MICHAKATO

Levis Rocky Ndekeno

This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Pages

Sunday, July 29, 2018

Ripoti: Mfumo wa uongozi WCB, mikataba ya wasanii pamoja na wanaomiliki hisa nyingi za kampuni

WCB ni moja kati ya label kubwa za muziki nchini Tanzania yenye mafanikio zaidi kutokana na ukubwa wa wasanii wake pamoja na uwekezaji walioufanya kwenye tasnia ya muziki wa BongoFleva.
Label hiyo inaongozwa na rais wa label hiyo ambaye pia ni msanii, Diamond Platnumz akishirikiana na Manangers,Sallam aka Mendez, Said Fella maarufu kama Mkubwa Fella pamoja na Hamisi Taletale aka Babu Tale.
Ukiachana na viongozi hao watatu pia kuna mameneja wengine wadogo wadogo ambao wana majukumu ya kuwasimamia wasanii waliosainiwa na label hiyo, ambao ni Ricardo Momo, Makame pamoja Sandra.
Label hiyo ina wasanii saba, Rayvanny, Queen Darleen, Harmonize, Lava Lava, Mbosso, Diamond Platnumz pamoja Rich Mavoko ambaye amekua yupo kimya kwa muda mrefu huku akihusishwa na kutaka kuachana na label hiyo.
Diamond ni nani WCB na wanahisa wengine wa label hiyo.
Diamond Platnumz ndio kila kitu ndani ya WCB, ni Mkurugenzi Mkuu na ndio mwenye hisa nyingi ndani ya kampuni hiyo, hivyo basi ndio mwenye kauli ya mwisho katika maamuzi. Wakurungezi wengine wenye hisa ni pamoja na Sallam, Mkubwa Fella, Babu Tale pamoja na Mama Diamond ambao wanatambuliwa na memorandum ya kampuni hiyo.
Diamond Platnumz
Kwa mujibu wa chanzo chetu cha uhakika kimedai, Mama Diamond yupo kwenye kampuni hiyo kama mkurugenzi huru ambaye ana jukumu la kuangalia kampuni inaendaje pamoja na kutoa ushauri katika baadhi ya mambo.
Kampuni ya WCB yenye makazi yake Mbezi jijini Dar es salaam, kwa sasa inamiliki Wasafi TV, Wasafi Redio,Wasafi.com, Wasafi Records Music Studio, Chibu Perfume pamoja na Diamond Karanga.
Mwaka mmoja uliopita wakati anatambulishwa Mbosso, Fella alitoa kauli ya kumtaka rais wa label hiyo Diamond Platnumz kuongeza kamisheni kwa mameneja hao kutokana na kazi kubwa wanazifanya.
“Kwa mara ya kwanza Diamond ameleta mapindunzi kwenye muziki kwa mameneja kulipwa. Wasanii wengine sisi ndio tunatoa hela, lakini huyu sisi anatulipa, Sallam analipwa japokuwa anauza magari, mimi diwani nalipwa na Diamond, Tale ana ishu zake nyingine lakini analipwa na huyu, na kuna deal nyingine inakuja tutakaa nusu kwa nusu,” alisema Mkubwa Fella
Fella aliwahi kunukuliwa na chombo kimoja cha habari nchini Tanzania  akisema kwamba katika kila mapato ya Diamond ya mwezi mmoja, asilimia 30 inaenda kwa mameneja wake hao watatu. Yaani kama Diamond akiingiza milioni 100 kwa mwezi basi milioni 30 zinaenda kwa mameneja wake.
Fella ana jukumu gani WCB?.
Mkubwa Fella ni mmoja kati ya wakurugenzi wa WCB, lakini pia ana simama kama mmoja kati ya mameneja watatu wa Diamond Platnumz.
“Mimi ni mmoja kati ya wakurungezi wa WCB lakini pia ni meneja wa Diamond, na kama unavyojua kazi ya mkurungezi wa kampuni ni kuhakikisha kampuni inaenda mbele na inaendelea kukua. Pia kusimamia utendaji mzima wa WCB, kuwaangalia wasanii wetu pamoja na mameneja wao,” Fella aliiambia Bongo5.
