MICHAKATO

Levis Rocky Ndekeno

This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Pages

Saturday, February 1, 2014

Japan kujenga reli iliyobomolewa na mafuriko Morogoro

Makamu wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan, Mitsuya Norio (Kushoto), akiwa na Naibu waziri wa uchukuzi, Dk. Charles Tizeba, wakati walipotembelea miundombinu ya reli jijini Dsm jana.



Serikali ya Japan imeahidi kukarabati kipande cha reli kinachosumbua mara kwa mara kilichoko kati ya Kilosa na Dodoma.

Hayo yalielezwa jana na Naibu Waziri wa Uchukuzi Dk. Charles Tizeba, wakati wa ziara ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan, Norio Mitsuya, aliyetembelea bandari ya Dar es Salaam na kampuni ya reli (TRL) kujionea uendeshaji.

Ziara hiyo ni utekelezaji wa ahadi ya Waziri Mkuu wa Japan Shinzo Abe, alizotoa wakati wa ziara ya Afrika ili kuisaidia sekta ya miundombinu.
Alisema baada ya waziri huyo kujionea shughuli mbalimbali, kwa niaba ya serikali yake ameahidi kuisaidia Tanzania kuimarisha reli na bandari.

Aliongeza kuwa juzi kampuni hodhi ya miundombinu ya reli (Rahco) na TRL zilifanya tathmini ya eneo la Kilosa hadi Dodoma ambapo serikali hiyo iliahidi kulikarabati.
Aliongeza kuwa, baada ya ukarabati huo Japan itasaidia kuitengeneza rasmi ambapo gharama yake itajulikana pale tathmini itakapofanyika. Alisema nia ya kuisaidia Tanzania kwenye usafiri wa reli ni ya muda mrefu na kwamba kwa sasa wanatimiza ahadi hiyo.

Kuhusu bandari ya Dar es Salaam, alisema Japan itaipanua kwa kutengeneza gati namba moja hadi saba. Waziri Mitsuya alisema lengo la ziara hiyo ni kuisaidia Tanzania katika kuboresha miundombinu kwa siku zijazo.

Awali, Waziri Tizeba alisema kuwa, vichwa 13 vya treni ambavyo wameviagiza nchini Marekani hivi karibuni vinatarajia kuingia mwishoni mwa mwaka huu. Aliongeza vichwa hivyo vinagharimu zaidi ya Shilingi bilioni 50.
Katika ziara hiyo, waziri wa Japan alipata nafasi ya kusafiri na treni ya Dar es Salaam kutoka stesheni hadi Ubungo.

Pinda: Tanzania itanufaika na uwekezaji ikizingatia mfumo wa uwekezaji

Waziri Mkuu Mizengo Pinda, amesema Tanzania ni miongoni mwa nchi zitakazonufaika katika masuala ya uwekezaji endapo itatekeleza mapitio ya mfumo wa uwekezaji yaliyoandaliwa na taasisi ya washirika walioendelea kiuchumi.

Pinda aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaa wakati akizindua taarifa ya uwekezaji.
Alisema malengo ya mapitio ya mfumo huo ni kuboresha hali ya uwekezaji na biashara ambayo matokeo yake yatasaidia kuongeza wawekezaji katika maeneo mengi.

“Kuna maeneo ya uwekezaji yanayopata mitaji kutoka nje FDI ambayo ni umeme, mafuta, gesi, madini, viwanda, ujenzi na huduma za jamii.” 

Alisema matokeo ya jitihada hizo ni makubwa na yameonekana ndani ya miaka miwili baada ya utafiti wa ripoti hiyo kufanyika.

Alitolea mfano kilimo ambacho kimekua kutoka Dola za Marekani milioni 304.5 mwaka 2010 hadi Dola milioni 355.4 mwaka 2011.
Pia alisema katika sekta ya umeme na gesi zimekua kutoka Dola milioni 328.6 hadi 539.8 mwaka 2011.

Pinda alisema hali hiyo imesababisha pato la taifa kuendelea kukua kwa asilimia sita kwa miaka kumi mfululizo ambapo kwa mwaka jana lilikua kwa asilimia saba na matarajio ni kufikia asilimia 7.2 kwa mwaka huu. 

Miongoni mwa maeneo yanayohusishwa na mfumo huu wa mapitio ya Uwekezaji ni yale yaliyoainishwa katika Matokeo Makubwa Sasa ambayo ni Kilimo, Maji, Uchukuzi, Elimu na Nishati. 

Aliomba wadau wote kwa kushirikiana na Sekta binafsi kuchambua kwa makini mapendekezo ya mapitio ya mfumo huo ambayo yanatumika pia kuharakisha mafanikio ya Matokeo Makubwa Sasa.

Naibu Katibu Mkuu wa Taasisi ya OECD, Bw. Rintaro Tamaki, alisema mazingira ya uwekezaji nchini yanabadilika kila mara kutokana na kuvumbuliwa kwa rasilimali mpya kama vile gesi, makaa ya mawe ambazo zinasababisha watu wavutiwe kuwekeza 
Aliitaka serikali kutozipuuza sekta kama ya kilimo na kueleza kuwa kinachotakiwa ni kuiboresha kwa kuanzisha viwanda ili kuongeza thamani ya mazao yenu.