MICHAKATO

Levis Rocky Ndekeno

This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Pages

Monday, March 31, 2014

HEEE MAAJABU YA DUNIA TAZAMA PICHA YA NYOKA MWENYE MIGUU


Friday, March 28, 2014

Lil Wayne asisitiza "The Carter V" ndio itakuwa album ya mwisho ya The Carter


Album ya Lil Wayne inayotarajiwa kutoka mwaka huu "The Catter v" itakuwa ndio album yake ya mwisho kama solo artist, labda mtu ampe ofa ya dola miliomi 25 mpaka 35 kumfanya atengeneze album nyingine.
 Wayne ametumia Interview alioifanya na MTV.com kutangaza kuwa baada ya album hiyo ya tano ndio itakuwa mwisho wa kutoa kwake kwa solo album.
 
 "Nina plan ya kuwa hii ndio iwe album yangu ya mwisho kama solo artist, ndio na ni kweli hii ndio Carter album ya mwisho, ni album ya mwisho ya Carter, inaishia ya 5." Dola milioni 25 mpaka 35 zitanifanya nifanye solo album nyingine baada ya hii." amesema Lil Wayne.
 
 The Carter V haijasemekana official itatoka tarehe ngapi kwa sasa, ila katika moja ya shows iliyofanyika New Orleand mwezi uliopita, Drake alimuita Lil Wayne na kutangaza kuwa album yake itatoka tarehe 5 May.
 The Carter V ikitoka itakuwa ni karibu miaka 3 tangu alipoiachia "The Carter 1V"
 

TUHUMA NZITO DHIDI YA WAZIRI MKUU NDANI YA BUNGE LA KATIBA


Dar es Salaam. Hali ya hewa jana ilichafuka kwenye Bunge la Katiba baada ya mjumbe Ezekiel Wenje kuwatuhumu Waziri Mkuu Mizengo Pinda na baadhi ya mawaziri kuwa waliwahonga baadhi ya wajumbe wa kundi la 201.

 Katika tuhuma hizo, Wenje alimtaja Waziri Profesa Jumanne Maghembe, Dk. Shukuru Kawambwa na Gaudensia Kabaka akisema kuwa walitoa rushwa ya vyakula, maji na vinywaji kwa wajumbe hao ili waunge mkono msimamo wa serikali mbili.

 Kauli hiyo, iliyotolewa katika mjadala wa mabadiliko ya kanuni, ilisababisha mawaziri hao kunyanyuka kujibu tuhuma hizo, huku Wenje akisisitiza kuwa aliyoyasema ni kweli tupu.

 Vilevile baadhi ya wajumbe wanaotoka katika kundi hilo walicharuka na kujaribu kujitetea huku mmojawapo akitishia kuwa iwapo Wenje asingeomba radhi, asingetoka ndani ya Bunge hilo.

 Hoja ilipoanzia

 Wenje, ambaye pia ni mbunge wa Nyamagana (Chadema), alianza kwa kueleza kwamba wapinzani “walilia” sana kuwa Bunge la Katiba lisingekuwa na usawa kutokana na Chama cha Mapinduzi kuwa na wajumbe wengi, ndipo ikaonekana wapatikane wajumbe wengine 201, lakini jambo la ajabu ni kwamba walioteuliwa katika kundi hilo asilimia 80 ni makada wa CCM akiwamo mzee maarufu ambaye ameingizwa kama mganga wa jadi.

 Ingawa hakumtaja jina, Wenje alikuwa anamaanisha kada mkongwe wa CCM, Kingunge Ngombale-Mwiru aliyeteuliwa kupitia kundi la waganga wa jadi.

 Kuhusu rushwa, Wenje alisema:“…Sasa kuna wajumbe wa kundi la 201 walipelekwa kwa Profesa Maghembe na Dk. Kawambwa wamepeana rushwa, vikao vingi vilifanyika usiku. Hii haikubaliki.”

