MICHAKATO

Levis Rocky Ndekeno

This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Pages

Saturday, June 28, 2014

TUZO ZA WATU ILIYOFANYIKA IJUMAA HII

 
Tuzo za watu za Tanzania au Tanzania People’s Choice Awards zimetolewa Ijumaa hii kwenye ukumbi uliopo Serena Hotel jijini Dar es Salaam. Jumla ya vipengele 11 vilikuwa vinashindaniwa. Mshindi katika kila kipengele ameibuka na zawadi ya shilingi milioni moja pamoja na trophy. Host wa tuzo hizo alikuwa mtangazaji mkongwe wa radio, Jimmy Kabwe.
1. MTANGAZAJI WA REDIO ANAYEPENDWA
 Millard Ayo – Clouds FM

2. KIPINDI CHA REDIO KINACHOPENDWA
 Amplifaya – Clouds FM

3.MTANGAZAJI WA RUNINGA ANAYEPENDWA
 Salim Kikeke – BBC Swahili

4. KIPINDI CHA RUNINGA KINACHOPENDWA
 Mkasi – EATV

5. MWANAMICHEZO ANAYEPENDWA
 Juma Kaseja – Yanga

6. MUONGOZAJI WA VIDEO ZA MUZIKI ZINAZOPENDWA
 Nisher

7. VIDEO YA MUZIKI INAYOPENDWA YA MWANAMUZIKI WA KIUME
 My Number – Diamond

8. VIDEO YA MUZIKI INAYOPENDWA YA MWANAMUZIKI WA KIKE
 Yahaya – Lady Jaydee

09. MUIGIZAJI WA KIUME KWENYE FILAMU ANAYEPENDWA
 King Majuto

10. MUIGIZAJI WA KIKE KWENYE FILAMU ANAYEPENDWA
 Elizabeth ‘Lulu’ Michael

11. FILAMU INAYOPENDWA
 Ndoa Yangu




Wednesday, June 25, 2014

June 25: Ni Miaka miaka mitano tangu kifo cha Michael Jackson






Michael Jackson alifariki June 25, 2009, katika muda aliokuwa akiutafuta sana usingizi huku akijiandaa kurejea kwa kufanya ziara yake ambayo aliamini ingemuondoa kwenye madeni mengi na kurudisha heshima yake kama mfalme wa pop. Katika siku zake za mwisho, Michael Jackson aliondoka nchini Marekani akiwa na wanae watatu muda mfupi baada ya kumalizika kwa kesi yake ya kulawiti watoto.

Alirejea Marekani kimyakimya mwaka 2006, baada ya kukaa huko Bahrain kwa mwaka mzima na miezi kadhaa nchini Ireland. Bill Whitfield na Jevon Beard walitumia miaka miwili kama walinzi wa MJ walisimulia mengi kwenye kitabu kipya kiitwacho s “Remember the Time: Protecting Michael Jackson in His Final Days.” Kipindi Jackson anashuka kutoka kwenye ndege binafsi jijini Las Vegas, watu aliokuwa nao walikuwa wanae na mlezi wa watoto wake tu. “Alikuwa peke yake,” Whitfield alisema kwenye mahojiano na CNN. Kikawa kitu kisicho cha kawaida. Kuna kitu hakipo sawa. Huu ni utani.”

Walinzi hao ambao wakati mwingine hawakuwa wakilipwa mshahara kwa miezi, walikuwa wakitumia fedha zao kusaidia masuala nyumbani kwa Jackson pale credit cards zake zilipokuwa zikiishiwa. Beard aliiambia CNN kuwa mameneja wake walikuwa wakimzunguka. “Jamaa alikuwa amechoka kiakili.” Whitfield na Beard walidai kuwa Jackson alikuwa na mambo yake ya siri yaliyokuwa yakijulikana labda kwa mashabiki wake waliokuwa wakimganda. Jackson alikuwa na mademu.

Mfalme huyo wa pop alikuwa akitumia muda wa faragha na mwanamke nyuma ya pazia kwenye siti ya nyuma ya gari wakati walinzi wakiendesha. Wanadai kuwa Jackson alikuwa akipenda wasichana na walimuona kwa macho yao akiwabusu. Wanawake hao, ambao walinzi waliamini walikuwa wakitokea Ulaya, hawakuwahi kwenda nyumbani kwake na hawakuwahi kukutana na wanae.

Alikuwa akirudi nyumbani kutoka kwenye mishe zake kabla ya wanae Prince, Paris na Blanket hawajaamika. Jackson aliwaagiza walinzi wake kuwazuia kaka zake, dada zake na baba yake kuingi kwake japo mama yake alikuwa akiruhusiwa kuingia nyumbani kwake.

