Thursday, September 18, 2014
Sunday, September 14, 2014
Monday, September 8, 2014
Sunday, August 24, 2014
Remnant Christian Centre: PICHA: 1Year of ANNIVERSARY Remnant Christian Cent...
Remnant Christian Centre: PICHA: 1Year of ANNIVERSARY Remnant Christian Cent...: TUNAMSHUKUR MUNGU TUMEFIKISHA MWAKA TANGIA HUDU...
REMNANT CHRISTIAN CENTRE
REMNANT CHRISTIAN CENTRE
Wednesday, July 2, 2014
MASANJA MKANDAMIZAJI AANDIKIWA BARUA ''NI VIZURI UKACHAGUA MOJA! MASANJA MKANDAMIZAJI AANDIKIWA BARUA ''NI VIZURI UKACHAGUA MOJA!
KWAKO, Emmanuel Mgaya ‘Masanja’. Naamini u mzima na unaendelea
vyema na majukumu yako ya kila siku. Kwa upande wangu nipo sawa, nakimbizana na
maisha.
Nina machache ya kukushauri kuhusiana na maisha yako kama staa ambaye kwa sasa umetangaza kuokoka. Kwa maneno mengine ni kwamba, umeondoka kwenye utaifa, upo mikononi mwa Muumba wako.Nimekufahamu kwa kitambo kidogo. Kwangu mimi, wewe ni mmoja wa mastaa wa ukweli katika uchekeshaji Bongo. Mwenye kipaji cha hali ya juu na unayejua unachokifanya.
Tatizo ni kwamba, nashangazwa na aina ya maisha yako baada ya kutangaza kuokoka. Ninavyojua mimi, kuokoka ni kuachana na maisha ya awali ambayo (pengine) yalikuwa hayampendezi Mola na kugeukia katika maisha safi.Niliposikia umeokoka nilifurahi kuona kuwa umeelekea sehemu sahihi zaidi kiimani. Lakini moyoni nilikuwa na shaka kidogo maana wapo wasanii wengi kwenye uigizaji ambao walitangaza kuokoka lakini baadaye wakaonekana kwenye njia zao za awali.
Ukiachana na waigizaji, pia kuna wasanii wa Bongo Fleva ambao nao waliingia kwenye ulokole na mara wakaamua kurudia maisha yao ya awali.Baadaye nikasikia kuwa unasomea Uchungaji (ingawa inaelezwa kuwa ni Uinjilisti), hapo sikuwa na shaka tena na wokovu wako. Niliamini kwa mtu ambaye ameamua kuingia kwenye kufundisha wengine njia iliyo sahihi hawezi kudanganya kuwa ameokoka.
Siyo kama naingilia maisha yako au nakukosoa kwenye suala la imani yako. Uzuri ni kwamba, nami ninaamini katika imani yako, hivyo sioni tatizo kukushauri.Tatizo lipo kwenye staili yako ya maisha. Ni kweli kwamba umeokoka, lakini itawezekana vipi usuke mabutu kichwani? Maandiko yanaeleza wazi kuwa, wanaoamini ni barua inayosomeka kwa watu wote.
Je, watu watasoma nini kupitia mabutu? Unaweza kusema kuwa, imani ya mtu iko moyoni, hapo sitakubaliana na wewe, maana kinachoonekana nje, kinawakilisha kilichomo ndani.Vipi kama kanisa zima, wanaume wataingia wamesuka? Nafikiri si jambo sahihi. Watu watapata shaka na wokovu wako, tena mchunga kondoo. Wengine wanaweza kuona wokovu si jambo ‘serious’. Kwamba mtu anaweza kuingia na akaendelea na mambo yake yaleyale, jambo ambalo si la kweli.
Wokovu ni pamoja na mwonekano wa nje. Mavazi, mitindo ya nywele n.k.Jambo jingine ambalo limenishangaza ni namna unavyoingiza komedi kwenye mambo yanayohusu dini.Usahihi wa kufanya utani kwenye vichekesho huku ukitaja jina la Mungu unatokea wapi? Masanja tumezuiwa kufanya mzaha au kulitaja bure Jina la Mungu wetu.
Nakushauri kama ni kweli umeamua kuokoka, badilika lakini kama unahisi bado unatamani maisha ya kawaida na kujichanganya, chagua moja ili jamii isikutafsiri tofauti.Ni uamuzi wako kufuata au kuacha hapahapa, lakini la muhimu ni kwamba, nitakuwa nimeshakushauri. Ubarikiwe sana mpendwa!