 Baada ya kauli hiyo ya Wenje, Profesa Maghembe alisimama ghafla huku akionekana kutaharuki, ambapo Makamu Mwenyekiti Samia Suluhu Hassan alimpa nafasi ya kujieleza.

 Profesa Maghembe alikiri kuwakaribisha baadhi ya wajumbe wa kundi hilo, akieleza kwamba ilikuwa ni katika hali ya ukarimu uliozoeleka miongoni mwa jamii ya Kitanzania.

 “Kuna kundi lipo hapa ambalo linafanya kazi ya kudhalilisha wenzao. Ni kweli niliwaalika kwa chakula wajumbe hao kwa taratibu za kawaida, lakini hakuna mbunge hapa anayeshindwa kujinunulia chakula, hakuna anayeweza kupewa rushwa.

 “Kwa sababu hiyo ninaomba kiti chako kimtake mjumbe aliyewasilisha hoja hiyo aniombe radhi. Wenje aniombe radhi,” alisema Profesa Maghembe akiwa katika hali ya hasira, huku kukiwa na sauti za kuzomea na kushangilia kutoka kwa wajumbe.

 Makamu mwenyekiti pia alifanya jitihada za kuwataka wajumbe kuwa wavumilivu, huku akitoa nafasi kwa Dk. Kawambwa kujieleza akisisitiza kwamba ni tuhuma nzito.

 Kawambwa alisema: “Ni kweli nilikutana nao; ni wajumbe ambao wanatoka kwenye taasisi zinazojihusisha na masuala ya elimu, lakini mbona wameshafanya mikutano yao mingine mingi ambayo mimi hawakuniita. Kama mtu akiwa hana hoja bora akae chini.”

 Makamu Mwenyekiti alimtaka Wenje aombe radhi kutokana na kauli yake, lakini katika hali ya kushangaza mjumbe huyo alisisitiza kwamba Profesa Maghembe na Dk. Kawambwa wamekiri.

 “Maghembe amekiri aliwaita wafugaji na wavuvi ndiyo waliokula chakula cha rushwa, pia wapo wengine walienda kwa Waziri Gaudensia Kabaka, kuna ushahidi mama mmoja siwezi kumtaja jina hapa alikwenda huko akafukuzwa, nitakupa jina lake mwenyekiti baadaye. Aliambiwa kwamba anatoa siri… hoja iliyojadiliwa huko ilikuwa ni kwamba msimamo ni wa serikali mbili… rushwa ya chakula, maji na bahasha walipewa,” alisema Wenje na kusababisha kulipuka kwa kelele zaidi.

 Wenje aliongeza kuwa kuna wajumbe wengine walikwenda hadi kwa waziri mkuu ambako walikula, walikunywa hadi saa 7:00 usiku.

 Alisema wengine walikwenda kwa Gaudensia Kabaka (Waziri wa Kazi na Ajira) na walikula na kunywa na kupewa bahasha.

 Baada ya Wenje kukaa, baadhi ya wajumbe wa kundi la 201 walichachamaa wakitaka kutetea hadhi yao, akiwamo mjumbe kutoka kundi la wafugaji, Esther Juma aliyesema hawatendewi haki kama kundi kusema kwamba walihongwa.

 Alisema yeye ana ng’ombe 3,000 na asingeweza kwenda kupokea rushwa ya chakula na kumtaka mbunge huyo kuwaomba radhi la sivyo asingetoka mlangoni.

 Wakati mjadala huo ukiendelea, mwenyekiti wa Bunge, Samuel Sitta aliyekuwa ametoka kwa udhuru, alirejea kimya kimya, na kumtaka Wenje kueleza iwapo anadhani kauli yake haikuwaudhi baadhi ya wajumbe.

 Wenje alikiri kuwa ni kweli baadhi ya wajumbe wameudhika kutokana na ukweli aliosema dhidi yao na kuwaomba radhi kwa ukweli huo.

 Kauli hiyo ilimfanya Sitta kutangaza kuwa anapeleka suala hilo kwenye Kamati ya Kanuni na Haki za Bunge na uamuzi utakaotolewa atautangaza bungeni.

