MICHAKATO

Levis Rocky Ndekeno

This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Pages

Monday, May 23, 2016

Siku 200 kwa Rais Magufuli kuiongoza Tanzania

Leo rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Magufuli ametimiza siku 200 tangu ameapishwa kuwa rais wa awamu ya tano kuiongoza Tanzania.

Tangu alipoapishwa Novemba 5 kwenye uwanja wa Uhuru na kuanza kazi siku hiyo hiyo aliyoapishwa, rais Magufuli amekutana na changamoto kadhaa zilizofanya uchumi wa nchi usikuwe kwa kasi inayotakiwa.
‘Hapa Kazi Tu’ ndiyo ulikuwa msemo wa rais Magufuli kwenye kampeni zake za kuwania urais lakini baadhi ya watu walidhani hayo yalikuwa ni maneno lakini kwenye utekelezaji wake wa vitendo usingeweza kufanya kazi kutokana na mizizi iliyopandikizwa tangu hapo awali.
Disemba 4 mwaka jana, Magufuli alifanya mkutano na wafanyabiashara na kuwapa siku saba wale wote waliopitisha makontena yao bandarini bila ya kuyalipia kodi ikiwa ni zaidi ya makontena 1300 yalipitishwa bila ya kulipiwa kodi.
Rais Magufuli ameweza kujitahidi kupunguza baadhi ya matumizi yasiyokuwa ya lazima kwa watu wachache na fedha zake kuzipeleka kwenye vitu vya msingi vyenye manufaa kwa wengi.
Hakika serikali ya Magufuli ina safari ndefu ya kupambana mpaka kumaliza awamu ya kwanza ya uongozi wake. “Kuanzisha mahakama ya mafisadi” ndiyo ilikuwa moja ya ahadi ya rais Magufuli aliyoitoa wakati wa kuomba kura kwa wananchi za Urais.
Rais Magufuli akiwa kwenye mapumziko nyumbani kwao, Chato alisema, “kama kule Dar es Salaam kuna mfanyakazi mmoja wa TRA analipwa mishahara hewa ya wafanya kazi 17.” Mpaka sasa agizo la rais kwa Wakuu wa Mikoa limetekelezeka kwa asilimia kubwa na kubaini zaidi ya watumishi hewa 2500 huku bado zoezi la uhakiki likiendelea zaidi.
Watumishi kadhaa mpaka sasa wamekutana na rungu la rais Magufuli na amefanikiwa kuwatumbua kutokana na oparesheni yake ya ‘Tumbua Majipu’ akiwemo aliyekuwa mkuu wa Mkoa wa Shinyanga [Anne Kilango], Waziri wa Mambo ya Ndani [ Charles Kitwanga], Mkurugenzi wa TIC [Juliet Kairuki], na wengine kibao.
Tatizo la sukari kwa sasa ndiyo changamoto kubwa inayokabiliana nayo serikali ya awamu ya tano huku baadhi ya maeneo sukari ikionekana kuuzwa kati ya shilingi 2500 mpaka 4000 kwa kilo moja.
Lakini wiki iliyopita Waziri Mkuu alizungumzia suala hilo bungeni na aliahidi serikali bado inalifanyia kazi tatizo hilo huku tukiendelea kusubiri tani elfu hamsini ambazo serikali imeziagiza nje ili zije kuziba tatizo la sukari lililopo nchini.
Hakuna binadamu aliye mkamilifu, kuna baadhi ya mambo rais Magufuli ameweza kuteleza kama binadamu lakini kwa kiasi kikubwa ameweza kuiongoza safari ya jahazi la Tanzania ipasavyo na kuwaacha midomo wazi wale walioamini kuwa hawezi.

Wednesday, May 18, 2016

Picha: Meli kubwa zaidi duniani yakamilika

Meli kubwa zaidi duniani imekamilika ikiwa na ukubwa wa viwanja vinne vya mpira wa miguu.
Meli hiyo iliyopewa jina la ‘Harmony Of The Seas’ imechukua miezi 32 mpaka kumaliza kutengenezwa. Ina vyumba 2747, mabwawa 23 ya kuogelea, hoteli na bar, sehemu za michezo, viwanja vya helkopta lakini pia ina uwezo wa kuchukua abiria 6780.








 Aidha gharama za kusafiri na meli hiyo ni £900 lakini kuingia mpaka sehemu za starehe inagharimu £2,760 kwa mtu mmoja. Watengenezaji wa meli hiyo wamesema ‘Harmony Of The Seas’ ni meli yao ya 25 kwenye kampuni Royal Caribbean International fleet.

Twitter yafanya mabadiliko makubwa

Mtandao wa kijamii Twitter yafanya mabadiliko makubwa  katika namna inavyohesababu herufi za tweets na hivyo kuwapa watumiaji uhuru wa kuandika ujumbe mrefu zaidi. Hivi karibuni itaacha kuhesabu picha na link kama sehemu ya herufu 140 za kikomo cha ujumbe unaoandikwa. Mabadiliko hayo yanaweza kuanza kuonekana katika wiki mbili zijazo.


