MICHAKATO

Levis Rocky Ndekeno

This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Pages

Friday, February 21, 2014

Habari Ludewa Blog: WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA AONGOZA WAOMBOLEZAJI MSI...

Habari Ludewa Blog: WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA AONGOZA WAOMBOLEZAJI MSI...: Maziri Mkuu Mizengo Pinda akiongoza mamia ya waombolezaji kutoa heshima za mwisho katika msiba wa mke wa Mheshimiwa Jaji Damian Lubuva...

HABARI KWANZA: RAIS WA ZANZIBAR DKT. SHEIN AKUTANA NA WAZIRI WA B...

HABARI KWANZA: RAIS WA ZANZIBAR DKT. SHEIN AKUTANA NA WAZIRI WA B...: Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Waziri wa Biashara za Nje wa Uholan...

HABARI KWANZA: TAZAMA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE (FORM FOUR) 2013

HABARI KWANZA: TAZAMA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE (FORM FOUR) 2013: NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA CSEE 2013 EXAMINATION RESULTS ENQUIRIES LINK

Thursday, February 20, 2014

Facebook yasema itainunua WhatsApp

Kampuni ya mtandao wa Kijamii ya Facebook imesema kuwa itanunua mtandao wa mawasiliano ya ujumbe mfupi wa WhatsApp kwa kima cha dola bilioni kumi na sita, na nyongeza zaidi ya dola bilioni tatu zitakazolipwa waanzilishi wa mtandao huo pamoja na wafanyikazi wake.

Hiyo ndiyo biashara kubwa zaidi ya ununuzi kuwahi kutekelezwa na Facebook hadi kufikia sasa.

WhatsApp ni maarufu sana miongoni mwa vijana wanaotafuta kuepuka kulipia huduma ya kutuma ujumbe mfupi wa simu yaani SMS.

WhatsAp imeweza kuwasajili zaidi ya watumiaji milioni mia nne hamsini.

Katika taarifa, mwanzilishi wa Facebook Mark Zuckerberg amesema kuwa mtandao huo upo njiani kuwaunganisha watu bilioni moja jambo litafanya Facebook kuwa na thamani kubwa.

Sunday, February 16, 2014

Chadema yatishia kususia Bunge la Katiba

    Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) akimtambulisha Grace Tendega Dar es Salaam jana kwa waandishi wa habari kuwa mgombea wa Uchaguzi Mdogo Jimbo la Kalenga. (Na Mpigapicha Wetu).

WAKATI keshokutwa Bunge Maalum la Katiba linaanza kukutana mjini Dodoma, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema huenda kikasusia Bunge Maalum la Katiba iwapo litaendeshwa kwa kufuata matakwa ya chama cha siasa na siyo ya wananchi.

Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe alisema hayo jana wakati akielezea maamuzi ya Kikao cha Kamati Kuu (CC) kilichofanyika jana na kueleza kuwa chama hicho kinaenda katika Bunge hilo kikiwa na hadhari ya hilo.

Alisema wanaenda kwenye kikao hicho wakiwa na masikitiko kutokana na uteuzi wa wajumbe 201 wa bunge hilo waliotangazwa hivi karibuni kuwa karibu asilimia 75 hadi 80 ni wanaCCM.

Akijibu hilo, Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye alisema “Tumewazoea, sio mara ya kwanza kususa waache wasuse najua nia yao tangu mwanzo ni Katiba isipatikane. Katiba mpya itapatikana hata wakisusa”.

Naye Mbowe alifafanua “Hatuendi katika bunge hilo kugoma lakini mambo yakienda visivyo kwa kufuata matakwa ya chama cha siasa na siyo mapendekezo ya rasimu ya pili ya Katiba hiyo ambayo ni ya wananchi tutalizira Bunge hilo,” alisema.

Alibainisha kuwa chama hicho hawatasita kurejea kwa wananchi wakati Bunge likiendelea au likiwa limeisha iwapo wingi wa wabunge wa chama tawala utaathiri Bunge hilo.