Yuleyule,
Mkweli daima,
.........................
Joseph Shaluwa.
Nina machache ya kukushauri kuhusiana na maisha yako kama staa ambaye kwa sasa umetangaza kuokoka. Kwa maneno mengine ni kwamba, umeondoka kwenye utaifa, upo mikononi mwa Muumba wako.Nimekufahamu kwa kitambo kidogo. Kwangu mimi, wewe ni mmoja wa mastaa wa ukweli katika uchekeshaji Bongo. Mwenye kipaji cha hali ya juu na unayejua unachokifanya.
Tatizo ni kwamba, nashangazwa na aina ya maisha yako baada ya kutangaza kuokoka. Ninavyojua mimi, kuokoka ni kuachana na maisha ya awali ambayo (pengine) yalikuwa hayampendezi Mola na kugeukia katika maisha safi.Niliposikia umeokoka nilifurahi kuona kuwa umeelekea sehemu sahihi zaidi kiimani. Lakini moyoni nilikuwa na shaka kidogo maana wapo wasanii wengi kwenye uigizaji ambao walitangaza kuokoka lakini baadaye wakaonekana kwenye njia zao za awali.
Ukiachana na waigizaji, pia kuna wasanii wa Bongo Fleva ambao nao waliingia kwenye ulokole na mara wakaamua kurudia maisha yao ya awali.Baadaye nikasikia kuwa unasomea Uchungaji (ingawa inaelezwa kuwa ni Uinjilisti), hapo sikuwa na shaka tena na wokovu wako. Niliamini kwa mtu ambaye ameamua kuingia kwenye kufundisha wengine njia iliyo sahihi hawezi kudanganya kuwa ameokoka.
Siyo kama naingilia maisha yako au nakukosoa kwenye suala la imani yako. Uzuri ni kwamba, nami ninaamini katika imani yako, hivyo sioni tatizo kukushauri.Tatizo lipo kwenye staili yako ya maisha. Ni kweli kwamba umeokoka, lakini itawezekana vipi usuke mabutu kichwani? Maandiko yanaeleza wazi kuwa, wanaoamini ni barua inayosomeka kwa watu wote.
Je, watu watasoma nini kupitia mabutu? Unaweza kusema kuwa, imani ya mtu iko moyoni, hapo sitakubaliana na wewe, maana kinachoonekana nje, kinawakilisha kilichomo ndani.Vipi kama kanisa zima, wanaume wataingia wamesuka? Nafikiri si jambo sahihi. Watu watapata shaka na wokovu wako, tena mchunga kondoo. Wengine wanaweza kuona wokovu si jambo ‘serious’. Kwamba mtu anaweza kuingia na akaendelea na mambo yake yaleyale, jambo ambalo si la kweli.
Wokovu ni pamoja na mwonekano wa nje. Mavazi, mitindo ya nywele n.k.Jambo jingine ambalo limenishangaza ni namna unavyoingiza komedi kwenye mambo yanayohusu dini.Usahihi wa kufanya utani kwenye vichekesho huku ukitaja jina la Mungu unatokea wapi? Masanja tumezuiwa kufanya mzaha au kulitaja bure Jina la Mungu wetu.
Nakushauri kama ni kweli umeamua kuokoka, badilika lakini kama unahisi bado unatamani maisha ya kawaida na kujichanganya, chagua moja ili jamii isikutafsiri tofauti.Ni uamuzi wako kufuata au kuacha hapahapa, lakini la muhimu ni kwamba, nitakuwa nimeshakushauri. Ubarikiwe sana mpendwa!
Yuleyule,
Mkweli daima,
.........................
Joseph Shaluwa.
Saturday, June 28, 2014
TUZO ZA WATU ILIYOFANYIKA IJUMAA HII
Tuzo za watu
za Tanzania au Tanzania People’s Choice Awards zimetolewa Ijumaa hii kwenye
ukumbi uliopo Serena Hotel jijini Dar es Salaam. Jumla ya vipengele 11 vilikuwa
vinashindaniwa. Mshindi katika kila kipengele ameibuka na zawadi ya shilingi
milioni moja pamoja na trophy. Host wa tuzo hizo alikuwa mtangazaji mkongwe wa
radio, Jimmy Kabwe.
1.