Tuesday, May 17, 2016

WhatsApp inajiandaa kuja na huduma ya ‘video call’

WhatsApp inatarajia kuanzisha huduma ya mawasiliano ya video.
Hivi karibuni iliweka version ya majaribio kwa watumiaji wachache lakini imeitoa kwaajili ya kuifanyia marekebisho zaidi.
Video calling kwa WhatsApp imekuwa ikifanyiwa kazi kwa takriban miezi sita sasa ambapo December mwaka jana screenshots za version ya iOS ya app hiyo ilivuja ikionesha huduma hiyo.
Na sasa huduma hiyo iko mbioni kutambulishwa kwa watumiaji wa app hiyo duniani kote. Wikiendi iliyomalizika baadhi ya watumiaji waliripoti kuwa option ya WhatsApp ilipatikana kwenye beta version 2.16.80.

list za juu za nchi zisizokuwa waaminifu Tanzania ikiwepo


Utafiti umefanywa na wanafunzi wa University of Nottingham Uingereza ukihusisha nchi 159, wanafunzi wa chuo kikuu cha Nottingham wamefanya utafiti wa kugundua ni nchi zipi zinaoongoza kwa uaminifu au ukweli duniani, utafiti umefanywa ukihusisha nchi 159 ikiwemo Tanzania.Wanafunzi hao wamefanya tafiti huku wakichanganya na data za 2003 za ukwepaji kodi, rushwa na udanganyifu katika siasa lakini wamegundua kuwa nchi za Lithuania, Uholanzi, Uingereza, Sweden, Ujerumani na Italia zimetajwa katika list ya nchi zinazoongoza kwa uaminifu.Wakati nchi za Tanzania, China, Uturuki, Poland na Morocco zimetajwa kuwa ni miongoni mwa nchi zinazoongoza watu wake kutokuwa waaminifu, utafiti huo unaeleza kuwa watu wanaoishi katika nchi zenye rushwa na siasa za udanganyifu wamekuwa sio waaminifu au wakweli, wakati watu wanaotokea katika nchi ambazo hazina rushwa na ukwepaji kodi ni waaminifu.Tafiti zimefanyika katika chuo kikuu cha Nottingham Uingereza, lakini kimetajwa kufanya majaribio kwa kuhusisha vijana 2,586 wenye wastani wa umri wa miaka 22 kutoka nchi 23 zikiwemo Vietnam, Morocco, China, UK, Hispania, Sweden, Italy na Czech Republic. Utafiti huu umetolewa na dailyamail.co.uk March 11 2016.
IMEANDIKWA : dailymail.co.uk

Thursday, May 12, 2016

Ukata wa Pesa: Walimu walipwa vifaranga badala ya mshahara

Wakati nchini Tanzania walimu wakiomba kuongezewa mishahara, Mji mmoja nchini Uzbekistan umekua ukiwapa waalimu wake kuku kama mshahara badala ya pesa.Mamlaka za mji wa Nukus katika jimbo linalojitawala la Karakalpakstan wamekua wakitia vifaranga wachanga kwa walimu kutokana na uhaba wa pesa nchini humo. Kituo cha radio kinachofadhiliwa na Marekani{Radio Ozodlik} kimemnukuu mwalimu mmoja akilaani hatua hiyo kama aibu kubwa kwa mamlaka. Mwalimu huyo aliyeghadhabishwa na hatua hiyo amesema hataki vifaranga kwa sababu anaweza kuwapata sokoni, lakini wanataka pesa zao. Vifaranga wanaotolewa kama mshahara wana gharama ya dola mbili kila mmoja, ikiwa ni maradufu bei inayouzwa vifaranga sokoni. Mamlaka za Uzbekistan hazikubalii uhuru wa vyombo vya habari na raia wa huko hutegemea vyombo vya habari vya kimataifa kutoa sauti yao, ila hawajitambulishi. Uzbekistan imekumbwa na uhaba wa fedha kwa miaka sasa hali inayosababisha serikali kuchelewesha mishahara ya wafanyikazi na malipo ya uzeeni. Mapema mwezi huu wafanyikazi wa serikali katika mji mkuu,Tashkent walilalamikia kwamba hawakuwa wamelipwa mshahara kwa miezi miwili kwa sababu benki hazikuwa na pesa.

Instagram kuanza kutumia nembo mpya

Instagram imezindua nembo mpya katika hatua ya kutaka kujiboresha na kutoonekana kuwa programu ya picha pekee.Nembo hiyo imetengezwa kuimarisha ujumbe unaotumwa. Nembo hiyo inaonyesha kamera ya kawaida na rangi za upinde wa mvua. Zaidi ya picha milioni 80 na video husambazwa kila siku katika mtandao wa Instagram, mtandao huo una takriban wateja milioni 400 na uliipiku Twitter mwaka 2014. Viongozi wa mtandao wa Instagram waliiambia Newbeat, “Wakati Instagram ilipokuwa inaanza ilikuwa na eneo la kukarabati na kusambaza picha. Miaka mitano baadaye likawa ni eneo linalopendwa na jamii kubwa ulimwenguni ambapo watu husambaza picha na video.” Watumiaji pia watagundua kwamba eneo la bluu katika nembo ya mtandao huo limeanza kubadilika na kuwa jeupe. Mtindo huo mpya una lengo la kuimarisha picha na video zinazotumwa bila kubadilisha unavyoingia katika mtandao huo. Ubunifu wa nembo hiyo mpya ulianza mwaka mmoja uliopita. Aidha walitaka kutengeza nembo ambayo ingewakilisha mahitaji ya awali ya sasa na ya siku za baadaye.