“Sasa wananchi watatuelewa dhamira yetu ya kutaka wajumbe hao wasiteuliwe na Rais kwani tulibishana sana lakini baadaye tulikubaliana jambo ambalo limeonesha kwa kuteuliwa makada wengi kwa manufaa ya chama tawala,” alisema Mbowe.

Alisema ingefaa makundi yenyewe yangeteua wawakilishi wao na siyo kupeleka kwa Rais hivyo Bunge hilo linaloanza keshokutwa wanaenda kwa tahadhari.

Vikao vya Bunge Maalum la Katiba linatarajia kuanza keshokutwa likihusisha wajumbe ambao ni wabunge wote wa Baraza la Wawakilishi ,Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano na wajumbe 201 walioteuliwa na Rais Jakaya Kikwete akishirikiana na Rais wa Zanzibar Ali Mohamed Shein.

Wajumbe hao 201 wameteuliwa kutoka makundi tofauti yakiwemo ya Taasisi zisizo za kiserikali, vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu, Taasisi za dini, Taasisi za elimu, watu wenye ulemavu, vyama vya wafanyakazi, vyama vinavyowakilisha wakulima, wafugaji, wavuvi na kundi la watu wenye malengo yanayofanana.

Bunge hilo litahusisha wajumbe takriban 650 wanaokwenda kuijadili rasimu ya pili ya Katiba na watatumia siku 70 na iwapo hazitatosha wataongezewa siku 20 ili kukamilisha mjadala huo. Kitakachofuata baada ya Bunge Maalum la Katiba ni wananchi kupiga kura ya maoni kupitisha Katiba hiyo mpya.

Katiba hiyo mpya itafuta Katiba ya sasa iliyodumu tangu Tanganyika ilipopata uhuru mwaka 1961 na mabadiliko kadhaa yaliyofuatia baada ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Alipoulizwa Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye amesema “tumewazoea, sio mara ya kwanza kususa waache wasuse najua nia yao tangu mwanzo ni Katiba isipatikane. Katiba mpya itapatikana hata wakisusa”

JK achoshwa na Siasa chafu



MWENYEKITI wa Taifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete amewataka wanachama wake kuacha unyonge na kujibu mapigo ya wapinzani hasa wale ambao wanaendesha siasa za vurugu katika kampeni za chaguzi mbalimbali nchini.

Rais Kikwete amesema kuwa uvumilivu una ukomo, na kwamba sasa wanachama wa CCM hawana budi kuacha unyonge, kutokana na siasa hizo za vurugu zinazoendeshwa na vyama vya upinzani.

Aliyasema hayo jana mjini hapa wakati akifungua kikao cha kawaida cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM kitakachokutana kwa siku mbili chini ya uenyekiti wake, ambacho ajenda kuu ni kuzungumzia Bunge Maalumu la Katiba.

“Tumelizungumzia hili katika Kamati Kuu, tumekubaliana kuacha unyonge (makofi). Ndio watu wamelisema hili katika Kamati Kuu, tumesema jamani tumekubaliana kuacha unyonge,” alisema Rais Kikwete ambaye wakati anafungua kikao hicho waandishi wa habari walikuwamo, na akaongeza: “Wacha wakaseme (waandishi wa habari), ndio tumekubaliana kuacha unyonge. Kabisa. Hata kama leo katika taarifa za habari, zisiwekwe habari nyingine, msikike ninyi tu. Uvumilivu una ukomo wake.”

Mwenyekiti huyo wa CCM alisema wamefikia hatua hiyo kwa sababu yanayotokea yanasikitisha sana na akatoa mfano wa matukio kadhaa ya uvunjifu wa amani katika kampeni katika maeneo ya Igunga mkoani Tabora na Kahama mkoani Shinyanga.