Pia Fella ni mzee wa busara ndani ya label hiyo, na mara nyingi ndiye mtu ambaye ana zima moto kama kuna jambo limetokea ndani ya kampuni hiyo. Yeye hufanya hivyo hata nje ya kampuni kama kuna suala ambalo limeleta taharuki huwa anaweka mambo sawa kwani sio mtu wakupaniki na kukurupuka.
Sallam SK ana majukumu gani WCB?.
Sallam aka Mendez ni mmoja kati ya Wakurungezi wa WCB ambaye pia ni meneja wa Diamond wa Kimataifa. Meneja huyo amekuwa akionekana sana katika kumtafutia deals Diamond, shows za nje pamoja na kuingia mikataba na makampuni mbalimbali ya muziki duniani kwa ajili ya kuipeleka kimataifa brand ya WCB.
Sallam SK
Kifesi ambaye alikuwa mpiga picha wa Diamond na WCB, alisema kwamba Sallam ni kiongozi wa kampuni hiyo ambaye amechukua jukumu kubwa la kulinda brand pamoja na kuhakikisha kazi za kampuni hiyo zinaenda kama zilivyopangwa.
Babu Tale ana majukumu gani WCB?
Huyu ni Master in Street Management kama anavyojiita mwenyewe. Babu Tale ndiye mwenye kitengo cha lawama WCB lakini ni mlezi wa wasanii pamoja na WCB nzima. Mara nyingi amekuwa mtatuzi wa shida nyingi za wafanyakazi wake lakini ni mtu mwenye maamuzi ya hapo hapo akiona kuna tatizo au kuna mtu analeta shida ndio maana hata baadhi ya wafanyakazi wanaotoka WCB mara nyingi wanamtupia lawama
Babu Tale
Tale ndiye aliyekabidhiwa kitengo cha lawama kama nilivyozungumza hapo awali, unakumbuka alivyojilipua kwa kauli yake ya kutaka ngoma zao zisipigwe katika vituo vya redio na TV, nani ungeweza kujilipua na kutamba kama alivyofanya Babu Tele?.
Wiki hii aliyekuwa mfanyakazi wa Social Media WCB, Almasi Zambele alidai alitimuliwa WCB na Tale kwa madai bosi huyo alikuwa anahitaji kuweka watu wake wapya. Kama nilivyosema hapo awali, Tale ni mkurugenzi, hawezi kubali mtu achafue brand ya WCB ndio maana hata wakati mwingine analaumiwa lakini kiukweli anatekeleza wajibu wake.
Mikataba ya Wasanii wa WCB
Kama unavyojua WCB ni label kubwa nchini Tanzania, Afrika Mashariki pamoja na Afrika kwa sasa, kwa uchunguzi tulioufanya tumegundua wasanii wengi wana mikataba ya muda mrefu tena yenye vipengele ambavyo ukitaka kusaliti kambi lazima ujiulize mara mbili mbili. Lakini wachache wanadaiwa hawana mikataba akiwemo Queen Darleen ambaye ni dada wa Diamond Platnumz.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya WCB, Harmonize na Rich Mavoko wanadaiwa kuwa na mkataba wa miaka 10 na WCB na mtu ambaye atataka kuvunja mkataba atatakiwa kulipa fidia isiyo chini ya tsh milioni 10. Lakini mikataba yao inaweza kubadilika muda wowote kutokana na mafanikio ya wasanii hao. Mikataba ya wasanii wengine imekuwa ni siri kubwa lakini nadhani umepata picha kwamba WCB ni label ya namna gani mpaka sasa.
Wasanii hao wanaingiza pesa kupitia shows na ishu za matangazo, ambapo kampuni huchukua asilimia kadhaa na pesa nyingine huwenda kwa msanii. Pia ishu za production zimebaki kwa WCB, kuanzia video mpaka audio.
Diamond aliwahi kunukuliwa na vyombo vya habari kwamba kuna baadhi ya wasanii kama Harmonize alitumia zaidi ya tsh milioni 100 kwaajili ya kuandaa kazi zake pamoja na kutengeza brand yake.
Hii imetupa picha kwamba WCB sio label ya kawaida, ni lavel za kimatifa, wasanii na wadau wa sanaa wanatakiwa kuanza kutengeza mazingira ya brand za wasanii kama walivyofanya WCB.