Monday, May 9, 2016

Lady Jaydee kuwasha moto kwenye ‘Naamka Tena Concert’ May 20

Kwenye tamasha hilo litakalofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City, Jaydee atatumbuiza pamoja na bendi yake.
Hiyo itakuwa ni show yake kubwa zaidi tangia atumbuize June 2013 kwenye show ya kihistoria ya miaka 13 kwenye muziki kipindi ametoa album yake ‘Nothing But The Truth.’
Hivi karibuni Jaydee aliachia kazi mpya inayotamba kwa sasa, Ndindindi ambayo itakapatikana kwenye album yake mpya, Woman.

Gadner G Habash kwa hili umeteleza kaka

Huwa nakuwa mzito sana kumshauri mtu anayenizidi umri, uwezo, status na tena ninayemchukulia kama moja wa role models wangu. Pale ambapo nitahitajika kufanya hivyo kutokana na uzito wa jambo lenyewe, huamua kutumia keyboard ya computer kuyasema yale ambayo naamini kwa uelewa wangu yanaweza kumjenga pia lakini nikiyasema kwa staha ya hali ya juu.
Gadner G Habash ni miongoni mwa watangazaji wa redio ninaowaheshimu katika muda wote. Si tu kwasababu ni mtangazaji mkongwe, bali pia ni mtangazaji mwenye sauti ya pekee hewani na mwenye busara inayoweza kuhamisha milima. Anapokuwa anaongea jambo, mamlaka anayoyaweka kwenye sauti, hukufanya kila neno limtokalo mdomoni likuingie vyema masikioni.

Na kwa hakika tangu aachane na mke wake, Lady Jaydee, amekuwa akijibu maswali yanayowahusu kwa werevu mkubwa. Miongoni mwa interview yake iliyonivutia sana ni ile aliyofanya na Zamaradi Mketema kwenye kipindi cha Take One cha Clouds TV.
“Siwezi kusema najuta kwamba [Jaydee] alitokea kwenye maisha yangu na siwezi kusema kwamba najuta tuliachana. Lakini ninachoweza kusema tu kwamba kwa suala la Jaydee ni suala ambalo nilichagua sana lisiwe ni jambo ambalo nalizungumzia au kulitolea comment kwasababu yule ni public figure unaposema kitu kuhusu yeye tafsiri zinakuwa ni tofauti na vile unavyotarajia,” alisema Gardiner.
“Kwahiyo sina majuto yoyote, na sina aina yoyote ya chuki au uadui na nategemea hata yeye atakuwa anafeel the same,” alisisitiza.
Pia nilipenda majibu yake ya maswali kuwa Ndindindi ni wimbo alioandikiwa na ex wake huyo.
Hadi hapo niliendelea kuamini kuwa mtangazaji huyo ameufunga ukurasa wake na Lady Jaydee kwa amani na kila mmoja ameangalia hamsini zake, maisha yanaendelea. Sishangai kabisa kama ukweli halisi ni kwamba wawili hao wanachukiana baada ya kuachana kwasababu ni kitu cha kawaida. Na mara nyingi chuki huwa kubwa pale pendo linapochanganyikana na chuki na hasira ya kutendwa au kwasababu yoyote ile inayomfanya mmoja wapo kukatisha uhusiano kwa kosa la mwingine.
Lakini nashangaa sana kwa mtu smart kama Gardiner kutamka maneno ya kumdhalilisha ex wake mbele ya kadamnasi. Kuna video imesambaa na naamini itakuwa viral sana wiki hii inayomuonesha mtangazaji huyo akiwa jukwaani kama mshereheshaji wa tukio moja jijini Dar es Salaam akiongea maneno makali kumhusu ex wake ambaye licha ya kutomtaja inajulikana wazi alikuwa anamuongelea nani.
“My name is Captain Gardiner G Habash all the way from Clouds FM, Jahazi hatari sana,” anasikika akisema kwenye kipande hicho cha video. “Na sina neno na yule mtoto wa kike. Nimeshamkojoza kwa miaka kama 15 hivi,” anasema Gardiner na kisha Dj anaucheza wimbo wa Lady Jaydee, Ndindindi. Mtangazaji huyo anaonekana kuucheza pia wimbo huo jukwaani huku watu wakimshangilia.
Nimependa ujasiri wa Gardiner katika kulisema jambo hilo na kudhihirisha kwa mara nyingine tena kuwa hana tatizo na ex wake lakini sijapendezwa na uchaguzi wake wa maneno. Kimsingi ni clip ambayo kwa namna nyingi inamdhalilisha ex wake lakini pia inamuondolea Captain ile busara ambayo najua anayo.
Sijachachagua kuiweka clip hiyo hapa kutokana na kilichosemwa lakini ningemshauri kaka yangu Gardiner kuendelea kusimamia busara yake aliyonayo siku zote na kujiepusha na kauli tata kama hizi ambazo mara nyingi huwa zina madhara kwenye brand. Video hiyo haijamdhilisha Jide tu bali wanawake wote ambao kwa hakika kwa kauli yake inawaelezea kama ni vyombo vya starehe tu.
Na utashangaa jinsi ambavyo video fupi kama ile ikaondoa heshima ya Gardiner aliyoitengeneza kwa muda mfupi. Matusi anayotukanwa sasa kwenye ukurasa wake wa Instaram yanatoa jibu la ni kwa kiasi gani watu hawajapendezwa na kauli zake. Pia ni kauli mbaya katika kipindi hiki ambacho amerejea kwa kasi Clouds FM kukalia kiti chake kilichoshindikana kukaliwa na watangazaji wengi.
Bahati nzuri binadamu husahau mapema, yataisha tu lakini ni vyema Captain akawa mwangalifu na kauli zake katika siku za usoni sababu ‘kile kinachotokea au kusemwa kwenye starehe hakibaki hapo tu.’