KUNDI LA UKAWA LAWA TISHIO BUNGENI..LAPANGWA KUSAMBARATISHWA


KUNDI la wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba linalowashirikisha wanasiasa wa vyama vya upinzani, maarufu kama Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), limekuwa mwiba mkali kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho kinapanga mikakati kulisambaratisha.

 Ukawa inayoongozwa na vinara wa vyama vikubwa vya CHADEMA, CUF, NCCR-Mageuzi pamoja na vingine vidogo visivyokuwa na wabunge, inaonekana kuwa mwiba kwa Mwenyekiti wa Bunge, Samuel Sitta kwa kudhibiti uvunjwaji wa kanuni ili kuibeba CCM.

 Awali CCM ililipuuza kundi hilo na kulibeza, lakini baada ya kuona nguvu yake wakati wa kumtetea Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba apewe muda wa kutosha, hofu ilitanda.

Tuesday, March 25, 2014

HABARI KWANZA: KAMATI YA UONGOZI YA BUNGE MAALUM YAFANYA KIKAO CH...

HABARI KWANZA: KAMATI YA UONGOZI YA BUNGE MAALUM YAFANYA KIKAO CH...:   Mwenyekiti wa Bunge Maalum Mhe. Samuel Sitta akiongoza kikao cha kwanza cha kamati ya Uongozi baada ya kuundwa leo. Kamati ...

Popo waeneza Ebola Guinea


Popo hutumiwa kutengeza kitoweo maarufu sana katika baadhi ya maeneo ya Guinea, lakini sasa inahofiwa kuwa popo wanachangia kusambaa kwa ugonjwa wa Ebola kusini mwa nchi hiyo.

NI marufuku kula na kuuza popo Guinea

Maafisa nchini humo sasa wamepiga marufuku uuzaji na ulaji wa nyama ya popo katika juhudi za kudhibiti ugonjwa hatari wa Ebola, ambao kufikia sasa umesababisha vifo vya watu 62.
Habari zinazohusiana
Ebola ni kiini cha ugonjwa hatari Guinea
Wasi wasi kuhusu virusi vya Ebola
Uganda imethibitisha kuwepo kwa Ebola


Taarifa zinazohusiana
Afrika

Nchi za kanda hiyo zikiwemo Liberia na Sierra Leone, zimechukua hatua kabambe kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa huo zikiwemo kuwafanyia uchunguzi wa kiafya watu wanaongia mipakani.

Maafisa wa afya wanapata msaada kutoka shirika la afya duniani na ujumbe wa kuhamasisha watu unapeperushwa kupitia televisheni.

Watu watano kati ya sita walioingia nchini Liberia kutoka Guinea walikua na ishara za ugonjwa huo na wamethibitishwa kufa.

Hatahivyo maafisa wa utawala nchini Liberia bado hawajathibitisha kikamilifu kama kweli walikufa kutokana na ugonjwa wa Ebola.


Uhuru ahimiza ushirikiano Afrika Mashariki


Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amewataka wabunge wa bunge la jumuia ya Afrika Mashariki kuhimiza utekelezaji wa sheria zilizopitishwa na wabunge hao ili ziweze kuridhiwa na kutekelezwa na nchi washirika.

Miongoni mwa sheria zilizopitishwa na bunge hilo ni ushuru wa forodha, soko la pamoja na sarafu ya pamoja, mkataba ambao bado haujaanza kutekelezwa.
Taarifa zinazohusiana
Afrika Mashariki

Rais Uhuru Kenyatta ambaye ni mwenyekiti wa wakuu wa nchi za jumuiya hiyo yuko mjini Arusha makao makuu ya jumuiya hiyo kuzungumza na wafanyakazi na pia kuwafungulia kikao cha bunge kitakachodumu kwa wiki mbili zijazo.

Rais Kenyatta amezidi kusisitiza kuwa ushirikiano wa nchi hizo ndio ukombozi wao kiuchumi, kijamii na kisiasa.

