAN CENTRE

Sunday, August 24, 2014

Remnant Christian Centre: PICHA: 1Year of ANNIVERSARY Remnant Christian Cent...

Remnant Christian Centre: PICHA: 1Year of ANNIVERSARY Remnant Christian Cent...: TUNAMSHUKUR MUNGU TUMEFIKISHA MWAKA TANGIA HUDU...

REMNANT CHRISTIAN CENTRE

Wednesday, July 2, 2014

MASANJA MKANDAMIZAJI AANDIKIWA BARUA ''NI VIZURI UKACHAGUA MOJA! MASANJA MKANDAMIZAJI AANDIKIWA BARUA ''NI VIZURI UKACHAGUA MOJA!


KWAKO, Emmanuel Mgaya ‘Masanja’. Naamini u mzima na unaendelea vyema na majukumu yako ya kila siku. Kwa upande wangu nipo sawa, nakimbizana na maisha.
Nina machache ya kukushauri kuhusiana na maisha yako kama staa ambaye kwa sasa umetangaza kuokoka. Kwa maneno mengine ni kwamba, umeondoka kwenye utaifa, upo mikononi mwa Muumba wako.Nimekufahamu kwa kitambo kidogo. Kwangu mimi, wewe ni mmoja wa mastaa wa ukweli katika uchekeshaji Bongo. Mwenye kipaji cha hali ya juu na unayejua unachokifanya.
Tatizo ni kwamba, nashangazwa na aina ya maisha yako baada ya kutangaza kuokoka. Ninavyojua mimi, kuokoka ni kuachana na maisha ya awali ambayo (pengine) yalikuwa hayampendezi Mola na kugeukia katika maisha safi.Niliposikia umeokoka nilifurahi kuona kuwa umeelekea sehemu sahihi zaidi kiimani. Lakini moyoni nilikuwa na shaka kidogo maana wapo wasanii wengi kwenye uigizaji ambao walitangaza kuokoka lakini baadaye wakaonekana kwenye njia zao za awali.
Ukiachana na waigizaji, pia kuna wasanii wa Bongo Fleva ambao nao waliingia kwenye ulokole na mara wakaamua kurudia maisha yao ya awali.Baadaye  nikasikia kuwa unasomea Uchungaji (ingawa inaelezwa kuwa ni Uinjilisti), hapo sikuwa na shaka tena na wokovu wako. Niliamini kwa mtu ambaye ameamua kuingia kwenye kufundisha wengine njia iliyo sahihi hawezi kudanganya kuwa ameokoka.
Siyo kama naingilia maisha yako au nakukosoa kwenye suala la imani yako. Uzuri ni kwamba, nami ninaamini katika imani yako, hivyo sioni tatizo kukushauri.Tatizo lipo kwenye staili yako ya maisha. Ni kweli kwamba umeokoka, lakini itawezekana vipi usuke mabutu kichwani? Maandiko yanaeleza wazi kuwa, wanaoamini ni barua inayosomeka kwa watu wote.
Je, watu watasoma nini kupitia mabutu? Unaweza kusema kuwa, imani ya mtu iko moyoni, hapo sitakubaliana na wewe, maana kinachoonekana nje, kinawakilisha kilichomo ndani.Vipi kama kanisa zima, wanaume wataingia  wamesuka? Nafikiri si jambo sahihi. Watu watapata shaka na wokovu wako, tena mchunga kondoo. Wengine wanaweza kuona wokovu si jambo ‘serious’. Kwamba mtu anaweza kuingia na akaendelea na mambo yake yaleyale, jambo ambalo si la kweli.
Wokovu ni pamoja na mwonekano wa nje. Mavazi, mitindo ya nywele n.k.Jambo jingine ambalo limenishangaza ni namna unavyoingiza komedi kwenye mambo yanayohusu dini.Usahihi wa kufanya utani kwenye vichekesho huku ukitaja jina la Mungu unatokea wapi? Masanja tumezuiwa kufanya mzaha au kulitaja bure Jina la Mungu wetu.
Nakushauri kama ni kweli umeamua kuokoka, badilika lakini kama unahisi bado unatamani maisha ya kawaida na kujichanganya, chagua moja ili jamii isikutafsiri tofauti.Ni uamuzi wako kufuata au kuacha hapahapa, lakini la muhimu ni kwamba, nitakuwa nimeshakushauri. Ubarikiwe sana mpendwa!
Yuleyule,
Mkweli daima,
.........................
Joseph Shaluwa.