MTANGAZAJI WA REDIO ANAYEPENDWA
Millard Ayo – Clouds FM
2. KIPINDI
CHA REDIO KINACHOPENDWA
Amplifaya – Clouds FM
3.MTANGAZAJI
WA RUNINGA ANAYEPENDWA
Salim Kikeke – BBC Swahili
4. KIPINDI
CHA RUNINGA KINACHOPENDWA
Mkasi – EATV
5.
MWANAMICHEZO ANAYEPENDWA
Juma Kaseja – Yanga
6.
MUONGOZAJI WA VIDEO ZA MUZIKI ZINAZOPENDWA
Nisher
7. VIDEO YA
MUZIKI INAYOPENDWA YA MWANAMUZIKI WA KIUME
My Number – Diamond
8. VIDEO YA
MUZIKI INAYOPENDWA YA MWANAMUZIKI WA KIKE
Yahaya – Lady Jaydee
09.
MUIGIZAJI WA KIUME KWENYE FILAMU ANAYEPENDWA
King Majuto
10.
MUIGIZAJI WA KIKE KWENYE FILAMU ANAYEPENDWA
Elizabeth ‘Lulu’ Michael
11. FILAMU
INAYOPENDWA
Ndoa Yangu
Wednesday, June 25, 2014
June 25: Ni Miaka miaka mitano tangu kifo cha Michael Jackson
Michael
Jackson alifariki June 25, 2009, katika muda aliokuwa akiutafuta sana usingizi
huku akijiandaa kurejea kwa kufanya ziara yake ambayo aliamini ingemuondoa
kwenye madeni mengi na kurudisha heshima yake kama mfalme wa pop. Katika siku
zake za mwisho, Michael Jackson aliondoka nchini Marekani akiwa na wanae watatu
muda mfupi baada ya kumalizika kwa kesi yake ya kulawiti watoto.
Alirejea
Marekani kimyakimya mwaka 2006, baada ya kukaa huko Bahrain kwa mwaka mzima na
miezi kadhaa nchini Ireland. Bill Whitfield na Jevon Beard walitumia miaka
miwili kama walinzi wa MJ walisimulia mengi kwenye kitabu kipya kiitwacho s
“Remember the Time: Protecting Michael Jackson in His Final Days.” Kipindi
Jackson anashuka kutoka kwenye ndege binafsi jijini Las Vegas, watu aliokuwa
nao walikuwa wanae na mlezi wa watoto wake tu. “Alikuwa peke yake,” Whitfield
alisema kwenye mahojiano na CNN. Kikawa kitu kisicho cha kawaida. Kuna kitu
hakipo sawa. Huu ni utani.”
Walinzi hao
ambao wakati mwingine hawakuwa wakilipwa mshahara kwa miezi, walikuwa wakitumia
fedha zao kusaidia masuala nyumbani kwa Jackson pale credit cards zake
zilipokuwa zikiishiwa. Beard aliiambia CNN kuwa mameneja wake walikuwa
wakimzunguka. “Jamaa alikuwa amechoka kiakili.” Whitfield na Beard walidai kuwa
Jackson alikuwa na mambo yake ya siri yaliyokuwa yakijulikana labda kwa
mashabiki wake waliokuwa wakimganda. Jackson alikuwa na mademu.
Mfalme huyo
wa pop alikuwa akitumia muda wa faragha na mwanamke nyuma ya pazia kwenye siti
ya nyuma ya gari wakati walinzi wakiendesha. Wanadai kuwa Jackson alikuwa
akipenda wasichana na walimuona kwa macho yao akiwabusu. Wanawake hao, ambao
walinzi waliamini walikuwa wakitokea Ulaya, hawakuwahi kwenda nyumbani kwake na
hawakuwahi kukutana na wanae.
Alikuwa
akirudi nyumbani kutoka kwenye mishe zake kabla ya wanae Prince, Paris na
Blanket hawajaamika. Jackson aliwaagiza walinzi wake kuwazuia kaka zake, dada
zake na baba yake kuingi kwake japo mama yake alikuwa akiruhusiwa kuingia
nyumbani kwake.
Pamoja na
kuwa hayupo tena, muziki wa Michael Jackson bado unaendelea kutoka ambapo sasa
album yake Xscape ipo sokoni na iliuza kopi milioni 2.3 katika wiki tatu tangu
itoke mwezi May. Ukurasa wake wa Facebook una likes milioni 75 ziadi hata
Justin Bieber, Lady Gaga, Katy Perry, Taylor Swift na Bruno Mars.
Chanzo: CNN.
Soma zaidi makala hiyo hapa.