Pamoja na kuwa hayupo tena, muziki wa Michael Jackson bado unaendelea kutoka ambapo sasa album yake Xscape ipo sokoni na iliuza kopi milioni 2.3 katika wiki tatu tangu itoke mwezi May. Ukurasa wake wa Facebook una likes milioni 75 ziadi hata Justin Bieber, Lady Gaga, Katy Perry, Taylor Swift na Bruno Mars.

Chanzo: CNN. Soma zaidi makala hiyo hapa.

Saturday, June 21, 2014

Meet Africa's first female captain flying the Dreamliner



Rubani wa kike wa Kenya, Irene Koki Mutungi ndiye rubani wa kwanza mwanamke wa Afrika kupaisha ndege kubwa aina ya Boeing 787 Dreamliner. Tazama mahojiano haya aliyofanyiwa na KTN.

Friday, June 13, 2014

Leo ni mwaka mmoja tangu Langa Kileo afariki dunia


Wakati ambapo mashabiki wa muziki wa Hip Hop nchini walikuwa wameanza kusahau majonzi ya kumpoteza Albert Mangweha aka Ngwair mwezi May mwaka jana, June 13, 2013 walitoneshwa tena kwa kifo cha mwana hip hop mwingine, Langa Kileo aka Lyrically And Naturally Gifted African.
Kwa mujibu wa Afisa Uhusiano wa hospitali ya taifa ya Muhimbili, Aminiel Aligaesha Langa alifariki une 13, saa 11 jioni baada ya kufikishwa hospitalini hapo tangia juzi mida ya jioni. Taarifa za awali zilidai kuwa Langa alikuwa anaumwa Malaria kali iliyopelekea kukimbizwa Muhimbili jana jioni.
Langa alikuwa ni mmoja wa matunda ya shindano la muziki la Coca-Cola Pop Stars mwaka 2004 ambalo washindi wake waliounda kundi la Wakilisha akiwa pamoja na Sarah Kaisi `Shaa’ na Witness Mwijage `Witness’ ambapo walitamba na nyimbo kama Unaniacha Hoi na Kiswanglish. Langa alizaliwa Desemba 22, 1985 jijini Dar es Salaam katika familia ya wanandoa Vanessa Kimei na mumewe Mengisen Kileo.
Alisoma Shule ya Msingi Olympio na Sekondari ya Loyola, zote za jijini Dar es Salaam. Hata hivyo, akiwa kidato cha pili alihamishiwa Kampala, Uganda katika Shule ya Vienna na baadaye shule ya Hillside International Academy, huko huko Uganda. Baadaye alirejea nchini na kujiunga na masomo ya Stashahada ya Masoko katika Chuo cha Biashara Dar es Salaam (CBE), Kampasi ya Dodoma (Global Publishers).
Wasanii na watu mbalimbali walituma salamu zao za rambirambi kwa familia ya Langa na kuomboleza kifo hicho.

Joh Makini

Wiki mbili nyuma tulipanga kufanya trak kwa Dunga tukaisogeza mbele kupisha msiba wa Ngwea nakumbuka mpaka session alipanga alhamis aliamplz tumalize msiba lkn kumbe yeye ndio alikua anafata daah! Mara ya mwisho kuongea ni uliponiambia nichek beat kwenye email alaf tuchangie mawazo kutakufuta idea daaah! Baadae tena ukanitext umepata idea mbili platinum ideas tukienda studio tunaua! Sasa umeondoka ghafla mimi na dunga tumebaki na beat tu sasa #RIP LANGA.

THE CITY of PHD ‏

DAAAAAAAH MUNGU TUSAIDIE!!MI NIMESHAKOSA AMANI KABISA HAPA NILIPO!!!HAYA NI MAJONZI MAKUBWA!!REST IN PEACE LANGA!!GONE TOO SOON!!DAAAAAH

Nick Mweusi

KAMA HIZI HABARI ZA LANGA NI KWELI SHOW YANGU NA GNAKO CLUB KAKALA HAiTAfANyIKA. RIP LANGA

Afande Sele The’King

Tunavyotaka sisi, sivyo anavyotaka yeye (Mungu) mapenzi yake ni zaidi.
 Mungu akupumzishe pema LANGA KILEO

K Wa MaujanjaSaplayaz

Kapumzike na amani zote hatuta acha kukukumbuka daima
 Mad Ice

Oh lord shed light on these dark moments of the Tanzanian Music Industry! Its not even a week since we buried Ngwea and another one is down :(… R.I.P Langa!