“Maana tunashindana na wenzetu wagomvi maana wao ugomvi ndio sehemu ya mwongozo wa kufanya kazi ya siasa. Maana pale Kahama kijana wamemtoa macho kwa bisibisi. Acheni unyonge (makofi). “Nasema kwa kweli kwa sababu yanayotokea yanasikitisha. Pale Igunga kijana yule wamemmwagia tindikali, pale Kahama kijana wamemtoa macho kwa bisibisi. Tuache unyonge,” alisisitiza Rais Kikwete huku akishinikizwa kwa shangwe za CCM Oyee, Mapinduzi Daima.

Ingawa Rais Kikwete hakutaja chama, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimekuwa kikihusishwa na vurugu za uchaguzi katika maeneo mbalimbali yakiwamo ya Igunga na Kahama katika uchaguzi mdogo wa madiwani uliofanyika hivi karibuni na pia katika chaguzi ndogo za ubunge.

Pongezi za ushindi

Akizungumzia uchaguzi mdogo wa kata 27 zilizofanyika hivi karibuni na CCM kuzoa kata 23, Rais Kikwete aliwapongeza wanaCCM kwa ushindi huo, lakini akawapa changamoto ya kuhakikisha wanarejesha kata hizo nne zilizokwenda kwa vyama vya upinzani.

“Huu ni ushindi mkubwa sana, ushindi mnono. Ni vizuri kutumia nafasi hii kujipongeza na kuwapongeza wenzetu kwa kazi nzuri, kazi nzuri waliyoifanya ya kujenga chama,” alisema Rais Kikwete na kuongeza: “Lakini tukumbushane kwamba kata nne hatukuzipata, hivyo tuna kazi ya kuzikomboa, sisi wakati wote nia yetu ni kushinda, kushindwa haiwezekani.”

Aidha, alizungumzia uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kalenga mkoani Iringa, akisema hadi sasa hali ni shwari, hakuna migawanyiko wala misukosuko kama ilivyokuwa kwa Jimbo la Arumeru Mashariki ambalo alisema tangu mwanzo hadi mwisho, hali haikuwa shwari.

Alisema hadi sasa wana uhakika wa ushindi katika jimbo hilo, lakini akawataka wanaCCM kujiandaa vyema kwa kila hali na kuhakikisha ushindi unapatikana katika jimbo lililoachwa wazi kutokana na kifo cha aliyekuwa Waziri wa Fedha, Dk William Mgimwa.

Mwanawe Geoffrey ndiye mgombea wa CCM. Pia aliwataka wanachama na viongozi wa Jimbo la Chalinze mkoani Pwani, nao kujiandaa kwa uchaguzi mdogo kwa sababu tayari Spika wa Bunge, ametoa taarifa serikalini kuhusu kuwa wazi kwa jimbo hilo kutokana na kifo cha mbunge wake, Said Bwanamdogo.

“Msikae tu kusubiri na kuendelea kuomboleza, kwa sababu Serikali haiombolezi, wao wanachotaka ni uchaguzi ujazwe, shughuli ziendelee. Maana watu wanaweza kusema hata orobaini bado. Kule Arumeru tuliambiwa tumbo bado halijapasuka. Kwani kwa Mgimwa orobaini tayari, mbona mchakato umeanza. “Ninyi fanyeni mchakato, orobaini yetu mnaweza kufanya wakati mambo mengine yakiendelea. Tujiandae mapema ili kuhakikisha tunashinda,” alisema Mwenyekiti huyo wa CCM na kuwapongeza viongozi wa mkoa na wilaya waliofanikisha ushindi katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kiembesamaki ambako mgombea wao, Mahmoud Thabit Kombo alishinda.

Alisema CCM ilibidi kumtosa aliyekuwa mbunge wao, Mansour Yussuf Himid, kwa sababu alikuwa akivaa magwanda ya chama hicho, lakini alikuwa akipinga sera na taratibu za chama hicho tawala.

“Kila akifungua mdomo wake anaitukana CCM, kila akifungua mdomo anapingana na sera za CCM. Tukasema inatosha, bora kuwa na mpinzani huko nje kuliko huyu, ndio maana niliwahi kusema katika NEC moja hapa kuwa sijui mtu anasema nitahama CCM, nikasema nendeni sasa hivi,” alisema Kikwete.