Rais Uhuru Kenyatta akiwa safarini kwenda Arusha

Rais Kenyatta kadhalika ameelezea nia ya mataifa yote ya jumuiya ya Afrika Mashariki kupambana vikali na tatizo la ujangili na kuutokomeza.

Rais Uhuru Kenyatta pia amesema jukumu la kukabiliana na vitendo vya ujangili ni la wananchi wote kwa sababu lina athari kwa kila mtu mkaazi wa Afrika Mashariki.

Ama kuhusu suala la uhuru wa uhamishaji wa mitaji na uhuru wa wananchi wa Afrika Mashariki kutembea kutoka nchi moja kwenda nyingine, amesema jambo hilo linaweza kumalizwa pindi kila nchi itapokamilisha taratibu za matumizi ya vitambulisho kwa raia wake:

Rais Uhuru Kenyatta na ujumbe wake wamerejea nyumbani kwa njia ya barabara kupitia mpaka wa Tanzania na Kenya eneo la Namanga. Ben Mwang'onda Dira ya Dunia BBC, Arusha.

Hewa chafu inaua mamilioni duniani


Watu milioni saba walifariki mwaka 2012 kutokana na hewa chafu. Hii ni kwa mujibu wa shirika la afya duniani .

Ripoti ya shirika hilo inasema kuwa kuna uhusiano mkubwa kati ya hewa chafu na maradhi ya moyo, tatizo la kupumua na ugonjwa wa Saratani.
Taarifa zinazohusiana
afya

Kifo kimoja kati ya vinane duniani kilitokana na hewa chafu , na kuifanya hali hiyo kuwa moja ya hatari ya mazingira chafu afya ya binadamu.

Tarkriban watu milioni sita waliofariki dunia walikuwa Asia ya Mashariki na katika eneo la Pacific.

Shirika hilo limesema kuwa takriban watu milioni 3.3 walifariki kutokana na hewa chafu katika nyumba zao kwa kutumia mkaa kukipikia na wengine milioni 2.6 walifariki kutokana na hewa chafu nje ya nyumba zao , hasa katika nchi zinazostawi.

Afisaa mmoja mkuu wa shirika hilo, Daktari Maria Neira, amesema kuwa, hewa chafu ina hatari kubwa kwa afya ya watu kuliko ilivyodhaniwa hasa kwa kusababisha maradhi ya Moyo na Kiharusi.

Ripoti hii inaonyesha umuhimu wa kushirikiana katika kuhakikisha kuwepo kwa hewa safi.

Shirika hilo limesema kuwa kupunguzwa kwa viwango vya hewa chafu kunaweza kuokoa maisha ya watu.

Kadhalika shirika hilo limesema: "usafi wa hewa tunayopumua unazuia maradhi ya kuambukizana na pia kuondoa hatari kwa watoto, wazee na wanawake.''
Taarifa zinazohusiana

Wanaowania Tuzo za KILI 2014 ndio hawa, zilizoachwa ziko hapa pia


 (BASATA) limetangaza rasmi matokeo ya mchakato wa kuwapata wateule rasmi yaani ‘nominees’ wa vipengele 34 vya tuzo za muziki Tanzania.
 Kabla ya kuanza kutajwa kwa wanaowania tuzo za KTMA 2014, BASATA ilitangaza nyimbo ambazo zimetolewa kwenye kuwania tuzo hizi kutokana na sababu za kimaudhui kama unavyoona hapa chini.











