MICHAKATO

Levis Rocky Ndekeno

This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Pages

Tuesday, February 2, 2016

Kisa nadra cha Zika charipotiwa Marekani

Kisa nadra sana cha virusi vya Zika kuambukizwa kupitia kushiriki ngono, badala ya kuumwa na mbu, kimeripotiwa nchini Marekani.
Mgonjwa aliyeambukizwa virusi hivyo Dallas, Texas, sana huenda aliambukizwa kupitia kufanya mapenzi, Kituo cha Udhibiti wa Maradhi (CDC) kimeambia BBC.
Mtu huyo hakuwa amesafiri maeneo ambayo yana virusi hivyo lakini mpenzi wake alirejea majuzi kutoka Venezuela.
Virusi vya Zika vinaenezwa sana na mbu na vimehusishwa na visa vya watoto kuzaliwa wakiwa na vichwa vidogo na ubongo kudumaa.
Vinaenea kwa kazi Amerika na Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza hali ya tahadhari duniani.
Shirika la msalaba mwekundu nchini Marekani limewahimisha watu waliotoka maeneo yaliyoathirika na Zika, na ambao wanataka kutoa damu, wasubiri angalau siku 28, kabla ya kutoa damu.
Ushauri huu umeelekezwa kwa watu waliorejea Marekani kutoka Mexico, visiwa vya Caribbean au Amerika ya Kati na Kusini katika kipindi cha wiki nne zilizopita, shirika hilo limesema kupitia taarifa.
Katika tukio jingine, visa viwili vya maambukizi ya Zika vimethibitishwa Australia.

Basi linalotumia umeme wa jua lazinduliwa Uganda

Basi linalotumia umeme wa nguvu za jua ambalo limedaiwa na watengezaji wake nchini Uganda kuwa la kwanza barani Afrika limeendeshwa hadharani.
Basi hilo la kielektroniki aina ya Kayoola linalomilikiwa na kampuni ya Kiira Motors lilionyeshwa katika uwanja wa Uganda mjini Kampala.
Mojawapo ya betri zake zinaweza kuwekwa chaji na vibamba vya umeme wa jua katika paa la nyumba ambavyo huongeza kasi ya gari hilo hadi kilomita 80 kwa saa.
Watengezaji wake sasa wanalenga kuwavutia wateja wataolitengeza basi hilo ili kuvutia soko kubwa la magari duniani.
Mkurugenzi mkuu wa Kiira Motors Paul Isaac Musasizi ameiambia BBC kwamba amefurahishwa na jaribio la gari hilo lilipoendeshwa.
Raia wamefurahishwa na wazo kwamba Uganda ina uwezo wa kutengeza mfano kama huu na bw. Musasizi anasema kwamba angependelea kulisaidia taifa hilo kushindana na kampuni nyengine za magari katika eneo hili.
Pia anatumai kwamba hatua hiyo itabuni ajira zifikiazo 7000 kufikia mwaka 2018.Hatahivyo mradi huo hauwezi kuanza bila ya usaidizi wa kampuni zinazotengeza vifaa vya magari.

Lengo ni kwamba kufikia 2039,kampuni hiyo itakuwa na uwezo wa kutengeza vifaa vya magari na kuviunganisha nchini Uganda bila kutegemea kampuni nyengine .
Basi hilo lenye viti 35 linalenga kufanya kazi katika miji midogo badala ya mji mkuu kutokana na masharti ya umbali linakoweza kusafiri.
Iwapo mabasi hayo yatazalishwa kwa wingi,kila basi litagharimu kiasi cha dola 58,000 ambacho bw,Musaizi anasema ni bei nzuri katika soko lenye ushindani mkubwa.
Kampuni ya Kiira Motors ilianzishwa kutokana na mradi uliofanyika katika chuo kikuu cha Makerere,ambacho ni mmoja wa mmiliki wa hisa katika kampuni hiyo na pia kimenufaika na ufadhili kutoka kwa hazina ya fedha ya serikali.