Monday, August 14, 2017

Youtube yawezesha wateja wake kuchat na kushare video kwenye programu yake

Mwaka jana 2016 mtandao wa Youtube ulitoa taarifa kuwa utaboresha programu yake ili kuwapa urahisi watumiaji wake kushare video moja kwa moja wakiwa kwenye mtandao huo na kuchat live kwa video watakayokuwa wameishare.

Habari nzuri ni kwamba tayari huduma hiyo imeshaingia barani Afrika kwa watumiaji wote wa Android na iOS ambapo sasa unaweza kufanya vitu vyote kupitia App yako ya YouTube.
Je, utashare na utachati vipi ukiwa kwenye mtandao huo maarufu zaidi duniani? Njia ya kwanza hakikisha ume-update programu yako ya Youtube.
Ukimaliza ku-update juu ya App kuna kitufe kimeongezwa cha Share bonyeza hapo kisha utakuta sehemu ya View Contacts bonyeza hapo kwa ajili ya kuongeza majina ya watu ambao utahitaji kushare na kuchati nao kuhusu video utakayoishare.
Hatua ya mwisho chukua link ya video uipendayo kisha iweke kwenye uwanja na hapo utaanza kuchati na ndugu jamaa na marafiki uliyowaalika.Tazama maelekezo vizuri kwenye video hapo chini (Video by TECH WORLD)
https://www.youtube.com/watch?v=33sY0BUTD44

Sunday, June 11, 2017

Makala: Saida Karoli amewachambua kama karanga Belle 9, Diamond na Darassa

Mwaka 2001 msanii wa muziki wa asili, Saida Karoli alitoa albamu yake ya kwanza ‘Maria Salome’ ambayo ilipata mafanikio makubwa na kuingia katika vitabu vya kumbukumbu vya muziki wa kitanzania.
Albamu hiyo iliyochota vionjo tele vya kabila la Kihaya, mashabiki wengi waliipachika jina la ‘Chambua kama Karanga’ kutokana na maneno yanayopatikana katika wimbo wa Maria Salome ambao umebeba jina la albamu.
Inaelezwa miezi mitatu baada ya kutoa albamu hiyo, Saida Karoli alipata mwaliko wa kuimba nchini Uganda ambapo Kabaka wa Buganda alimwalika katika sherehe ya kiutamaduni, pia kumfanya kuwa mwanamuziki wa mwaka katika sherehe hiyo.
Pia albamu hiyo ilifuatiwa na ziara kubwa alizofanya katika nchi za Burundi, Rwanda, Uganda na Kenya ambapo alipata mafanikio makubwa na Saida kujikuta akibatizwa na kupewa jina la malkia wa nyimbo za asili.
 Karibu Diamond, Darassa na Belle 9
Septemba 18 mwaka jana Diamond Platnumz alitoa wimbo uitwao Salome akiwa amemshirikisha Rayvanny. Wimbo ukiwa umekopa beat, melody na baadhi ya maneno kutoka kwenye wimbo wa Maria Salome wa Saida Karoli.
Wimbo huu uliotengenezwa na prodyuza Lizer kutoka Wasafi Records na video yake kuongozwa na Nocorux kutoka Afrika Kusini, watu wengi walihoji juu ya uhalali wa Diamond kutumia vionjo wa wimbo wa Saida Karoli, lakini uzuri ni kwamba pande zote mbili zilikuwa tayari zimeshahafikiana.
Baada ya Diamond kufanya vizuri sana na wimbo huo, haikuwa ajabu November 23 mwaka jana kuona rapper Darassa akitumia baadhi ya vionjo kutoka kwenye wimbo wa Maria Salome katika wimbo wake ‘Muziki’ aliomshirikisha Ben Pol.
Muziki ni hit sing iliyoweka historia katika maisha ya muziki ya Darassa akipata baraka kutoka kwenye mikono ya prodyuza wa watatu, Mr Vs, Abbah na Mr T Touch.
Wakati watu wakiruka madebe na ngoma ya Muziki na Salome, huku wakijikumbushia mwanzoni mwa miaka ya 2000 walivyolirudi na ngoma ya Maria Salome, mkali wa muziki wa RnB, Belle 9 anadondosha ngoma yenye vionjo sawa na hizi mbili za mwanzo.
Belle 9 alikuja na wimbo uitwao Give It To Me, hiyo ikiwa ni December 17 mwaka jana. Wimbo huu alimshirikisha mkali wa chorus kutoka Weusi, G Nako chini ya prodyuza Luffa.
Saidi Karoli awachambua kama karanga
Wiki hii Saida Karoli ameamua kuvunja ukimya kwa kuachia wimbo uitwao Urugambo. Wimbo huu tunaweza kusema ameamua kijilipa fadhila kwani amechukua baadhi ya maneno kutoka kwenye nyimbo zote tatu nilizozielezea hapo juu.
Akiwa anaimba kiswahili na kikabila (kihaya) kama ilivyo kawaida yake, ameweza kuchanganya nyimbo zote tatu na kutoa kitu kimoja cha kipekee sana ambacho kila upande utakielewa. Najua hujanielewa, namaanisha mashabiki walioanza na Saida Karoli hawatochoka kuusikiliza, na kizazi cha sasa cha Bongo Fleva kitapenda kuusikiliza pia.
Katika wimbo huu wenye dakika 3 na sekunde 58, Saida Karoli ananza kuchambua ngoma ya Darassa Muziki kwa kusema, “Nikamuuliza baba yangu, akasema utafute ule mpaka Dar es Salaama… Nimesimama wima x 2…. Maisha na muziki, acha maneno weka muziki x 2”.
Kisha anaendelea na wimbo wa Belle 9 ‘Give It To Me’, “Nikaenda Dar es Salaam nikakuta wazangu, wanaongea kizungu na mimi nikaimba kizungu,‘Baby give it to me, ahaaa!! x 6”. Wakati akichanganya lugha mbili anaendele na wimbo wa Diamond ‘Salome’.
“Nikaeenda Dar es Salaa nikashanga ‘majumba’,….  “Wanakodoa kodo wanakodoa!! (macho kodo) (wale kodo) x 2”. Kisha chorus fupi yenye melody ya aina yake, watoto wa mjini wanasema amazing, “Baby nimekuweka moyonii, usije ukaniacha nitaumia”.
 Ni faida kwa Bongo Fleva
Bila shaka leo katika vitu 10 ambavyo Fid Q anajivunia katika muziki wake, hawezi kuweka kando mafanikio ya kufanya kazi na wasanii wa zamani kama Zahir Zorro na Bibi Kidude.
Pia tumeona mwaka huu Kassim Mganga akitoa wimbo na Killimanjaro Band (Njenje) ambapo pia Mwana FA alishatoa nao ngoma. Hii maana yake nini?, wasanii wa zamani na wa Bongo Fleva wanapokuwa karibu na kufanya kazi, maana kuna vitu wanaleta katika muziki wa sasa na pengine huko mbeleni tutakuja kupata utambulisho (ID) ya muziki wa kitanzania ambao umekuwa ukisemakana haupo.