Cpwaa

Another Brother, Another Soldier, Another buddy,another talented Tanzanian Hip Hop Artist gone!……bado siamini.. #RIPLanga #BongoFlavaStayCalmAndUnited

Fina Mango ‏

RIP Langa. Pole sana Mama na Mzee Kileo Mungu awake nguvu Kwa wakati huu mgumu

D knob ‏

Rip Langa. Sijui cha kuongea kiukweli Dah.

Nikki Mbishi

Langa unaenda wapi kichaa wangu?Mwanao bado nalia na Ngwea halafu unasepa badala ya kubaki tuanue matanga.

LANGA NDANI YA THE JUMP OFF WITH JABIR SALEH

Thursday, June 12, 2014

Picha:Mabanda ya wafanyabiashara wa soko la Karume yateketea kwa moto


Moto mkubwa umetetekeza kabisa soko kubwa kabisa la mitumba la karume jijini Dar es Salaam usiku wa Jumatano, na kusababisha hasara kubwa kwa wafanyabiashara wote wa soko hilo.
Baadhi ya mabanda yakiteketea kwa moto

 Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, wamedai moto huo ulianza kuteketeza mabanda hayo majira ya saa 4 usiku, huku wakijaribu kutafuta msaada kuuzima bila mafanikio yeyote.

Wazima moto walifanikiwa kuudhibiti moto uloweza kufikia karibu na kiwanda cha Breweries, lakini haujasababisha hasara yeyote katika nyumba za jirani wa soko hilo kwa mujibu wa mwandishi habari wa Raia Mwema Mbaraka Islam alipozungumza na Sauti ya Amerika.

Anasema hakuna kibada cha biashara kilichosalimika na hakuna mtu aliyefanikiwa kuokowa mali yake. Mfanya biashara Wilson magembe anasema amepoteza kila kitu na ilikuwa vigumu kuweza kuchukua bidhaa zao kwa sababu moto uliwaka kwa haraka sana.







Picha: Jennifer Lopez na Pitbull wapamba sherehe za ufunguzi wa kombe la dunia 2014, Brazil





Maelfu ya mashabiki wamejitokeza jioni ya leo kwa saa za Brazil (June 12) katika sherehe za ufunguzi wa fainali za kombe la dunia 2014 kwenye uwanja wa ‘Arena de Sao Paulo’ nchini Brazil, ambapo Jennifer lopez, rapper Pitbull na mwimbaji wa Brazill Claudia Leitte wametumbuiza mbele ya mashabiki waliofurika kwa wingi na kuimba wimbo rasmi wa kombe la dunia kwa mwaka huu ‘We Are One (Ola Ola)’.Maandalizi ya sherehe hizo za ufunguzi yalifanywa kuanzia March mwaka huu, na jumla ya masaa 84 yalitumika kwaajili ya rehearsal za sherehe hizo.Mechi ya ufunguzi wa michuano hiyo inafanyika usiku huu kati ya wenyeji Brazil na Croatia.



Brazil waanza vyema kombe la dunia kwa kuichapa Croatia 3-1


Wenyeji wa michuano ya kombe la dunia, Brazil wameianza vyema baada ya kuichapa Croatia mabao 3-1.


 Croatia ndio walikuwa wa kwanza kupata bao baada ya mchezaji wa Brazil Marcelo kujifunga katika dakika 11. Brazil walijipatia goli lao la kuwasazisha kutoka kwa Neymar aliyezitikisa nyavu za Croatia katika dakika ya 29 kwa shuti la umbali wa yards 25. Mpaka timu hizo zinaenda mapumziko magoli yalikuwa 1-1.



Katika dakika ya 70 referee wa mchezo huo Yuichi Nishimura aliwapa penalty Brazil iliyotumiwa vyema na Neymar aliyeipa Brazil bao la pili.

Wakati zikiwa zimesalia dakika 2 kumalizika kwa mchezo huo, Brazil waliongeza bao la tatu lililofungwa kirahisi na Oscar aliyemwacha mlinda mlango wa Pletikosa akijitupab kujaribu kuuokoa bila mafanikio.

Ushindi wa Brazil umepokelewa kwa furaha kubwa na mashabiki wengi waliokuwa wamefurika kwenye uwanja uliopo mjini Sao Paulo.

Michuano hiyo inaendelea tena Ijumaa hii kwa mechi ya Mexico vs Cameron, Spain vs Netherlands na Chile vs Australia.