Mfalme Abdullah wa Jordan anasema kuwa nchi yake iko kwenye hatari kubwa kufuatia wimbi la maelfu ya wakimbizi kutoka nchini Syria.
Kabla ya kufanyika kwa mkutano kuhusu utoaji misaada nchini Syria, mfalme Abdullah aliiambia BBC kuwa kuna shinikizo kubwa katika utoaji wa huduma za kijamii nchii Jordan, za miundo msingi na kwa uchumi.
Amesema kuwa jamii ya kimataifa inahitaji kutoa usaidizi zaidi ikiwa itahitaji Jordan iendelee kuwachukua wakimbizi zaidi.
Umoja wa Mataifa unatafuta dola billioni 7.7 kufadhili oparesheni za kutoa misaada kwa watu milioni 22.5 nchini Syria na nchi majirani mwaka ujao.
Jordan inawahifadfhi watu 635,000 kati ya watu millioni 4.6 ambao ni wakimbzi raia wa Syria waliosajiliwa na Umoja wa Mataifa. Serikali inasema kuwa zaid ya watu milioni moja raia wa Syria wanaoishi nchini humo wakiwemo wale waliowasilii kabla ya mzozo kuanza mwaka 2011.

Lubuva: Magufuli hafai kuingilia kati Zanzibar

Mwenyekiti wa tume ya taifa ya uchaguzi Tanzania Jaji Damian Lubuva amesema Rais John Magufuli hafai kuingilia kwenye mzozo wa uchaguzi unaoendelea visiwani Zanzibar.
Akizungumza alipokutana na Dkt Magufuli katika ikulu, Dar es Salaam Jumatatu, Jaji Lubuva amesema tume za uchaguzi zinafaa kuwa huru na hazifai kuingiliwa kimaamuzi na Rais wala kiongozi yeyote.
Amesema wanaosema Rais anapaswa kuingilia kati masuala ya uchaguzi iwe Tanzania bara ama Zanzibar wanafanya makosa, kwani Rais hana mamlaka hayo.
“Unaposikia kwamba Rais wa Jamhuri ya Muungano aingilie hilo suala la uchaguzi wa Zanzibar, yeye kwa kweli hana mamlaka kabisa. Pili ni kama kujikanganya, huku unasema tuwe na tume huru isiyoingiliwa halafu huku unasema aingilie kati maamuzi ya tume,” amesema Jaji Lubuva, kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa kutoka ikulu na kaimu mkurugenzi ya mawasiliano ya ikulu, Bw Gerson Msigwa.
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar Jecha Salim Jecha alitangaza kufutwa kwa matokeo ya uchaguzi uliofanyika visiwani humo tarehe 25 Oktoba mwaka uliopita akisema kulikuwa na kasoro nyingi.
Wiki iliyopita, Bw Jecha, kupitia tararifa, alitangaza kwamba uchaguzi utarudiwa Machi 20.
Chama cha Wananchi (CUF), ambacho kimekuwa kikisisitiza kwamba mshindi wa uchaguzi wa mwaka jana anafaa kutangazwa, kimesema hakitashiriki marudio hayo ya uchaguzi.

Meli iliyokuwa hatarini yarejeshwa baharini

Meli iliyokuwa ikielekea kwenye ufuo wa Ufaransa ikiwa imeinama imerejeshwa ndani ya bahari, maafisa wa baharini wanasema.
Meli ya kuvuta meli nyingine kutoka Uhispania imefanikiwa kuivuta meli hiyo na kuiingiza ndani ya baharini, msemaji wa chama cha mabaharia Ufaransa Louis-Xavier Renaux amesema.
Meli hizo mbili sasa zinaelekea magharibi ndani ya bahari ya Atlantic kwa kasi ya kilomita tano kwa saa, ameongeza.
Mabaharia 22 waliokuwa kwenye meli hiyo kwa jina Modern Express ambayo imesajiliwa Panama, waliondolewa salama kwa kutumia ndege kutoka kwenye meli hiyo Jumanne wiki iliyopita.
Maafisa walikuwa wamehofia kwamba meli hiyo, iliyokuwa kilomita 44 pekee kutoka ufuo wa Ufaransa eneo la Arcachon karibu na Bordeaux, ksuini magharibi mwa Ufaransa ingezama.
Lakini wataalamu wane walifanikiwa kushikisha mnyororo wa kuvuta meli hiyo na kuwezesha kuvutwa kwake.
Iwapo operesheni hiyo ingefeli, meli hiyo ingegonga ufuo wa kusini magharibi mwa Ufaransa kati ya Jumatatu usiku na Jumanne asubuhi.