Nauli za Mabasi yaendayo haraka ziko hapa, siku mbili bure

Baada ya Kampuni ya UDA-RT kuwasilisha maombi ya nauli zitakazotumika kwa mabasi yaendayo haraka kwa Mamlaka ya udhibiti usafiri wa nchi kavu na majini (SUMATRA) May 09 206 SUMATRA imetangaza nauli hizo.
SUMATRA imesema kuwa njia ya pembezoni (Freeder Route) nauli ya mtu mzima ni 400 na mwanafunzi 200 na njia kuu (Trunk Route) ni 650 na mwanafunzi 200 na kwa abiria atakayetumia kusafiri njia kuu (Freeder Route) na kuendelea na safari kwa njia ya pembezoni nauli yake itakuwa ni 800 na mwanafunzi 200. 
Huduma hiyo itatolewa kuanzia kesho bure kwa wananchi kwa siku mbili na May 12 2016 zitaanza kutozwa nauli zilizotajwa.
Msimamizi wa mradi kutoka DART, Eng Ronald Lwakatare amesema>>>‘Wakati huo tunafanya majaribio tutakuwa tunaangalia mfumo unavyofanya kazi kwa hiyo tutawabeba abiria kwa siku kadhaa bila kulipa nauli’

Rais Magufuli asema yeye siyo katili, anawatumikia Watanzania ili kurejesha nchi kwenye mstari

Rais John Magufuli amewataka Watanzania wasimuone katili kwa kuwafukuza kazi baadhi ya watendaji wa Serikali, kwakuwa anataka kuirejesha nchi kwenye mstari.Akizungumza katika misa ya Jumapili kwenye Kanisa Katoliki Parokia ya Tokeo la Bwana Burka jijini Arusha, Rais Magufuli alisema watu katili ni wale ambao walikuwa wanawaibia Watanzania na kuwanyonya wanyonge.
Dk Magufuli alisema analazimika kuchukua hatua ya kuwafukuza kazi si kwamba ni katili, bali lengo ni kuwatumikia Watanzania na kuirejesha nchi kwenye mstari.
Alisema Tanzania ni taifa tajiri, hakuna sababu ya wananchi kulalamika kila kona, kwani kuna ardhi ya kutosha, madini ya kila aina, wanyama wa aina mbalimbali ambao baadhi wameanza hadi kupelekwa nje.
“Ninapochukua hatua nataka kuweka Tanzania iliyonyooka, mimi tayari nimesema nimejitoa sadaka kwa Watanzania hasa wanyonge,” alisema.
Aliongeza kuwa hatawaangusha Watanzania na hatabadilika, ataendelea kusimama na kutetea haki za Watanzania maskini na siku zote atatembea na maskini.

Mrisho Mpoto apata shavu la ubalozi wa kampeni ya ‘Kili Challenge’

 Msanii wa muziki wa asili, Mrisho Mpoto amepata shavu jipya la kuwa balozi wa kampeni ya ‘Kili Challenge’ itayokuwa inaelimisha jamii kuhusu kuendeleza mapambano dhidi ya Ukimwi.
Kupitia instagram, Mpoto ameandika:


Mgodi wa dhahabu wa Geita (GGM) kwa kushirikiana na Tume ya kupambana na kudhibiti Ukimwi nchini (TACAIDS) imeniteua kama msanii na mtanzania kuwa Balozi wa Kampeni ya Kili Challenge.
Napenda kuwashukuru sana TACAIDS na GGM kwa kuniamini na kunipa fursa hii ya kipekee.
Naomba nitoe wito kwa watanzania na waafrika wote kuwa tuendelee na mapambano dhidi ya Ukimwi. Tuzungumze na tuchukue hatua dhidi Ukimwi ili tufikie lengo la Kampeni ikiwa kama lengo letu sote tuhakikishe tunafikia idadi ya Zero katika Maambukizi Mapya, Zero ya Unyanyapaa, Zero ya vifo vitokanavyo na Ukimwi.

Picha: Msichana asiye na mikono ashinda tuzo la muandiko bora


 Msichana wa miaka saba aliyezaliwa bila mikono ameshinda shindano la muandiko mzuri nchini Marekani.
Anaya Ellick kutoka Chesapeake, Virginia hatumii viungo vya kumsaidia wakati anapoandika.
Wakati anapoandika yeye husimama huku akishikilia kalamu yake katika mikono.
Mwalimu wake mkuu Tracy Cox kutoka shule ya Greenbrier Christian amemtaja kuwa mtu wa mfano mwema.
“Yeye uhakikisha kuwa hakuna kitu kinachomzuia kufanya atakalo”, alisema Cox.”Ni mkakamavu na ana muandiko mzuri katika darasa lake”.
Msichana huyo anadaiwa kuwashinda washindani wengine 50 ili kushinda taji hilo la kitaifa.
Orodha hiyo ya tuzo huwazawadi wanafunzi wenye akili, matatizo ya kimwili, au ulemavu endelevu