By Peter Akaro

Sunday, May 21, 2017

Makala: Safari ya Nisher kwenye game

 Mwaka 2012 akiwa kama director mchanga anayechipukia kwenye game, Nisher alilazimisha macho yetu kutazama runinga ili kushuhudia video mpya ya Joh Makini ‘Sijutii’ ambayo aliifanya yeye. Maswali yakawa ni mengi juu ya ubora wa video ile, ila maswali mengi zaidi yalitaka kujua juu ya aliyetengeneza video huyo. Ndipo jina la Nisher lilipochomoza na watu kuelewa jamaa ni wa Arusha na kazi zake anazifanyika huko huko A Town.
Baada ya majibu hayo haikuwa ajabu kuona baadhi wasanii wakifunga safari kutoka Dar es Salaam hadi Arusha kufanya video na Nisher. Kama unabisha hilo kamuulize Ben Pol alipoifanyia video ya wimbo wake wa Jikubali.
Siku zilivyozidi kuenda jina lake likazidi kukua, yaani ilikuwa ni kazi juu ya kazi kama Darassa anavyoeleza katika wimbo wake wa Muziki. Hii ilikuwa ni zaidi ya ‘Bampa to Bampa’. Jamani twendeni taratibu.
Unakumbuka video kama Nje ya Box ya Weusi, Mama Yeyoo ya G Nako, Xo ya Joh Makini, Unanichora ya Ben Pol, Kijukuu ya Young Dee, 13 ya Young Killer, Bongo Hip Hop ya Fid Q, Press Play ya Dj Choka, Dole ya Mabeste na nyinginezo kiba? Zote zilitoka kwake.
                                        Nisher aliposhinda tuzo, ‘Tuzo za Watu’
Ukali wa video hizo bado hautoshi kuelezea uwezo wake kwenye game ulikuwa wa kiwango gani. Chukua na hii; Mwaka 2014 alishinda award ‘Tuzo za Watu’ akiwa kama Muongozaji wa video anayependwa. Hivyo ndivyo tunaweza kumzungumzia Nisher kwa ufupi
Kwa nini leo Nisher

