MICHAKATO

Levis Rocky Ndekeno

This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Pages

Tuesday, April 12, 2016

Watoto wengi hutumiwa na Boko Haram

Umoja wa mataifa unasema kuwa kutumiwa kwa watoto kama washambuliaji wa kujitoa mhanga na kundi la wanamgambo wa Boko Haram nchini Nigeria, imeongezeka tangu mwaka uliopita.
Shirika la kuhudumia watoto la umoja wa mataifa UNICEF linasema kuwa watoto 44 walitumiwa kufanya mashambulizi kama hayo nchini Cameroon, Chad na Nigeria mwaka uliopita, ikilinganishwa na watoto wanne waliotumiwa mwaka 2014.
Inaripotiwa kuwa washambuliaji watano wa kujitoa mhanga sasa ni watoto huku robo tatu wakiwa na wasichana.
UNICEF inasema kuwa wasichana hao wakati mwingine huleweshwa, kisha hufungwa milipuko kwenye miili yao na kulazimishwa kufanya mashambulizi.

Wanafunzi 62 wafukuzwa chuoni Nairobi

Jumla ya wanafunzi 62 wa chuo kikuu cha Nairobi nchini Kenya wamefukuzwa kutoka chuo hicho, baada ya kushuhudiwa ghasia zilizosababisa kufungwa kwa chuo kwa muda usio julikana wiki moja iliyopita.
Wanafunzi waliteketeza kwa moto afisi za chuo hicho kutokana na kile kinachotajwa kuwa matokeo ya uchaguzi wa kumchagua kiongozi wa wanafunzi chuoni.
Chuo kikuu cha Nairobi kiliseme kuwa kilichukua hatua hizo za kinidhamu dhidi ya wanafunzi walioshiriki katika kuharibu mali ya umma.

Rousseff kupigiwa kura ya kumtoa ofisini

Kamati ya bunge nchini Brazil imeidhinisha hatua ya kumuondoa madarakani Rais Dilma Rousseff, na kutoa fursa ya kupigwa kura baadaye wiki hii kuamua ikiwa ataondolewa ofisini.
Baada ya mjadala mkali, kamati hiyo ilipiga kura kwa asilimia 38 kwa 27 na kupitisha kuondolewa kwake madarakani.
Rais Rossef anakana madai ya kuvuruga akaunti za serikali ili kuficha kudorora kwa uchumi.
Amelaani hatua hiyo na kuitaja kuwa mapinduzi ya kisiaia. Shughuli za Rais zimehujumiwa na uchumi unaozidi kuzorota pamoja na sakata kubwa ya ufisadi inayoikumba kampuni ya mafuta ya serikali Petrobras.

Maji ni machafu mno nchini China

Serikali ya China inasema kuwa zaidi ya asilimia 80 ya maji ya maji ya kina kifupi yaliyo chini ya ardhi ni machafu mno na hata hayaweza kutumiwa kwa kunywa wala kuoga.
Wizara inayoshughulikia maji nchini China ilifanyika uchunguzi wa zaidi ya visima 2000 eneo la mashariki, na kugundua kuwa takriban asilimia 30 ya visima hivyo ndivyo vinaweza kutumiwa kwa kilimo na viwandani.
Karibu asilimia 50 ya sampuli za maji haitatumiwa na binadamu. Maafisa nchini China wameuhakikishia umma kuwa kiwango kikubwa cha maji kinachotumiwa mijini hutokana na kirefu chini ya radhi.