Saturday, June 28, 2014

TUZO ZA WATU ILIYOFANYIKA IJUMAA HII

 
Tuzo za watu za Tanzania au Tanzania People’s Choice Awards zimetolewa Ijumaa hii kwenye ukumbi uliopo Serena Hotel jijini Dar es Salaam. Jumla ya vipengele 11 vilikuwa vinashindaniwa. Mshindi katika kila kipengele ameibuka na zawadi ya shilingi milioni moja pamoja na trophy. Host wa tuzo hizo alikuwa mtangazaji mkongwe wa radio, Jimmy Kabwe.
1. MTANGAZAJI WA REDIO ANAYEPENDWA
 Millard Ayo – Clouds FM

2. KIPINDI CHA REDIO KINACHOPENDWA
 Amplifaya – Clouds FM

3.MTANGAZAJI WA RUNINGA ANAYEPENDWA
 Salim Kikeke – BBC Swahili

4. KIPINDI CHA RUNINGA KINACHOPENDWA
 Mkasi – EATV

5. MWANAMICHEZO ANAYEPENDWA
 Juma Kaseja – Yanga

6. MUONGOZAJI WA VIDEO ZA MUZIKI ZINAZOPENDWA
 Nisher

7. VIDEO YA MUZIKI INAYOPENDWA YA MWANAMUZIKI WA KIUME
 My Number – Diamond

8. VIDEO YA MUZIKI INAYOPENDWA YA MWANAMUZIKI WA KIKE
 Yahaya – Lady Jaydee

09. MUIGIZAJI WA KIUME KWENYE FILAMU ANAYEPENDWA
 King Majuto

10. MUIGIZAJI WA KIKE KWENYE FILAMU ANAYEPENDWA
 Elizabeth ‘Lulu’ Michael

11. FILAMU INAYOPENDWA
 Ndoa Yangu




Wednesday, June 25, 2014

June 25: Ni Miaka miaka mitano tangu kifo cha Michael Jackson






Michael Jackson alifariki June 25, 2009, katika muda aliokuwa akiutafuta sana usingizi huku akijiandaa kurejea kwa kufanya ziara yake ambayo aliamini ingemuondoa kwenye madeni mengi na kurudisha heshima yake kama mfalme wa pop. Katika siku zake za mwisho, Michael Jackson aliondoka nchini Marekani akiwa na wanae watatu muda mfupi baada ya kumalizika kwa kesi yake ya kulawiti watoto.

Alirejea Marekani kimyakimya mwaka 2006, baada ya kukaa huko Bahrain kwa mwaka mzima na miezi kadhaa nchini Ireland. Bill Whitfield na Jevon Beard walitumia miaka miwili kama walinzi wa MJ walisimulia mengi kwenye kitabu kipya kiitwacho s “Remember the Time: Protecting Michael Jackson in His Final Days.” Kipindi Jackson anashuka kutoka kwenye ndege binafsi jijini Las Vegas, watu aliokuwa nao walikuwa wanae na mlezi wa watoto wake tu. “Alikuwa peke yake,” Whitfield alisema kwenye mahojiano na CNN. Kikawa kitu kisicho cha kawaida. Kuna kitu hakipo sawa. Huu ni utani.”

Walinzi hao ambao wakati mwingine hawakuwa wakilipwa mshahara kwa miezi, walikuwa wakitumia fedha zao kusaidia masuala nyumbani kwa Jackson pale credit cards zake zilipokuwa zikiishiwa. Beard aliiambia CNN kuwa mameneja wake walikuwa wakimzunguka. “Jamaa alikuwa amechoka kiakili.” Whitfield na Beard walidai kuwa Jackson alikuwa na mambo yake ya siri yaliyokuwa yakijulikana labda kwa mashabiki wake waliokuwa wakimganda. Jackson alikuwa na mademu.

Mfalme huyo wa pop alikuwa akitumia muda wa faragha na mwanamke nyuma ya pazia kwenye siti ya nyuma ya gari wakati walinzi wakiendesha. Wanadai kuwa Jackson alikuwa akipenda wasichana na walimuona kwa macho yao akiwabusu. Wanawake hao, ambao walinzi waliamini walikuwa wakitokea Ulaya, hawakuwahi kwenda nyumbani kwake na hawakuwahi kukutana na wanae.

Alikuwa akirudi nyumbani kutoka kwenye mishe zake kabla ya wanae Prince, Paris na Blanket hawajaamika. Jackson aliwaagiza walinzi wake kuwazuia kaka zake, dada zake na baba yake kuingi kwake japo mama yake alikuwa akiruhusiwa kuingia nyumbani kwake.

Pamoja na kuwa hayupo tena, muziki wa Michael Jackson bado unaendelea kutoka ambapo sasa album yake Xscape ipo sokoni na iliuza kopi milioni 2.3 katika wiki tatu tangu itoke mwezi May. Ukurasa wake wa Facebook una likes milioni 75 ziadi hata Justin Bieber, Lady Gaga, Katy Perry, Taylor Swift na Bruno Mars.

Chanzo: CNN. Soma zaidi makala hiyo hapa.