Birdman atangaza kuandaa birthday party ya kufuru, itakagharimu tshs mil 800, itakuwa na models 30 watupu na wengine 700 waliovaa nguo...soma zaid hapa




Katika kusherehekea siku yake ya kuzaliwa ya miaka 45, Birdman ataangusha party ya nguvu itakayogharibu dola laki 5 (sawa na shilingi milioni 800) itakayokuwa na walimbwende watakaokuwa watupu, crew yote ya Young Money na gari zake zote zinazofikia thamani ya dola milioni 7.

 Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ, sherehe hiyo itafanyika Jumamosi usiku katikati ya NBA All-Star Weekend. Rapper huyo amekodi uwanja alioupa jina “Birdman’s New Era Voodoo Lounge.”
 Pamoja na wanawake 30 walio watupu, kutakuwa na models wengine 700 watakaovaa nguo. Zaidi ya hapo atasafirisha gari zake kutoka Miami ambazo kwa pamoja zina thamani ya dola milioni 7 zikiwemo Bugatti 2, Maybachs, 2 na basi 3 za tour.
 Wageni waalikwa ni pamoja na James Harden, Paul George, Blake Griffin, Shaq, Kenny Smith na rappers wa Young Money, Lil Wayne, Drake, Nicki Minaj, na wengine. Pia wasanii wa zamani wa Cash Money, Mystikal, Turk, Juvenile, na Mannie Fresh watakuwepo.

Sunday, February 2, 2014

WAUMINI wa Kanisa la Break Through Assemblies lililoko eneo la Boko Magengeni nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam linadaiwa kuuza Sakramenti kwa Sh 100,000 kwa kila muumini. Hatua hiyo inadaiwa kuwanyima wasio na fedha chakula hicho cha Bwana hivyo kusababisha malalamiko dhidi ya uongozi wa Kanisa hilo la Walokole.

Habari za uhakika zilizolifikia gazeti hili, zilisema tukio hilo lililoshangaza waumini lilitokea Januari 19. Kanisa hilo linaongozwa na Mchungaji Godfrey Simtomvu.

Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti, na kwa masharti ya kutotajwa majina, waumini walisema kitendo hicho kiliwashangaza siku hiyo kanisani hapo walikokuwa wamekwenda kwa ajili ya Ibada kama siku zingine.

Akisimulia, mmoja wao alisema baada ya Mchungaji kuhubiri, vililetwa vikombe na mikate ambayo hutumiwa kanisani kama ishara ya kushiriki pamoja Chakula cha Bwana. Makanisa mengine hutambua ibada hiyo kama ya Sakramenti ya Chakula cha Bwana.

“Baada ya vifaa hivyo kufika kanisani hapo vilionekana kuwa vichache tofauti na waumini waliokuwa kanisani hapo…ndipo Mchungaji alipopaza sauti kuwa mwenye Sh 100,000 na zaidi ndiye atakayeshiriki,” alisema na kuongeza kuwa Januari 26, alishindwa kuabudu kutokana na kitendo hicho.

Alisema baada ya kutamka hivyo, waumini wengi walinywea wakashindwa kusogea na kupisha watu wapatao 10; lakini baada ya kuona idadi imekuwa ndogo zaidi ikatangazwa kuwa hata wenye Sh 50,000 wanaweza kusogea mbele kushiriki.

Aliongeza kuwa wakati wote huo waumini walikuwa wakitazamana, wakijiuliza juu ya utaratibu huo mpya, jambo ambalo ni kinyume na ilivyokuwa awali kanisani.

Alisema Mchungaji baada ya kuona idadi ya waumini inazidi kupungua, akawatangazia kuwa wasiokuwa na fedha wajiandikishe kisha wapokee chakula hicho kisha na kesho yake wapeleke kiwango hicho cha fedha. Muumini mwingine alisema jambo lililoshangaza wengi ni utaratibu huo mpya ambao awali haukuwapo kwani walikuwa wakitangaziwa wiki moja kabla na kutakiwa kujitayarisha kwa ajili ya ibada hiyo ya Chakula cha Bwana.