Agnes Masogange afunguka maisha yake ya jela yalivyokuwa

Wednesday, June 11, 2014



Tuesday, June 10, 2014

French Montana performing at the MTV MAMA, Durban, SA

Khuli Chana and other South African bands performing at MTV MAMA, Durban

Trey Songz performing at the MTV MAMA, Durba, SA

Miguel performing at the MTV MAMA, Durban, SA

Diamond Platnumz and Davido performing at the MTV MAMA, Durban, SA

Monday, June 9, 2014

Ubakaji 'Silaha ya vita'



Viongozi wa kimataifa wanakutana jijini London kwa wiki nzima, kwa kongamano la kumaliza dhulma za kimapenzi katika mataifa yanayokabiliwa na mizozo.Mkutano huo, wa siku nne umeandaliwa na Waziri wa masuala ya nchi za kigeni wa Uingereza, William Hague na muigizaji maarufu na mjumbe maalum wa Umoja wa mataifa, Angelina Jolie. Kongamano hilo linajiri huku mataifa kadhaa barani Afrika yakikabiliwa na changamoto ya kumaliza ubakaji unaotumiwa kama silaha ya kivita. Ni mwanzo wa kuidhinishwa kampeni ya miaka miwili kutoa uhamasisho kuhusu kutumiwa kwa ubakaji na unyanyasaji wa kimapenzi kama silaha wakati wa vita. Waandalizi wa kongamano hilo wanasema wanataka huu uwe wakati ambapo ulimwengu utazinduka na kutangaza kwamba unyanyasaji wa kimapenzi sio jambo lisiloweza kuepukika wakati wa vita. Ujumbe ni ubakaji sio jambo lisiloweza kuepukika wakati wa vita. Uwajibikaji wa kimataifa Tangu William Hague na Angelina Jolie wazinduwe kampeni hiyo, mataifa mia moja na arobaini na nane yameidhinisha azimio la uwajibikaji wa kumaliza unyanyasaji huo wa kimapenzi katika mizozo. Lakini lengo sasa ni kuchukua hatua madhubuti, kuendeleza uchunguzi na kuripotiwa kwa visa hivyo vya unyanyasaji wa kimapenzi. Pia katika kutoa usaidizi zaidi kwa waathiriwa na kuhakikisha kuwa usawa wa kijinsia unahimizwa katika operesheni za siku zijazo za kulinda amani.  Kiwango cha jukumu hilo ni kikubwa: katika miaka ya tisaini, vita vya Bosnia vilisababisha kuwepo takriban waathiriwa elfu hamsini wa unyanyasaji wa kimapenzi. Takriban miongo miwili tangu vita hivyo vimalizike, ni wahalifu wapatao 60 pekee walioshtakiwa.

Wanawake 20 wanaume 3 watekwa Nigeria


Wapiganaji wanaoshukiwa kuwa wanachama wa Boko Haram wamewateka nyara wanawake 20 kutoka jamii inayohamahama Kaskazini Mashariki mwa Nigeria.

Wanawake hao walichukuliwa katika Makazi ya Gakini Fulani karibu na mji wa Chibok ambako zaidi ya wasichana wanafunzi 200 walitekwa nyara Aprili, mwaka huu.
Walioshuhudia tukio hilo walisema kuwa wapiganaji hao waliokuwa wamejihami kwa bunduki waliwalazimisha wanawake hao kuingia katika magari yao kabla ya kutoroka nao katika Jimbo la Borno.

Mlinzi mmoja wa kijiji alisema kuwa washambulizi hao pia waliwateka nyara wanaume watatu waliojaribu kuwazuia wasiondoke na wanawake hao.

Hadi sasa jeshi halijasema lo lote kuhusiana na tukio hilo.

Shambulio hilo lilitokea katika mji wa Chibok ambako wapiganaji wengine wa silaha waliwteka nyara zaidi ya wasichana 200 wanafunzi Aprili, mwaka huu.

Wakati huo jeshi la Nigeria limesema kuwa limewaua wapiganaji 50 katika kampeni yake dhidi ya magaidi mwishoni mwa wiki katika majimbo la Borno na Aladawa.

Mfululizo wa mashambulizi Kaskazini Mashariki mwa taifa hilo umeimarisha ukosoaji wa vyombo vya usalama vya Serikali.

Licha ya kuwepo kwa hali ya hatari katika eneo la Kaskazini Mashariki mwa Nigeria wanajeshi hawajachukua hatua dhabiti na wakati mwingine hawapo wakati washambulizi wanaotekeleza uhalifu wao