Nyingine ni
 WIMBO BORA WA AFRIKA MASHARIKI – Tubonge ya Jose Chameleone, Nakupenda pia ya Wyre na Alaine, Badilisha ya Jose Chameleone, Kipepeo ya Jaguar, Kiboko changu ya Amani, Weasal na Radio.
 WIMBO BORA WA TAARAB – Wasiwasi wako wa Mzee Yusufu, asie kujua hakuthamini Isha na Saida Ramadhani, Nipe stara Rahima Machupa, sitaki shari Leila Rashid, fahari ya mwanamke ya Khadija Kopa, mambo bado Khadija Yusufu, kila muomba Mungu ya Mwanahawa Ally.
 WIMBO BORA WA RAGGA/DANCEHALL – Nishai ya Chibwa ft Juru, Sexy Lady ya Dr. Jahson, My sweet ya Jettyman Dizano, feel alright ya Lucky Stone na wine ya Princess Delyla.
 WIMBO BORA WA KUSHIRIKISHWA/KUSHIRIKIANA – Muziki gani ya Ney wa Mitego ft Diamond, Joto hasira ya Lady Jaydee ft Prof J, kidela ya Ally Kiba na Abdu Kiba, bila kukunja goti ya MwanaFA, Ay ft J Martins na tupogo ya Ommy Dimpoz ft J Martins.
 RAPA BORA WA MWAKA WA BENDI – Kitokololo, Chokoraa, Ferguson, Canal Top na Totoo ze bingwa.
 MTUMBUIZAJI BORA WA KIKE WA MUZIKI – Khadija kopa, Vanessa Mdee, Isha Ramadhani, Luiza Mbutu, Catherine (Cindy)
 MTAYARISHAJI BORA WA NYIMBO WA MWAKA TAARAB – Enrico, Ababuu mwana wa Zanzibar na Bakunde.
 MTAYARISHAJI BORA WA NYIMBO WA MWAKA (BENDI) – Allan Mapigo, C9, Enrico, Amoroso na Ababuu mwana wa Zanzibar.
 WIMBO BORA WA REGGAE – Niwe nawe ya Dabo, hakuna matata ya Lonka, tell me ya Dj Aron ft Fidempha, bado nahitaji ya Chikaka ft Bless P & Lazzy B, Bongo reggae ya Warriors from the east.
 WIMBO BORA WENYE VIONJO VYA ASILI YA KITANZANIA – Kwejaga nyangisha ya Batarokota, Nalonji ya Kumpeneka, bora mchawi Dar bongo massive, tumbo lamsokota ya Ashimba, Aliponji ya Wanakijiji na Agwemwana ya Cocodo african music band.


Monday, March 24, 2014

TAFADHALI ACHA KILA UNACHOFANYA NA SOMA HII, NI MUHIMU SANA.

Mwanamke huyu masikini yupo Labour sasa yapata siku mbili, tatizo ni kwamba ana hofu kubwa ya kufanyiwa upasuaji. Madaktari wamejaribu kufanya kila linalowezekana kwa uwezo wao lakini bado mambo yanelekea mrama.

Sasa kwa pamoja tuungane kumwambia Mungu kuwa hajalishi madaktari wamesema nini lakini Mama huyu ajifungue salama kwa njia sahihi.

Comment "Amen" kama unatarajia Taarifa nzuri hivi karibuni .Plezz DON'T IGNORE PLEASE SHARE FOR MORE PRAYERS! HII YAWEZA KUKUTOKEA HATA MAMA YAKO, DADA YAKO, MDOGO WAKO, HATA RAFIKI NA NDUGU YAKO WA KARIBU.....narudia usidharau plzzzzz

MBUNGE WA CCM AFIKISHWA KWA SPIKA KWA KUTOKUMLIPA MSHAHARA HOUSEBOY WAKE LIVE!!

Mbunge wa jimbo la Bahi (CCM) Omar Baduel amefikishwa kwa Katibu wa Bunge Dr Kashilila kwa kosa la kuto mlipa mshahara msaidizi wake wa jimbo kwa kipindi chote cha miaka minne,Said Kayumbo amelalamikia ofisi ya bunge na kuomba iingilie kati ili apate mshahara wake kwa miaka yote minne. Said kayumbo alisema mbunge huyo amekua akimpa 20,0000 au 30,000 wakati mshahara wa msaidizi wa mbunge ni 450,000.

