MICHAKATO

Levis Rocky Ndekeno

This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Pages

Tuesday, April 26, 2016

Lucy Kibaki afariki

Aliyekuwa mke wa rais wa zamani nchini Kenya Lucy Kibaki amefariki. Lucy alifariki katika hospitali ya Bupa Cromwell mjini London. Alisafrishwa hadi mjini Landon wiki moja iliopita kwa matibabu

Sunday, April 24, 2016

Lady Jaydee - NdiNdiNdi (Official Music Video)

Icheck video ya wimbo wa Lady Jaydee ‘Ndindindi’ iliyoongozwa na Justin Campos.

Hii ndiyo maana ya wimbo wa Lady Jaydee ‘Ndindindi’

Lady Jaydee ametoa maana ya wimbo wake ‘Ndindindi’ ambalo lilikuwa ni fumbo lililokuwa linawapa majibu mengi yasiyokuwa na uhakika mashabiki wake.

Wimbo wa ‘Ndindindi’ unazidi kufanya kwenye medi mbalimbali na kumrudisha vizuri Jide aka Binti Komando kwenye muziki wa Bongo Fleva baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu bila ya kuachia wimbo wowote.

Akiongea kwenye kipindi cha FNL, kinachoruka kupitia EATV, Lady Jaydee alisema, “The Ndi mimi ni kitu tori wewe si kitu” lakini pia aliongezea “ili kuleta fleva ya muziki ndiyo nikaiita Ndindindi. Mimi ni kitu na wewe si chochote.”

Friday, April 22, 2016

Mabasi yaendayo kasi yaanza safari zake Dar

Mabasi yaendayo kasi, yameanza kufanya safari zake katikati ya jiji la Dar es Salaam Ijumaa hii.
 Jumla ya mabasi 50 yameingia barabarani. Kwa wewe ambaye hujui njia mbalimbali za mabasi hayo, chini ni sehemu yanapopita.
1) RUTI YA KIMARA- KIVUKONI Mabasi Sita (6). Kati ya mabasi Hayo sita wakati wa Kutoka Jangwani matatu yataenda Kimara na Matatu Kivukoni.
2. RUTI YA KIMARA – KARIAKOO Mabasi Sita (6). Kati ya hayo Matatu yataelekea Kariakoo na Matatu Kimara.
3. RUTI YA UBUNGO – KIVUKONI Mabasi nane (8). Kati ya hayo Mabasi Manne yataelekea Ubungo na Manne Kivukoni.
4. RUTI YA UBUNGO – KARIAKOO Mabasi nane (8). Kati ya hayo Mabasi manne Yataenda Ubungo na Manne yataenda Kariakoo.
5. RUTI YA UBUNGO – MOROCCO Mabasi nane (8). Kati ya hayo Manne yataenda Ubungo Manne yataenda Morocco.
6. RUTI YA MOROCCO – KARIAKOO Mabasi sita (6). Kati ya hayo mabasi Matatu Morocco na Matatu Kariakoo.
7. RUTI YA MOROCCO – KIVUKONI Mabasi nane (8). Kati ya Hayo Mabasi Manne yataenda Moroco na mabasi manne Kivukoni.
DESPATCH PLAN SAA KUMI NA MBILI KAMILI. 1. Kimara Terminal Mabasi Sita (6) 2. Ubungo Terminal Mabasi kumi na mbili (12) 3. Morocco Termial Mabasi kumi na moja (11) 4. Kariakoo Terminal Mabasi kumi (10) 5. Kivukoni Terminal Mabasi kumi na moja (11) JUMLA NI MABASI HAMSINI (50)

Chanzo cha kifo cha Prince chabainika, alitumia madaya ya kulevya kumzidi

Muimbaji, Prince alikuwa akitibiwa kutokana na kutumia madawa ya kulevya kupitiliza siku sita kabla ya kifo chake, TMZ wameandika.Kwa mujibu wa tovuti hiyo, ndege binafsi ya Prince ilitua kwa dharura huko Moline, Illinois Ijumaa iliyopita, saa chache baada ya kutumbuiza Atlanta.
Kipindi hicho wawakilishi wake walidai kuwa alikuwa akisumbuliwa na mafua, kitu ambacho kilizua maswali kwasababu ndege yake ilikuwa imebakiza dakika 48 tu kufika nyumbani kabla ya kuamua kutua kwa dharura.
Vyanzo mbalimbali kutoka Moline vimeuambia mtandao huo kuwa Prince aliwahishwa hospitali na kupewe huduma ya haraka (save shot) kumsaidia.
Vyanzo hivyo vimedai kuwa madaktari walimshauri Prince akae hospitali hapo kwa saa 24. Watu wake walitaka chumba binafsi na walipoambiwa kuwa haiwezekani, Prince na wenzake waligoma.
Muimbaji huyo aliondoka saa tatu baada ya kufika hapo na kuelekea nyumbani. Vyanzo hivyo vimedai kuwa Prince aliondoka akiwa hajisikii vizuri.
Prince alikutwa hajitambui jana kwenye lifti kabla ya kutangazwa kuwa amefariki.