Imenilazimu kumkumbuka Nisher kwa sasa. Narudia tena, imenilazimu kufanya hivyo kwa sababu kuu mbili. Mosi: Wiki hii makali wa Hip Hop, Joh Makini alikaririwa akisema kuwa ataendelea kushoot video za ngoma zake nje ya nchi kutokana na kufuata ubora huku akiwataka madirector wa ndani kubadilika.
                                                                           Nisher kazini
Kauli hii inaonyesha kuwa industry ya video Bongo bado ipo nchini na itachukua muda kukua kwa sababu wasanii wote walio mainstream wanakimbilia kushoot video nje.
Sababu ya pili kumkumbuka Nisher ni kwamba tangu mwaka huu kuanza ametoa video moja tu ambayo ni ya Edu Boy ‘Naiee’ aliyompa shavu Bill Nas. Uzuri ni kwamba bado ubora na ubunifu wa kazi zake uko pala pale, kama umefanikiwa kuitazama video hii ya Edu Boy utakubaliana na mimi kwa asilimia kubwa, pongezi za kutosha kwake Nisher.
Tuanzie hapa
Wakati Nisher anakaribia nusu mwaka akiwa na video moja mkononi, aliyekuwa mshindani wake mkubwa, Hanscana ameshatoa video 13 tangu kuanza mwaka huu.
Hanscana ameshatoa video kama Phone ya Ben Pol, Ollah ya Christiana Bella, Up In The Air ya Rose Ree, Sugar ya Mimi Mars, Kijuso ya Queen Darling, Kibabe ya Prof Jay, Shauri Yako ya Edu Kenzo, Down ya Quick Rocka, Ila ya Foby, Umenikamata ya Jux, Happy BithDay ya Harmonize, Hasara Roho ya Darassa, na Ukivaaje Utapendeza ya Dogo Janja.
Bila uoga naweza kusema Hancana kwa sasa amelishika soko la ndani, ni jambo zuri ambalo anastahili pongezi, tangu kuanza kwake hakuna alipopotea, ameendelea kushikilia mafanikio yake. Weka nukta hapo kwanza.
Nisher alifanikiwa sana kuleta ushindani mkubwa katika uongozaji wa video nchini. Kwa kipindi kifupi alichokuwepo katika game ilifika wakati watu walianza kumlinganisha na director mkongwe Adam Juma ambaye alileta mapinduzi makubwa katika utengenezaji wa video za muziki nchini.
Nisher alidumu kwenye game kwa kipindi kifupi sana lakini mchango wake mkubwa bado unaonekana. Alikuwa ni mwenye kujituma, mbunifu na mwenye vifaa vya kutosha, kiufupi si mtu wa mchezo mchezo. Leo hii yupo kimya, anajaribu kurudi kwenye game ambapo mapambano yamepamba moto.
Amekuwa akijaribu kurudi lakini amekuwa akikwamishwa na baadhi ya mambo. Huenda ‘ugonjwa’ unaomkwamisha Nisher kurejea ni kama ule unaokumbana nao Alikiba anapopamba kuirejesha nafasi yake katika Bongo Fleva (ufalme).
Nisher kuna kipindi alipumzika kufanya kazi kwa kuchukua mapumziko nje ya nchi, na pia alibainisha kuwa alifanya hivyo ili kupata muda wa kuwa karibu na mchumba wake. Unajua alipotaka kurudi nini alikumbana nacho?.
Chukua huu mfano, Alikiba alipoamua kupumzika kufanya muziki kwa kipindi cha zaidi ya miaka miwili, aliporejea alikuta Diamond Platnumz ameshasimamisha ufalme wake, hivyo kazi ikawa kubwa mara mbili. Mosi; kurejesha muziki wake ambao ulikuwa hujasikika kwa muda, pili; kupambana na utawala alioukuta.
Alikiba amefanikiwa kurejesha muziki wake ila itamchukua muda kuondoa utawala ambao ameukuta, utawala ambao kipindi anaamua kupumzika kufanya muziki, haukuwepo.
Hii ndio hali anayokumbana nayo Nisher anapotaka kurejea, wakina Hanscana, Khalfan na wengineo wameshasimika utawala wao, hivyo kazi ya kurejea ni kubwa si kitoto.
Twende mbele turudi nyuma, vyote vyote itakavyokuwa bado mchango wake unahitajika katika game, lakini kama ni hivyo mbona hapati nafasi?. Sababu ni hizi
Biashara na Weusi kuanguka
Katika wimbo ya Nako 2 Nako Soldiers ‘Hawatuwezi’ ambao wamefanya Lord Eyes, Ibra Da Hustler na Enika, kuna mstari Lord Eyes anaseme ‘Yule aliyetupandisha ndiye atakayetushusha’.
Kama nilivyotangulia kueleza kuwa tulianza kumfahamu Nisher kupitia Joh Makini, pia umaarufu wake kwa asilimia fulani ulichochewa na video alizokuwa anafanya na Weusi.
Weusi walipoanza kwenda kufanya video nje ya nchi, biashara na Nisher kwa kiasi fulani ilishuka, kitu kilichoanza kuondoa ushawishi wa kikazi aliokuwa nao kwenye game.