NE-YO kutumbuiza Mwanza May 21


Mwanamuziki nguli kutoka nchini Marekani NE-YO anayetamba kwa muziki wa kizazi kipya anatarajia kufanya ziara nchini mwezi huu kwa mwaliko wa kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania kwa kushirikiana na Jembe Media Limited.Akitangaza ujio wa mwanamuzi huyo, Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu alisema NE-YO atawasili nchini Mei 19 na Mei 21 atatoa burudani ya aina yake katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza kwenye tamasha la Jembeka na Vodacom 2016 liloandaliwa na kampuni ya Jembe chini ya udhamini mkuu wa Vodacom Tanzania.Nkurlu alisema kuwa Vodacom imedhamini ujio wa mwanamuziki huyu kwa ajili ya kuwapatia burudani ya kimataifa wateja wake na watanzania wote kwa ujumla kupitia tamasha lake la Jembeka na Vodacom 2016.“Vodacom tunaamini kuwa wateja wetu wanahitaji kupata burudani baada ya majukumu ya kazi ya kila siku ndio maana tumekuwa tukidhamini michezo na matamasha mbalimbali ya muziki kwa ajili ya kuwapatia burudani kama ambavyo tumefanikisha kumleta NE-YO nchini,” alisema Nkurlu.Aliongeza kuwa mbali na kukonga nyoyo za wapenzi wa muziki NE-YO anayetamba kwa vibao maarufu baadhi yake vikiwa ni Let Me Love You, Beautiful Monster, Coming With You na She Knows featuring Juicy J atashiriki katika shughuli za kusaidia jamii kupitia taasisi ya Vodacom Foundation pia atashiriki katika hafla ya uzinduzi wa duka la Vodacom lililopo kwenye Mall kubwa jijini Mwanza.Aliwataka wasanii wa hapa nchini na wananchi kwa jumla kujitokeza kwa tamasha hilo ili wapate burudani ambapo pia wasanii watapata fursa ya kujifunza mambo mbalimbali na kubadilishana uzoefu na mwanamuziki huyu wa kimataifa.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi wa Tamasha la Jembeka festival 2016, Costantine Magavilla,alisema kuwa wanayo furaha kumleta mwanamuziki NE-YO kwenye tamasha hili na wana imani kuwa wapenzi wa muziki nchini watapata burudani iliyokuwa na hadhi ya kimataifa kutoka kwa msanii huyo.Alisema tamasha la Jembeka na Vodacom litaendelea kufanyika kila mwaka na litakuwa linasambaza burudani za kila aina kwa wapenzi wa muziki na burudani katika kona zote za Tanzania “Wapenzi wa muziki tunawataka wakae mkao wa kula kwa kuwa tutazidi kuuwapatia burudani za muziki wa hapa nchini na wa kimataifa.

Friday, May 6, 2016

Spika Paul Ryan ampinga Donald Trump

Spika wa Republican katika Baraza la Wawakilishi la Marekani,Paul Ryan,amesema hayupo tayari kumuunga mkono Donald Trump kuwa mgombea wa Urais kupitia chama hicho.
Mfanyabiashara huyo bilionea anaonekana dhahiri kushinda katika mbio za uteuzi kukiwakilisha chama hicho lakini Ryan alisema kuwa kabla hakuweza kuidhinisha suala hilo,Na kuwa Trump alipaswa kuwaonyesha watu kuwa anaheshimu taratibu za Republican na angepata kura za Wamarekani wengi zaidi.
Katika kulijibu hilo Trump lisema hakuwa tiyari kuunga mkono ajenda ya RyanMapema Marais wa zamani wa Marekani George W Bush na babaye George Bush waliweka wazi kuwa hawatunga mkono kupita kwa Trump.

Mfanyabiashara Jacob Juma auawa Nairobi

Mfanyabiashara mashuhuri Jacob Juma, ambaye amekuwa akizua mjadala mitandaoni Kenya kutokana na ujumbe wake anaoandika hasa kwenye Twitter, ameuawa kwa kupigwa risasi jijini Nairobi. Taarifa zinasema Bw Juma alipigwa risasi na watu ambao walikuwa wakiendesha pikipiki alipokuwa akielekea nyumbani kwake mtaa wa Karen mwendo wa saa nne usiku. Gari lake lilipatikana na zaidi ya matundu 10 ya risasi.
Kwa mujibu wa gazeti la Daily Nation la Kenya, polisi wanasema hakuna kilichoibiwa kutoka kwenye gari lake. Simu zake mbili na pesa vilipatikana ndani ya gari. Bw Juma alikuwa mwanakandarasi ambaye pia alihusika katika sekta ya uchimbaji madini.

WhatsApp kuja na ‘version’ rasmi ya kwenye computer

Najua kuwa kwa sasa unaweza kutumia WhatsApp kwenye computer yako kwa kuscan code maalum na kuunganisha app ya simu na whatsapp web. Lakini siku zijazo, utaweza kutumia WhatsApp ya kwenye computer inayojitegemea yenyewe, imebainika.Kuna tetesi kuwa WhatsApp itakuja kwenye desktop kwa computer za Mac na Windows katika nia ya kujipanua zaidi. WhatsApp ya kwenye computer itakuwezesha kupiga simu za sauti na video na huduma zingine.Ikianza, hautakuwa na haja tena ya kuscan QR code kujiunganisha na browser yako. Hatua hii itakuwa huduma mbadala wa huduma kama Slack, Messenger au Skype kwa mawasialino yasiyo kuwa ya maandishi.

Tuesday, April 26, 2016

Lucy Kibaki afariki

Aliyekuwa mke wa rais wa zamani nchini Kenya Lucy Kibaki amefariki. Lucy alifariki katika hospitali ya Bupa Cromwell mjini London. Alisafrishwa hadi mjini Landon wiki moja iliopita kwa matibabu

Sunday, April 24, 2016

Lady Jaydee - NdiNdiNdi (Official Music Video)

Icheck video ya wimbo wa Lady Jaydee ‘Ndindindi’ iliyoongozwa na Justin Campos.