“Awali Mchungaji alikuwa akitupa taarifa wiki moja kabla, akiwataka waumini kujitayarisha na kusafisha nyoyo zao kabla ya kushiriki kitendo hicho ambacho tuliamini kuwa ni kitakatifu na chenye mafundisho makubwa kwa waumini,” alisema na kuongeza kuwa hilo la kununua chakula lilizuka ghafla na hakujua hatma yake.

Mwingine alisema mbali na kununua chakula hicho, pia jambo lililozusha mshangao kwa waumini ni Mchungaji huyo kuleta watu kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kuhubiri Neno la Mungu akidai kuwa ni wahubiri ambao nao husisitiza neno la kutoa tu.

“Waumini tunaamini kuwa Bwana Yesu alitoa chakula hicho bure…iweje leo waumini wauziwe tena kwa kupangiwa kiwango?” Alihoji.

Akizungumzia madai hayo, Mzee wa Kanisa hilo alisisitiza kuwa yeye si msemaji wa Kanisa hilo na kusema madai hayo hayana ukweli na kwamba siku hiyo, Mchungaji hakumaanisha kwamba utakuwa utaratibu, bali ilikuwa ni kuhamasisha utoaji kwa muumini mwenye nacho. Alisema kufanya hivyo halikuwa lengo la kutafuta fedha bali kupeleka Neno la Mungu mbele.

“Msemaji wa Kanisa ni Mchungaji mwenyewe, ukiniuliza sana mimi utakuwa unanionea, kama unamtafuta na ukamkosa atakuwa redioni katika kipindi,” alisema mzee huyo.

Akizungumzia malalamiko hayo, Mchungaji Simtomvu alisema kutokea kwa hali hiyo si imani ya Kanisa hilo bali ilitokana na mhubiri kutoka Kongo ambaye alifunuliwa na Mungu na kutaka waumini kuweka maagano yao na Mungu kwa mwaka huu.

Alisema hayo yalikuwa mafunuo ya mtu na si imani na ni kitu ambacho hutokea mara moja tu na kutolea mfano wa yai linapouzwa kwenye mnada kwa bei kubwa, ingawa bei yake halisi inajulikana.

“Laiti ningemfahamu aliyeleta taarifa hiyo ningemsaidia, kwani amekengeuka, mbona Mchungaji TB Joshua wa Nigeria huuza maji katika vichupa vidogo kwa gharama kubwa inayoweza kufikia Sh 75,000,” alisema Mchungaji Simtomvu.


Alisema tukio hilo ilikuwa ni kwa muumini anayetaka kuweka agano na Mungu wake, kwamba mwaka huu amtendee mambo gani na kuhoji kuwa zipo imani za ajabu ajabu lakini haziripotiwi.

Saturday, February 1, 2014

Japan kujenga reli iliyobomolewa na mafuriko Morogoro

Makamu wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan, Mitsuya Norio (Kushoto), akiwa na Naibu waziri wa uchukuzi, Dk. Charles Tizeba, wakati walipotembelea miundombinu ya reli jijini Dsm jana.



Serikali ya Japan imeahidi kukarabati kipande cha reli kinachosumbua mara kwa mara kilichoko kati ya Kilosa na Dodoma.

Hayo yalielezwa jana na Naibu Waziri wa Uchukuzi Dk. Charles Tizeba, wakati wa ziara ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan, Norio Mitsuya, aliyetembelea bandari ya Dar es Salaam na kampuni ya reli (TRL) kujionea uendeshaji.

Ziara hiyo ni utekelezaji wa ahadi ya Waziri Mkuu wa Japan Shinzo Abe, alizotoa wakati wa ziara ya Afrika ili kuisaidia sekta ya miundombinu.
Alisema baada ya waziri huyo kujionea shughuli mbalimbali, kwa niaba ya serikali yake ameahidi kuisaidia Tanzania kuimarisha reli na bandari.