                                    Nisher alipokuwa akishoot video ya Joh Makini ‘XO’
Kilichoashiria anguko kubwa la kibiashara kati yao ni utata uliojitokeza katika video ya Arosto ambayo mwanzoni aliifanya Nisher lakini baadae G Nako akaja kutoa ya pili ambayo aliifanya kwa Hanscana.
Tunaweza kusema Weusi wamekinai huduma kutoka kwa Nisher, kama nitakuwa nimekosea nafasi ya kurekebisha ipo wazi. Kwa mujibu wa Nisher video ya Arosto pamoja na nyingine tatu ndizo zilikuwa katika mipango yake ya kumrejesha katika game.  Lakini hilo halikufanikiwa kitu ambacho naamini kimemnyima hata nguvu ya kuendelea kwa kasi aliyokuwa nayo mwanzo.
Kabla ya ujio huu wa sasa niliwahi kufikiri kuwa Nisher ameamua kuachana na utengenezaji wa video za Bongo Fleva baada ya kuona vipande vya movie yake aliyoipa jina la Alex katika mtandao, lakini sivyo bado jamaa anaiona nafasi yake katika game.
Maneno nje ya kazi
Hii huenda ikawa sababu ya pili kupotea kwa Nisher na itakayo kwamisha kufana kwa ujio wake. Sote tunafahamu tabia yake si mtu wa kuficha hisia zake, kama kitu anakijua atakuambia anakijua, kama kitu anacho atakuambia anacho wala hatokudanganya.
Falsafa zake ni kama za Rais John Magufuli, kama kitu ni cheupe atakueleza uhalisia wake, hawezi kukuambia ni rangi ya maziwa. Ndivyo alivyokuwa Nisher na watu wenye tabia hii mara nyingi ni watu wachache wanaoweza kuwaelewa. Kama unabisha, fuatilia changamoto anazokumbana nazo Rais wa Marekani kwa sasa, Donald Trump.
Nisher alikuwa haoni haya kukueleza kiasi cha fedha ulichonacho sitoweza kufanya kazi yako kwa sababu familia yake inajimudu kiuchumi. Jambo hili lilifanya watu wengi kuamini kuwa jamaa anaringa.  Kiufupi Nisher ni mtu wa kunyoosha maneno na ndio maana hakuogopa kutamka hadharani kuwa G Nako amemuingizia hasara ya sh. milioni tatu kwenye video ya Arosto.
Kuna kipindi prodyuza Samtimber wa Arusha alilalamika kuwa Nisher anamletea dharau katika kazi. Samtimber alienda mbali zaidi kwa kudai Nisher alikataa kufanya video ya wasanii waliorekodi studio kwake kwa madai audio ni mbuvu.
Unakumbuka kipindi walikuwa wanavutana na B.O.B micharazo kuhusu masuala ya kazi, stori za chini ya kapeti zikadai kuwa jamaa alikataa kufanya video ya kundi hilo la Hip Hop ili kulinda utawala wa Weusi katika game kwa kutoa video kali. Kiufupi hayo ndio yalikuwa maisha ya Nisher kwenye game.
Purukushani kama hizi na zile nilizotangulia kuzieleza huenda zilichangia kumpoteza Nisher kwenye game. Sasa sijaelewa hapa anayepaswa kulaumiwa ni Nisher mwenyewe au ni watu wa karibu aliokuwa anafanya nao kazi.
Endapo akifanikiwa kuruka vizingiti hivi viwili nina amini Nisher atarejeza vizuri zaidi na kulishika soko upya kama ilivyokuwa hapo awali
Anachopaswa kufanya Nisher
Binafsi bado nimaamini katika uwezo wa Nisher na nafasi yake katika game ipo pale pale, ni kitendo cha yeye kujipanga upya na kutafuta nafasi ya kufanya kazi na wasanii ambao wapo mainstream kwa sasa kama alivyoanza.
Licha ya kuwa wasanii wa aina kwa sasa wanakimbilia nje kufanya video lakini bado kuna uwezekano wa hata yeye kuongozana nao kwenda huku huku kufanya kazi. Bila hivyo ni vigumu kurejea kwa kasi ile.
Hanscana alisafiri hadi Kenya na Christian Bella kufanya video ya Ollah, hii ikiwa ni ishara kuwa jamaa anahitaji kukua zaidi. Unaweza kudharau hatua hiyo lakini kipindi cha nyuma wasanii wengi wa Bongo Fleva walikuwa wanakimbilia Kenya kufanya video na Ogopa DJs.
Ommy Dimpoz, Rich Mavoko, Madee, Chenge na Temba kwa nyakati tofauti walisafiri na Adam Juma hadi Afrika Kusini kufanya video, utamaduni huu ingeendelezwa ungesaidia madirector wetu kuwepo kwenye game kwa kipindi kirefu na kujulikana mbali zaidi.
Nisher akitaka kurejea atafute nafasi ya kuenda kufanya video nje ya nchi, kazi za ndani asizipe nafasi sana, endapo akifanikiwa nje ni rahisi kuliteka soko la ndani upya.