Hii ndiyo maana ya wimbo wa Lady Jaydee ‘Ndindindi’

Lady Jaydee ametoa maana ya wimbo wake ‘Ndindindi’ ambalo lilikuwa ni fumbo lililokuwa linawapa majibu mengi yasiyokuwa na uhakika mashabiki wake.

Wimbo wa ‘Ndindindi’ unazidi kufanya kwenye medi mbalimbali na kumrudisha vizuri Jide aka Binti Komando kwenye muziki wa Bongo Fleva baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu bila ya kuachia wimbo wowote.

Akiongea kwenye kipindi cha FNL, kinachoruka kupitia EATV, Lady Jaydee alisema, “The Ndi mimi ni kitu tori wewe si kitu” lakini pia aliongezea “ili kuleta fleva ya muziki ndiyo nikaiita Ndindindi. Mimi ni kitu na wewe si chochote.”

Friday, April 22, 2016

Mabasi yaendayo kasi yaanza safari zake Dar

Mabasi yaendayo kasi, yameanza kufanya safari zake katikati ya jiji la Dar es Salaam Ijumaa hii.
 Jumla ya mabasi 50 yameingia barabarani. Kwa wewe ambaye hujui njia mbalimbali za mabasi hayo, chini ni sehemu yanapopita.
1) RUTI YA KIMARA- KIVUKONI Mabasi Sita (6). Kati ya mabasi Hayo sita wakati wa Kutoka Jangwani matatu yataenda Kimara na Matatu Kivukoni.
2. RUTI YA KIMARA – KARIAKOO Mabasi Sita (6). Kati ya hayo Matatu yataelekea Kariakoo na Matatu Kimara.
3. RUTI YA UBUNGO – KIVUKONI Mabasi nane (8). Kati ya hayo Mabasi Manne yataelekea Ubungo na Manne Kivukoni.
4. RUTI YA UBUNGO – KARIAKOO Mabasi nane (8). Kati ya hayo Mabasi manne Yataenda Ubungo na Manne yataenda Kariakoo.
5. RUTI YA UBUNGO – MOROCCO Mabasi nane (8). Kati ya hayo Manne yataenda Ubungo Manne yataenda Morocco.
6. RUTI YA MOROCCO – KARIAKOO Mabasi sita (6). Kati ya hayo mabasi Matatu Morocco na Matatu Kariakoo.
7. RUTI YA MOROCCO – KIVUKONI Mabasi nane (8). Kati ya Hayo Mabasi Manne yataenda Moroco na mabasi manne Kivukoni.
DESPATCH PLAN SAA KUMI NA MBILI KAMILI. 1. Kimara Terminal Mabasi Sita (6) 2. Ubungo Terminal Mabasi kumi na mbili (12) 3. Morocco Termial Mabasi kumi na moja (11) 4. Kariakoo Terminal Mabasi kumi (10) 5. Kivukoni Terminal Mabasi kumi na moja (11) JUMLA NI MABASI HAMSINI (50)

Chanzo cha kifo cha Prince chabainika, alitumia madaya ya kulevya kumzidi

Muimbaji, Prince alikuwa akitibiwa kutokana na kutumia madawa ya kulevya kupitiliza siku sita kabla ya kifo chake, TMZ wameandika.Kwa mujibu wa tovuti hiyo, ndege binafsi ya Prince ilitua kwa dharura huko Moline, Illinois Ijumaa iliyopita, saa chache baada ya kutumbuiza Atlanta.
Kipindi hicho wawakilishi wake walidai kuwa alikuwa akisumbuliwa na mafua, kitu ambacho kilizua maswali kwasababu ndege yake ilikuwa imebakiza dakika 48 tu kufika nyumbani kabla ya kuamua kutua kwa dharura.
Vyanzo mbalimbali kutoka Moline vimeuambia mtandao huo kuwa Prince aliwahishwa hospitali na kupewe huduma ya haraka (save shot) kumsaidia.
Vyanzo hivyo vimedai kuwa madaktari walimshauri Prince akae hospitali hapo kwa saa 24. Watu wake walitaka chumba binafsi na walipoambiwa kuwa haiwezekani, Prince na wenzake waligoma.
Muimbaji huyo aliondoka saa tatu baada ya kufika hapo na kuelekea nyumbani. Vyanzo hivyo vimedai kuwa Prince aliondoka akiwa hajisikii vizuri.
Prince alikutwa hajitambui jana kwenye lifti kabla ya kutangazwa kuwa amefariki.

Director wa filamu za James Bond afariki akiwa na umri wa miaka 93

Muongazaji wa filamu ya James Bond Guy Hamilton amefariki akiwa na umri wa miaka 93.
Aliyekuwa nyota wa filamu hiyo ya 007 Roger Moore alituma ujumbe katika mtandao wake wa Twitter kwamba alihuzunishwa na kifo chake.

Hamilton alimuelekeza Roger Moore katika filamu ya Live and Let Die pamoja na The man with the Golden Gun.
Pia alifanya uelekezaji katika filamu za Sean Connery in GoldFinger na Diamond are Forever.
Hospitali moja katika kisiwa cha Uhispania cha Majorca ,ambapo Hamilton aliishi ilithibitisha kwa chombo cha habari cha AP kwamba amefariki sikju ya Jumatano.
Filamu nyengine zilizoelekezwa na Hamilton ni pamoja na The Battle in Britain,Force 10 from Navarone,Evil under the sun na The Mirror Crack’d.