Director wa filamu za James Bond afariki akiwa na umri wa miaka 93

Muongazaji wa filamu ya James Bond Guy Hamilton amefariki akiwa na umri wa miaka 93.
Aliyekuwa nyota wa filamu hiyo ya 007 Roger Moore alituma ujumbe katika mtandao wake wa Twitter kwamba alihuzunishwa na kifo chake.

Hamilton alimuelekeza Roger Moore katika filamu ya Live and Let Die pamoja na The man with the Golden Gun.
Pia alifanya uelekezaji katika filamu za Sean Connery in GoldFinger na Diamond are Forever.
Hospitali moja katika kisiwa cha Uhispania cha Majorca ,ambapo Hamilton aliishi ilithibitisha kwa chombo cha habari cha AP kwamba amefariki sikju ya Jumatano.
Filamu nyengine zilizoelekezwa na Hamilton ni pamoja na The Battle in Britain,Force 10 from Navarone,Evil under the sun na The Mirror Crack’d.

Tuesday, April 12, 2016

Watoto wengi hutumiwa na Boko Haram

Umoja wa mataifa unasema kuwa kutumiwa kwa watoto kama washambuliaji wa kujitoa mhanga na kundi la wanamgambo wa Boko Haram nchini Nigeria, imeongezeka tangu mwaka uliopita.
Shirika la kuhudumia watoto la umoja wa mataifa UNICEF linasema kuwa watoto 44 walitumiwa kufanya mashambulizi kama hayo nchini Cameroon, Chad na Nigeria mwaka uliopita, ikilinganishwa na watoto wanne waliotumiwa mwaka 2014.
Inaripotiwa kuwa washambuliaji watano wa kujitoa mhanga sasa ni watoto huku robo tatu wakiwa na wasichana.
UNICEF inasema kuwa wasichana hao wakati mwingine huleweshwa, kisha hufungwa milipuko kwenye miili yao na kulazimishwa kufanya mashambulizi.

Wanafunzi 62 wafukuzwa chuoni Nairobi

Jumla ya wanafunzi 62 wa chuo kikuu cha Nairobi nchini Kenya wamefukuzwa kutoka chuo hicho, baada ya kushuhudiwa ghasia zilizosababisa kufungwa kwa chuo kwa muda usio julikana wiki moja iliyopita.
Wanafunzi waliteketeza kwa moto afisi za chuo hicho kutokana na kile kinachotajwa kuwa matokeo ya uchaguzi wa kumchagua kiongozi wa wanafunzi chuoni.
Chuo kikuu cha Nairobi kiliseme kuwa kilichukua hatua hizo za kinidhamu dhidi ya wanafunzi walioshiriki katika kuharibu mali ya umma.

Rousseff kupigiwa kura ya kumtoa ofisini

Kamati ya bunge nchini Brazil imeidhinisha hatua ya kumuondoa madarakani Rais Dilma Rousseff, na kutoa fursa ya kupigwa kura baadaye wiki hii kuamua ikiwa ataondolewa ofisini.
Baada ya mjadala mkali, kamati hiyo ilipiga kura kwa asilimia 38 kwa 27 na kupitisha kuondolewa kwake madarakani.
Rais Rossef anakana madai ya kuvuruga akaunti za serikali ili kuficha kudorora kwa uchumi.
Amelaani hatua hiyo na kuitaja kuwa mapinduzi ya kisiaia. Shughuli za Rais zimehujumiwa na uchumi unaozidi kuzorota pamoja na sakata kubwa ya ufisadi inayoikumba kampuni ya mafuta ya serikali Petrobras.

Maji ni machafu mno nchini China

Serikali ya China inasema kuwa zaidi ya asilimia 80 ya maji ya maji ya kina kifupi yaliyo chini ya ardhi ni machafu mno na hata hayaweza kutumiwa kwa kunywa wala kuoga.
Wizara inayoshughulikia maji nchini China ilifanyika uchunguzi wa zaidi ya visima 2000 eneo la mashariki, na kugundua kuwa takriban asilimia 30 ya visima hivyo ndivyo vinaweza kutumiwa kwa kilimo na viwandani.
Karibu asilimia 50 ya sampuli za maji haitatumiwa na binadamu. Maafisa nchini China wameuhakikishia umma kuwa kiwango kikubwa cha maji kinachotumiwa mijini hutokana na kirefu chini ya radhi.