Thursday, April 6, 2017

Jifunze haya toka kwa Bilionea aliyekataliwa mara nyingi zaidi

Tujifunze kutoka kwa ‘Ma Yun’ maarufu kwenye ulimwengu wa biashara ya mtandao kama Jack Ma. Bilionea kutoka China mwanzilishi na mwenyekiti mtendaji wa Alibaba Group, moja ya familia ya biashara ya mtandao iliyofanikiwa zaidi duniani
Jack Ma ni mtu wa kwanza kutoka China (Mainland China) kuonekana kwenye kurasa ya mbele ya jarida maarufu la Forbes. Mwaka 2014 dunia ilishuhudia IPO (Initial Public Offering- kuuzwa kwa mara ya kwanza kwa hisa za kampuni kwenye soko la hisa) kubwa zaidi kuwahi kutokea duniani kwenye soko la hisa la Newyork, na kuifanya Alibaba group kuweka rekodi kama world’s biggest public stock offering.
Pamoja na kupingwa mara kwa mara kuwa Alibaba hawaweki nguvu ya kutosha katika kuzuia udanganyifu wa mauzo kwenye mtandao wa Alibaba, Ma bado anaipeleka Alibaba kwenye mauzo ya hali ya juu na mafanikio makubwa. Rekodi ya shughuli za kibiashara zipatazo $463 bilioni zilifanyika kupitia mtandao wa Alibaba mpaka mwezi machi 2016.
Kampuni ya Alibaba imeweka malengo ya kutengeneza biashara zenye faida milioni 10 na si chini ya ajira milioni 100 kwa miaka 20 ijayo.
Mafanikio sio ajali. Haikumchukua Jack Ma usiku mmoja kufikia hatua hii kubwa na inayoshangiliwa kila kona ya dunia. Ilimgharimu mapambano na kukataliwa mara kadhaa lakini alisonga mbele.
Ma alianza kujifunza Kiingereza katika umri mdogo na kwa bidii ya hali ya juu, na hapo ndipo alipopata jina la “Jack” baada ya rafiki wa kigeni kushindwa kutamka jina lake la kichina. Akiwa kijana mdogo, Ma alihangaika kuingia chuo kikuu. Mitihani ya kujiunga na chuo kikuu hufanyika mara moja kila mwaka nchini China na ilimchukua Jack Ma miaka minne kufanikiwa, akajiunga kusoma digrii ya kiingereza-B.A in English (Jinsi gani Ma alipenda kiingereza).
Baada ya kumaliza chuo Jack ma aliomba kazi 30 tofauti bila mafanikio, zote alikataliwa. “Niliomba kazi ya upolisi; wakasema ‘wewe sio mzuri kwa kazi hii” Ma alimwambia mwanahabari Charlie Rose. KFC walivyoenda kwa mara ya kwanza kuanzisha biashara kwenye mji anaotoka Ma, Watu 24 waliomba kazi, 23 walifanikiwa kupata kazi. Alikuwa ni Jack Ma peke yake ambaye alikosa kazi hiyo. Lakini pia Ma aliomba kujiunga na chuo kikuu cha Harvard mara kumi na mara zote alikataliwa.
Maisha ya Jack ma ni ushahidi mwingine mkubwa wa bilionea aliyekutana na vikwazo na kukataliwa mara nyingi zaidi, lakini hakukata tamaa. Moja ya misimamo mikuu katika maisha yake ni kuzoea kukataliwa (Get used to rejection) na kuendelea kuifanya ndoto yako iishi (Keep your dream alive). May 2015 kwenye kituo cha televisheni cha KBS cha nchini Korea ya kusini, Ma alizungumza na vijana na wajasiriamali wadogo na kuwapa maneno yenye nguvu kubwa mno kwenye maisha yao , alisema ; Usiogope kila kosa unalofanya ni kipato kwako, kabla ya miaka 20 kuwa mwanafunzi mzuri, jifunze kwa nguvu. Kabla ya miaka 30 kuwa mfuasi wa mtu mwenye mafanikio, mwenye uzoefu na anayefanya vizuri kwenye maisha yake, nenda kwenye kampuni ndogo ndogo, mara nyingi kwenye kampuni kubwa ni kama unakuwa part of the big machines. Lakini ukienda kwenye kampuni ndogo ndogo unajifunza kuwa na shauku, unajifunza kuhusu ndoto zako. Unajifunza kufanya vitu vingi kwa wakati mmoja. Kitu muhimu kabla ya miaka 30 sio kampuni gani uliyofanyia kazi, lakini ni bosi wa aina gani umekuwa chini yake. Hii ni muhimu sana, kwasababu kila bosi anakufundisha tofauti.
Ukiwa chini ya miaka 40 unahitaji kuchukua muda wako na kujiuliza kwa makini sana, kama unataka kufanya kazi kwaajili yako na kama kweli unataka kuwa mjasiriamali. Miaka 40 mpaka 50 hakikisha unafanya vitu ambavyo una uwezo navyo na unavijua zaidi, sio muda wa kujaribu tena. Weka malengo na maisha yako, kama Mungu atakupa uhai ukafika miaka 60 wekeza kwa vijana, fanya kazi na vijana kwasababu wao wana nguvu kuliko wewe, wanafikiri vizuri kuliko wewe. Ukiwa ndani ya miaka ya ishirini fanya makosa mengi, fanya makosa kadri ya uwezo wako kwa lengo la kujifunza zaidi.
Haijalishi ni mara ngapi umejaribu ukashindwa na kukataliwa, usiache kusonga mbele, unahitaji kufanikiwa mara moja tu kwenye maisha yako. Unahitaji kutengeneza uvumilivu mkubwa na hali ya kutokukatisha mambo yako (Procrastination). Jifunze zaidi katika umri mdogo kuliko kufikiria kulipwa pesa nyingi tu, work to learn and money will follow you. Tembea na ndoto zako popote uendako na uzifanyie kazi kila siku bila kuchoka wala kukata tama mpaka pale ushindi wako utakapotengeneza historia kama Jack Ma na Alibaba.