Tuesday, April 12, 2016

Watoto wengi hutumiwa na Boko Haram

Umoja wa mataifa unasema kuwa kutumiwa kwa watoto kama washambuliaji wa kujitoa mhanga na kundi la wanamgambo wa Boko Haram nchini Nigeria, imeongezeka tangu mwaka uliopita.
Shirika la kuhudumia watoto la umoja wa mataifa UNICEF linasema kuwa watoto 44 walitumiwa kufanya mashambulizi kama hayo nchini Cameroon, Chad na Nigeria mwaka uliopita, ikilinganishwa na watoto wanne waliotumiwa mwaka 2014.
Inaripotiwa kuwa washambuliaji watano wa kujitoa mhanga sasa ni watoto huku robo tatu wakiwa na wasichana.
UNICEF inasema kuwa wasichana hao wakati mwingine huleweshwa, kisha hufungwa milipuko kwenye miili yao na kulazimishwa kufanya mashambulizi.

Wanafunzi 62 wafukuzwa chuoni Nairobi

Jumla ya wanafunzi 62 wa chuo kikuu cha Nairobi nchini Kenya wamefukuzwa kutoka chuo hicho, baada ya kushuhudiwa ghasia zilizosababisa kufungwa kwa chuo kwa muda usio julikana wiki moja iliyopita.
Wanafunzi waliteketeza kwa moto afisi za chuo hicho kutokana na kile kinachotajwa kuwa matokeo ya uchaguzi wa kumchagua kiongozi wa wanafunzi chuoni.
Chuo kikuu cha Nairobi kiliseme kuwa kilichukua hatua hizo za kinidhamu dhidi ya wanafunzi walioshiriki katika kuharibu mali ya umma.

Rousseff kupigiwa kura ya kumtoa ofisini

Kamati ya bunge nchini Brazil imeidhinisha hatua ya kumuondoa madarakani Rais Dilma Rousseff, na kutoa fursa ya kupigwa kura baadaye wiki hii kuamua ikiwa ataondolewa ofisini.
Baada ya mjadala mkali, kamati hiyo ilipiga kura kwa asilimia 38 kwa 27 na kupitisha kuondolewa kwake madarakani.
Rais Rossef anakana madai ya kuvuruga akaunti za serikali ili kuficha kudorora kwa uchumi.
Amelaani hatua hiyo na kuitaja kuwa mapinduzi ya kisiaia. Shughuli za Rais zimehujumiwa na uchumi unaozidi kuzorota pamoja na sakata kubwa ya ufisadi inayoikumba kampuni ya mafuta ya serikali Petrobras.

Maji ni machafu mno nchini China

Serikali ya China inasema kuwa zaidi ya asilimia 80 ya maji ya maji ya kina kifupi yaliyo chini ya ardhi ni machafu mno na hata hayaweza kutumiwa kwa kunywa wala kuoga.
Wizara inayoshughulikia maji nchini China ilifanyika uchunguzi wa zaidi ya visima 2000 eneo la mashariki, na kugundua kuwa takriban asilimia 30 ya visima hivyo ndivyo vinaweza kutumiwa kwa kilimo na viwandani.
Karibu asilimia 50 ya sampuli za maji haitatumiwa na binadamu. Maafisa nchini China wameuhakikishia umma kuwa kiwango kikubwa cha maji kinachotumiwa mijini hutokana na kirefu chini ya radhi.

Thursday, February 4, 2016

Upimaji wa ubikira wakosolewa Afrika Kusini

Waziri mmoja wa Afrika Kusini ameshtumu kuwa kinyume cha sheria ufadhili wa elimu ya wasichana wanaopita kipimo cha ubikira.
Mwezi Uliopita,Manispaa ya uthukela katika jimbo la Kwazulu Natal nchini Afrika Kusini ilisema itawapa zawadi wanafunzi 16 wa kike kwa masharti kwamba wasalie mabikira.
''Mpango huo ulilenga kupunguza maambukizi ya virusi vya HIV na mimba za mapema miongoni mwa wasichana'',alisema Meya Dudu Mazibuko.
Katika taarifa ya gazeti la Daily Maverick,waziri wa maendeleo ya kijamii Bathabile Dlamini alielezea upimaji wa ubikira kama usiowezekana,mchafu na ukiukaji mkubwa na haki za kibiniaadamu.
''Kujamiana kwa mara ya kwanza hakutakikani,licha ya hilo kuna unyanyapaa miongoni mwa wasichana ambao hufeli kipimo hicho'',alisema,akiutaja mpango huo kama ''kosa la kingono''.
Bi. Dlamini ,ambaye ni kiongozi wa chama tawala cha ANC upande wa wanawake ndio kiongozi mwenye hadhi ya juu kupinga kipimo hicho.

