MICHAKATO

Levis Rocky Ndekeno

This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Pages

Saturday, January 18, 2014

KUNA UWEZEKANO MKUBWA KESHO KUTANGAZWA MAWAZIRI



Zipo taarifa  kuwa  Ikulu kesho  imetoa  mwaliko kwa wanahabari nchini na  yawezekano wito huo ukaenda sanjari na  kutangaza  mawaziri  walioteuliwa  kuziba nafari  za  mawaziri  wanne  waliotenguliwa  nafasi  zao na ile  ya  aliyekuwa  waziri  wa  fedha  marehemu Dr Wiliam Mgimwa  ama  yawezekana  wito huo ukawa wa  tofauti na hayo  kwani  yote  yanawezekana  ila  tuombe tufike  salama kesho jumapili
                                                 ............................................
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
 Katibu Mkuu Kiongozi na Mkuu wa Utumishi wa Umma, Balozi Ombeni Y. Sefue ambaye ni Katibu wa Baraza la Mawaziri, kesho, Jumapili, Januari 19, 2014, saa 5 asubuhi atazungumza na waandishi wa habari katika mkutano utakaofanyika Ikulu, Dar es Salaam.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu, DAR ES SALAAM.
18 Januari, 2014

Miraji Kikwete na Aima Mahmoud wakiondoka kwenye ukumbi wa Mlimani City baada ya kufunga ndoa yao jana.



Shamra shamra na nderemo zilitawala jana kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Mlimani City wakati Miraji Kikwete, mtoto wa Rais wa Tanzania, Jakaya Kikwete alipofunga ndoa na Alma Mahmoud.
Sherehe hizo zilianza saa 7:00 mchana baada ya ndoa kufungwa na maharusi hao kuingia ukumbini hapo wakiongozana na Rais Kikwete.
Hali nje ya ukumbi huo ilikuwa tulivu ingawa uwanja ulikuwa umefurika magari ya polisi, viongozi na wageni waalikwa. Huku kikosi cha kudhibiti ulinzi na usalama kikiwa kimefunga mitambo ndani na nje ya ukumbi huo.
Ulinzi katika eneo hilo ulikuwa ni mkali kupita kiasi ambapo hakuna yeyote aliyeruhusiwa kuingia ukumbini humo bila kadi maalumu, hata angeomba kwa kupiga magoti.
“Hata sisi tumetoka Bagamoyo hadi hapa tuna undugu kabisa na mkubwa (Rais Kikwete), lakini wametunyima kwa sababu hatuna kadi,” alilalamika mwanamke mmoja aliyeongozana na wanaume wawili.
Hakuna waandishi wa habari walioruhusiwa kuingia ndani ya ukumbi huo, isipokuwa waandishi na wapiga picha maalumu wa Serikali ambao walipewa vitambulisho maalumu na tisheti.
Wengine walioonekana wakipiga picha ni wanafamilia ambapo watoto wa kiume wa Rais Kikwete, walionekana wakiwa na kamera huku wamevalia kanzu nadhifu.
Mfanyakazi mmoja wa Ikulu alipomwona Mwandishi wa gazeti hili, alimfuata na kumwambia kuwa sherehe hiyo ni ya kibinafsi na haruhusiwi mwandishi yeyote kufanya kitu chochote.
“Tumenyimwa kuruhusu waandishi kwenye sherehe hii, sawa wewe ni mwandishi lakini hii ni sherehe binafsi na ya kifamilia, huruhusiwi kupiga picha yeyote,” alisema mfanyakazi huyo, jina linahifadhiwa.
Hata hivyo, mwandishi alitumia mbinu kupata picha za maharusi hao pamoja na matukio mengine yaliyokuwa yakiendelea ukumbini hapo.
Wageni wengi waalikwa walianza kuingia ukumbini humo majira ya mchana na wengine waliendelea kuwasili hadi saa 11 za jioni.
Miongoni mwa viongozi wa kitaifa waliohudhuria sherehe hizo ni pamoja na Makamu wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilal, Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi, Waziri wa Afya, Dk Hussein Mwinyi, Naibu Waziri wa Afya, Dk Seif Rashid na Waziri wa Maendeleo ya Wanawake Jinsia na Watoto, Sophia Simba

PICHA YA LEO: BARABARA YA MAGARI YAENDAYO KASI ZAGEUKA KUWA MADAMPO



Hii ni Barabara Mpya kabisa ya Magari yaendayo kwa kasi Jijini Dar es salaam ambapo sasa Baadhi ya maeneo yamegeuka Madampo ya kutupia takataka kama inavyo onekana pichani.Ina maana uongozi wa jiji hamjaliona hili? Picha na  Levis Ndekeno