Monday, April 3, 2017

nchi 12 duniani zenye wafanyakazi wengi wa kike wenye elimu kubwa

Wanaharakati mbalimbali wa Haki za Wanawake duniani wanapambana kuhakikishaWanawake wanakuwa katika nafasi nzuri kazini, shuleni na popote inapowezekana ili kuwainua kiuchumi, kisiasa, kijamii na kiutamaduni.
April 2, 2017 nimekutana na stori hii  ambayo inahusu nchi zenye wafanyakazi wengi wa kike wenye kiwango cha juu zaidi cha elimu duniani ambapo Canada ikitajwa kuwa kinara kwa kuwa na wafanyakazi wa kike wenye elimu kubwa zaidi duniani.
Hizi hapa nchi 12 ambazo zina wafanyakazi wa kike wenye elimu kubwa zaidi duniani.
NafasiNchi% ya wafanyakazi wa kike wenye elimu kubwa
1Canada58%
2Cyprus50%
3Estonia50%
4Ireland49%
5Ubelgiji48%
6Luxembourg48%
7Lithuania47%
8Finland47%
9Norway47%
10Sweden44%
11Uingereza43%
12Uhispania42%

Thursday, March 23, 2017

Ijue haki yako unapokamatwa na polisi

1. Askari akikuweka chini ya ulinzi muulize kitambulisho ni haki yako.
2. Askari akikukamata akuoneshe kitambulisho chenye muhuri wa mahakama kama anasema ametumwa na mahakama kukumata, ni haki yako.
3. Askari akikukamata akwambie kwanini anakukamata na anakupeleka kituo gani, ni haki yako.
4. Unaruhusiwa na sheria kukataa kukamatwa hata kutumia nguvu kama hukuambiwa sababu ya kukamatwa.
5. Askari anapokiuka taratibu za ukamataji anageuka na kuwa mhalifu ni haki yako kujikinga naye.
6. Askari haruhusiwi kukuvuta shati, kukukaba koo, kukushika suruali kama hujakataa kukri amri halali.
7. Askari haruhusiwi kuondoka na mtu mwingine baada ya kumkosa mtuhumiwa halisi.
8. Askari haruhusiwi kupekua nyumba ya mtu bila kibali cha kupekua.
9. Askari lazima akuoneshe kibali cha kupekua na ukisome.
10. Kibali kieleze jina la aliyekitoa, kituo kilipotolewa,jina la mtu au sehemu ya upekuzi, au uchanganuzi wa mtu au sehemu.
11. Hairuhusiwi kupekuliwa usiku kuanzia saa 1 jioni mpaka saa 12 asubuhi.
12. Ni haki yako kumpekua askari kabla hajakupekua ili asipandikize kitu.
13. Usipekuliwa nyumbani bila kuwapo kiongozi wa mtaa.
14. Kila kitakachochukuliwa katika upekuzi lazima kiandikwe na askari aweke sahihi.
15. Mali iliyochukuliwa katika upekuzi lazima ibaki salama.
16. Mwanaume haruhisiwi kumpekua mwanamke na mwamke haruhisiwi kwa mwanaume.
17. Unaruhusiwa kukataa kupekuliwa iwapo taratibu hizi hazikufuatwa.
18. Askari haruhusiwi kukutukana wala kukupiga.
19. Unaruhusiwa kutozungumza lolote mpaka unayemuamini afike uwapo chini ya ulinzi, ni haki yako.
20. Usilazimishwe kuongea au kuandika ambacho hutaki, ni haki yako.
21. Usitoe maelezo bila uhakika yatatumika mahakamani yatakuletea shida.
22. Unaruhusiwa kukaa kimya na usizungumze kitu uwapo chini ya ulinzi.
                                       HIZI ZOTE NI HAKI ZAKO, ZILAZIMISHE USIBEMBELEZE WALA USIZIOMBE.