Wanaotuhumiwa kumvua nguo Mtanzania mbaroni India

Wanaume wanne wanaotuhumiwa kuhusika katika kumshambulia na kumvua nguo mwanafunzi wa kike kutoka Tanzania wamekamatwa, shirika la habari la AP limeripoti.
Waziri wa mashauri ya kigeni wa India Sushma Swaraj, aliandika kwenye Twitter kwamba amezikitishwa sana na “kisa hicho cha aibu” kilichotokea Jumapili eneo la Bangalore.
Bi Swaraj amesema polisi wamewakamata washukiwa wanne ambao watafunguliwa mashtaka.
Wanafunzi Waafrika mjini Bangalore wamesema wanaishi na hofu ya kushambuliwa.
Bw Bosco Kaweesi, mshauri wa kisheria wa Chama cha Wanafunzi kutoka Afrika, anasema wanafunzi wengine watatu wa kike kutoka Tanzania waliokuwa pamoja na mwanafunzi huyo garini pia walipigwa.
Gari lao liliteketezwa.
Kaweesi amesema huenda kisa hicho kilitendeka kimakosa, akisema gari la wanafunzi hao lilikuwa limefuata gari la mwanafunzi kutoka Sudan ambalo lilimgonga na kumuua mwanamke aliyekuwa amelala pembezoni mwa barabara.
Wanafunzi hao hawakumfahamu mwanafunzi huyo wa kiume aliyetoka Sudan, ambaye pia alipigwa na gari lake kuteketezwa.

Trump ataka mchujo wa Iowa urudiwe


Donald Trump anataka uchaguzi wa mchujo wa kuteua atakayegombea urais kupitia chama cha Republican katika jimbo la Iowa urudiwe, akisema mshindi Ted Cruz alitumia ulaghai.
Bw Trump anasema wakati wa kikao cha Iowa, maafisa wa kampeni wa Cruz waliwaambia wapiga kura kwamba mgombea mwingine Ben Carson alikuwa amejitoa kwenye kinyang’anyiro hicho, habari ambazo hazikuwa za kweli.
Maafisa wa kampeni wa Cruz baadaye walimuomba radhi Carson, wakisema lilikuwa kosa lisilokusudiwa.
Bw Trump alimaliza wa pili katika mchujo huo wa kwanza kufanyika nchini humo kwa ajili ya uchaguzi mkuu baadaye mwaka huu.
Mchujo utakaofuata utafanyika New Hampshire Jumanne ijayo.
"Ted Cruz hakushinda Iowa, aliiba. Hii ndiyo maana kura zote za maoni zilionekana kukosea na ndiyo sababi alipata kura nyingi kuliko ilivyotarajiwa. Ni vibaya!,” Bw Trump amesema.
Awali, alikuwa ameandika kwenye Twitter kwamba Bw Cruz alishinda mchujo wa Iowa kwa njia haramu, lakini baadaye akafuta ujumbe huo.
Matamshi ya Bw Trump ni kinyume na hotuba yake ya kukubali kushindwa ambayo aliitoa Jumatatu usiku baada ya matokeo kujulikana, jambo ambalo lilishangaza wengi ikizingatiwa ukali wake.
Kambi ya Cruz haijafurahishwa na madai ya sasa ya Bw Trump.
“Ukweli umemfika nyota huyu wa runingani – alishindwa Iowa na sasa hakuna anayezungumza kuhusu ubabe wake, kwa hivyo anachomoza kwenye Twitter,” afisa wa mawasiliano wa Bw Cruz Rick Tyler aliandikia Politico kupitia barua pepe.
“Kuna makundi yanayosaidia watu kudhibiti uraibu wa kutumia Twitter, labda anafaa kuwasiliana na tawi moja.”
Katika historia, haijatokea uchaguzi wa mchujo ukarudiwa.
Bw Carson alikubali ombi la msamaha kutoka kwa Bw Cruz lakini maafisa wake wa kampeni wamesema kambi ya Cruz ilitumia “mbinu chafu”.
Jumatano, seneta wa Kentucky Rand Paul na seneta wa zamani wa Pennsylvania Rick Santorum walijitoa kwenye kinyang’anyiro cha kutafuta tiketi ya chama cha Republican baada ya kutofanya vyema Iowa.

Obama awakemea wanaoshtumu Waislamu


Rais Barrack Obama ameshtumu kile alichokitaja kuwa Matamshi machafu dhidi ya Uislamu,kufuatia tamko la hivi majuzi lililotolewa na mgombea wa urais kupitia tiketi ya Republican Donald Trump.
Katika ziara yake ya kwanza katika msikiti kama rais,Obama amesema kuwa matamshi machafu dhidi ya waislaumu hayakubaliki nchini Marekani.
Aliwapongeza Wamarekani Waislamu kama walio na heshima na uzalendo wa hali ya juu na taifa lao.Bwana Trump ametoa wito kwa waislamu kutoruhusiwa kuingia nchini Marekani.
Obama alikuwa akizungumza katika msikiti wa jamii ya waislamu mjini Baltimore Maryland.
Ametembelea misikiti katika maeneo mengine ya dunia katika ziara rasmi katika kipindi chake cha miaka saba akiwa rais.
Ikulu ya Whitehouse imesema kuwa ziara hiyo ni kutetea uhuru wa kidini na matamshi ya kutovumiliana dhidi ya jamii za walio wachache.
Obama amesema kuwa anajua kwamba Waislamu Wamarekani wanalengwa na kulaumiwa kwa vitendo vya wachache.
''Wamarekani wengi hawawajui Waislamu'',alisema.Wengi huwasikia Waislamu na Uislamu kutoka kwa vyombo vya habari baada ya tendo la ugaidi ama katika chombo cha habari kinachoouangazia Uislamu,TV ama hata katika filamu.
Rais Obama amekuwa na uhusiano wa kutatiza na Waislamu.Mapema katika uongozi wake aliapa kuimarisha uhusiano na waislamu katika mataifa ya kigeni baada ya vita vya Iraq.