Aidha mbunge huyo amekua na kashifa nyingi kama ile ya rushwa ambayo kesi yake inaendelea kisutu,mwezi wa february 2014 alisomewa tuhuma ya kula pesa ya mfuko wa jimbo,mwaka 2009 alifukuzwa uenyekiti wa halmashauri ya bahi kwa tuhumu za kuiba mifuko ya cement ya shirika la world vision kwenye kata yake ya Chipanga pamoja na tuhuma ya kushirikiana na mkurugenzi wa bah

SHOPRITE IMEUZWA WAFANYA KAZI WAGOMA NA KUANDAMANA MLIMANI CITY

Leo mida ya Jioni pale mlimani City nimeshuhudia wafanya kazi wa Duka Kubwa la Shoprite wakiwa wamegoma wakizua watu wasiingie kwenye duka hilo kwa kile kilichodaiwa kuwa duka hilo limeuzwa bila wao kupewa mafao yao ...Habari zilizopo ni kuwa duka hilo limenunuliwa na Super Market Ingine kubwa Nchini Kenya Ambayo inakuja kupanua biashara zake hapa Dar .....

ETI UGONJWA MKUBWA UNAOTUSUMBUA WA TANZANIA SIO UKIMWI WALA MALARIA NI HUU HAPA..NINI , EMBU SOMA KUJUA

Kwenye nchi zinazoendelea Tanzania ikiwemo magonjwa ya kuambukizwa yameonekana kuwa ndio tishio sana kwa afya za wananchi. Magonjwa kama ukimwi, malaria, TB, kichocho, kipindupindu na homa za matumbo yamekuwa yakisumbua sehemu kubwa ya watu katika nchi hizi.

Ili kuokoa afya za wananchi serikali za nchi hizi zinazoendelea zimekuwa zikiweka mipango kabambe ya kupambana na magonjwa haya. Mipango mingi iliyowekwa imefanikiwa ila sio kwa kiwango kikubwa sana. Hii ni kwa sababu kuna ugonjwa mwingine mkubwa zaidi ya magonjwa haya ya kuambukizwa unaosumbua wananchi.

Kabla hatujaangalia ugonjwa huo hebu tuangalie tofauti kati ya mataifa yenye magonjwa ya kuambukizwa na yale ambayo hayana kwa kiwango kikubwa. Ukiangalia kwa makini utagundua kwamba mataifa yanayosumbuliwa sana na magonjwa ya kuambukizwa ni mataifa ambayo watu wake ni masikini sana. Na hata ndani ya taifa sehemu ambazo magonjwa haya yameshamiri ni sehemu ambazo watu ni masikini. Nina hakika unajua kipindupindu huwa kinatokea maeneo gani sana sana.

Kwa mantiki hii basi ugonjwa mkubwa unaoisumbua nchi yetu sio ugonjwa wa kuambukiza bali ni umasikini. Umasikini ndio ugonjwa mkuu ambao unapoteza maisha ya wananchi wengi. Umasikini ndio ugonjwa mkubwa unaofanya maisha ya wananchi wengi kuwa magumu. Na kwa kuwa kwenye mipango ya kupambana na magonjwa umasikini haujawekwa, basi hakuna anayefunguka macho kuuangalia.

Ni umasikini unaofanya wengi kufanya ngono zembe na wakati mwingine ukahaba na kujikuta wanaambukizwa magonjwa ya zinaa na ukimwi. Ni umasikini unaofanya watu wakose maji safi na salama na kuishia kutumia maji machafu yanayowasababishia magonjwa ya tumbo na minyoo. Na ni umasikini unaofanya watu kukosa elimu na hivyo kushindwa kujikinga na magonjwa yanayoweza kuzuilika.

Tunawezaje kutokomeza ugonjwa huu?

Kwa kuwa ugonjwa huu hauko wazi basi serikali haijaweka mikakati ya kupambana nao au kuutokomeza. Hata baadhi ya mipango mingi iliyowahi kuwekwa kupambana na ugonjwa huu haikuzaa matunda yaliyotarajiwa na mwishowe kufa.
Mipango mingi imeshindwa kwa sababu serikali imekuwa ikiangalia sehemu isiyohusika kwenye kupambana na ugonjwa huu. Huwezi kuondoa umasikini kwa kutegemea misaada. Misaada haiondoi bali inaongeza umasikini.