Hali mbaya ya hewa ilitatiza juhudi za uokoaji Jumapili, siku mbili baada ya mnyororo mwingine wa kuivuta meli hiyo kukatika.

Meli hiyo ilikuwa imebeba tani 3,600 za mbao na mashine za kuchimba ardhini.
Ilikuwa imeinama kwa pembe ya nyuzi 40 hadi 50.

Maafisa wa baharini wamesema haiwezekani kuisimamisha.
AP
Meli hiyo ina mafuta tani 300 na kwa mujibu wa gazeti la Sud-Ouest, mipango ya dharura ilikuwa imeandaliwa kuhifadhi na kuyatoa mafuta hayo iwapo ingezama

Brazil: Virusi vya Zika havitaathiri Olimpiki


Brazil Serikali ya Brazil imesema Michezo ya Olimpiki, inayotarajiwa kufanyika Agosti mwaka huu, haitaahirishwa kwa sababu ya mlipuko wa virusi vya Zika.
Maafisa wa serikali wamesema hakuna hatari yoyote kwa wanariadha na mashabiki, ila tu kwa wanawake wajawazito.
Awali, Shirika la Afya Duniani (WHO) lilikuwa limeonya kuwa virusi vya Zika ni hatari kubwa kwa afya ya umma duniani na kutangaza hali ya tahadhari.
Shirika hilo limeyataka mataifa kuungana kuukabili ugonjwa huo.
Virusi hivyo vimehusishwa na kuzaliwa kwa watoto wanaozaliwa wakiwa na vichwa vidogo na ubongo uliodumaa
Wataalamu wameonya kwamba virusi hivyo vinavyoenezwa na mbu vinasambaa sana Amerika Kusini na kusababisha madhara makubwa.
"Lazima tuwafafanulie wale wanaojiandaa kuja Brazil, wanariadha, kwamba hawakabiliwi na hatari yoyote kama wewe si mwanamke mjamzito,” shirika la habari la Reuters limemnukuu msemaji wa Rais Dilma Rousseff, Jaques Wagner.

Rais Rousseff awali alikuwa ameidhinishwa wakaguzi wa afya na usafi kutumia nguvu, ikibidi, kufikia nyumba za watu binafsi, kama sehemu ya juhudi za serikali za kuangamiza maeneo ambayo mbu wanatumia kuzaana, hasa maji yaliyotulia.
Wakaguzi sasa wako huru kuitisha usaidizi wa polisi ikihitajika.
Zaidi ya wanajeshi 200,000 wanatumiwa kusaidia katika ukaguzi huo.
Wizara ya afya nchi humo imesema 25% ya nyumba 49 milioni nchini humo kwa sasa zimekaguliwa.

Ted Cruz amshinda Trump mchujo wa Iowa

Seneta wa Texas Ted Cruz ameshinda mchujo wa uchaguzi wa mgombea wa uchaguzi wa Republican katika jimbo la Iowa, Marekani.
Huo ndio mchujo wa kwanza katika uchaguzi wa urais wa 2016 ambao utafanyika baadaye mwezi Novemba.
Cruz amepata asilimia 28 ya kura.
"Huu ni ushindi wa wahafidhina jasiri," mgombea huyo amesema baada ya kubainika kwa ushindi wake.
Mfanyabiashara Donald Trump alikuwa akiongoza kwenye kura za maoni kabla ya kura kupigwa lakini sasa amekuwa wa pili na asilimia 24.
Seneta wa Florida Marco Rubio amefanya vyema kuliko ilivyotarajiwa, na akamaliza nambari tatu na asilimia 23.
Kura za mchujo wa chama cha Democratic bado zinahesabiwa.
Asilimia 85 ya kura ambazo zimehesabiwa zinaonyesha pengo kati ya Hillary Clinton na mshoshialisti wa chama cha Democratic Bernie Sanders ni 1% pekee.
Akizungumza baada ya matokeo kujulikana, Marco Rubio amempongeza Bw Cruz na kusema ndiye mgombea ambaye anaweza kuunganisha chama cha Republican ambacho kimegawanyika.
Dakika chache baadaye, Bw Trump alipanda jukwaani katika ukumbi mwingine na kumpongeza seneta huyo wa Texas, na kusema anaridhika kumaliza katika nambari mbili.
Wagombea wawili wamejiondoa kinyang’anyironi