Njia pekee ya kuondoa umasikini ni kuwajengea watu uwezo wa kufanya kazi yenye manufaa kwa watu wengine. Kuzalisha bidhaa au huduma zinazohitajika na watu wengine hivyo kutengeneza biashara kwa ngazi ya kitaifa na baadae kitaifa.

Serikali ingepaswa kuwajengea watu uwezo wa kuajiriwa, kujiajiri na kufanya biashara. Na kwa kuwa kuajiriwa nafasi hazitoshi basi kujiajiri na biashara ni njia nzuri za kupambana na ugonjwa huu. Kwa kuwa serikali haifanyi hivi je wewe unalala?

Usilale, tulishakubaliana kwamba usimlaumu yeyote, AMKA na chukua hatua juu ya maisha yako. Jijengee uwezo wa kujiajiri na kufanya biashara ili uweze kuutokomeza ugonjwa huu mbaya kwako, kwa familia yako na kwa jamii inayokuzunguka. Kama watu wachache tutachukua hatua hii baadae itasambaa na kufanyika na watu wanaotuzunguka na hatimaye taifa zima.

Unawezaje kujijengea uwezo?

Katika mtandao huu wa AMKA MTANZANIA tumeshajadili njia nyingi sana za kujijengea uwezo kwa kujifunza na kuchukua hatua. Anza kuzitumia njia hizi kwenye kazi na biashara zako na utaona mabadiliko makubwa. Kama wewe ni mgeni kwenye mtandao huu endelea kusoma makala nyingi utakutana na mawazo mengi juu ya kuchukua hatua na kubadilika.

Ili uweze kujiondoa kwenye ugonjwa huu wa umasikini inabidi ujue ni nini kinakufanya mpaka sasa unateseka na ugonjwa huo. Kwa kujua sababu itakuwa rahisi kwako kupambana nazo na hatimaye kushinda. Unaweza kuzijua sababu hizo kwa kusoma kitabu KWA NINI MPAKA SASA WEWE SIO TAJIRI. Kupata kitabu hiko bonyeza maandishi hayo.

Njia kubwa ya kupambana na ugonjwa huu wa umasikini ni kujijengea uwezo. Na njia bora ya kujijengea uwezo ni kujifunza na kuchukua hatua ya kutekeleza yale unayojifunza. Kama unataka kujifunza zaidi juu ya biashara na mambo mengine jiunge na kisima cha maarifa na uchote maarifa yatakayokusaidia. Kujiunga na kisima cha maarifa bonyeza maandishi haya.

Kuanzia sasa jua ugonjwa namba moja unaotakiwa kupambana nao ni umasikini na usifikiri msaada utakusaidia kuondokana na umasikini.

Thursday, March 20, 2014

Wednesday, March 19, 2014

Owago too hot for TV (condom joke)



REMNANT CHRISTIAN CENTRE

Tuesday, March 18, 2014

Rick Ross – Mastermind Tracklist Lyrics 2014

 

1. Intro
2. Rich Is Gangsta
 3. Drug Dealer's Dream
4. Shots Fired
5. Nobody
6. The Devil Is A Lie (feat. JAY Z)
7. Mafia Music III (feat. Sizzla & Mavado)
8. War Ready (feat. Jeezy)
9. What A Shame
10. Supreme
11. BLK & WHT
 12. Dope Bitch Skit
13. In Vein (feat. The Weeknd)
14. Sanctified (feat. Kanye West & Big Sean)
 15. Walkin On Air (feat. Meek Mill)
16. Thug Cry (feat. Lil Wayne)
                                           Deluxe

1. Blessing In Disguise (feat. Scarface & Z-Ro)
 2. Paradise Lost
 3. You Know I Got It (Reprise)