Aliongeza kuwa juzi kampuni hodhi ya miundombinu ya reli (Rahco) na TRL zilifanya tathmini ya eneo la Kilosa hadi Dodoma ambapo serikali hiyo iliahidi kulikarabati.
Aliongeza kuwa, baada ya ukarabati huo Japan itasaidia kuitengeneza rasmi ambapo gharama yake itajulikana pale tathmini itakapofanyika. Alisema nia ya kuisaidia Tanzania kwenye usafiri wa reli ni ya muda mrefu na kwamba kwa sasa wanatimiza ahadi hiyo.

Kuhusu bandari ya Dar es Salaam, alisema Japan itaipanua kwa kutengeneza gati namba moja hadi saba. Waziri Mitsuya alisema lengo la ziara hiyo ni kuisaidia Tanzania katika kuboresha miundombinu kwa siku zijazo.

Awali, Waziri Tizeba alisema kuwa, vichwa 13 vya treni ambavyo wameviagiza nchini Marekani hivi karibuni vinatarajia kuingia mwishoni mwa mwaka huu. Aliongeza vichwa hivyo vinagharimu zaidi ya Shilingi bilioni 50.
Katika ziara hiyo, waziri wa Japan alipata nafasi ya kusafiri na treni ya Dar es Salaam kutoka stesheni hadi Ubungo.

Pinda: Tanzania itanufaika na uwekezaji ikizingatia mfumo wa uwekezaji

Waziri Mkuu Mizengo Pinda, amesema Tanzania ni miongoni mwa nchi zitakazonufaika katika masuala ya uwekezaji endapo itatekeleza mapitio ya mfumo wa uwekezaji yaliyoandaliwa na taasisi ya washirika walioendelea kiuchumi.

Pinda aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaa wakati akizindua taarifa ya uwekezaji.
Alisema malengo ya mapitio ya mfumo huo ni kuboresha hali ya uwekezaji na biashara ambayo matokeo yake yatasaidia kuongeza wawekezaji katika maeneo mengi.

“Kuna maeneo ya uwekezaji yanayopata mitaji kutoka nje FDI ambayo ni umeme, mafuta, gesi, madini, viwanda, ujenzi na huduma za jamii.” 

Alisema matokeo ya jitihada hizo ni makubwa na yameonekana ndani ya miaka miwili baada ya utafiti wa ripoti hiyo kufanyika.

Alitolea mfano kilimo ambacho kimekua kutoka Dola za Marekani milioni 304.5 mwaka 2010 hadi Dola milioni 355.4 mwaka 2011.
Pia alisema katika sekta ya umeme na gesi zimekua kutoka Dola milioni 328.6 hadi 539.8 mwaka 2011.

Pinda alisema hali hiyo imesababisha pato la taifa kuendelea kukua kwa asilimia sita kwa miaka kumi mfululizo ambapo kwa mwaka jana lilikua kwa asilimia saba na matarajio ni kufikia asilimia 7.2 kwa mwaka huu. 

Miongoni mwa maeneo yanayohusishwa na mfumo huu wa mapitio ya Uwekezaji ni yale yaliyoainishwa katika Matokeo Makubwa Sasa ambayo ni Kilimo, Maji, Uchukuzi, Elimu na Nishati. 

Aliomba wadau wote kwa kushirikiana na Sekta binafsi kuchambua kwa makini mapendekezo ya mapitio ya mfumo huo ambayo yanatumika pia kuharakisha mafanikio ya Matokeo Makubwa Sasa.

Naibu Katibu Mkuu wa Taasisi ya OECD, Bw. Rintaro Tamaki, alisema mazingira ya uwekezaji nchini yanabadilika kila mara kutokana na kuvumbuliwa kwa rasilimali mpya kama vile gesi, makaa ya mawe ambazo zinasababisha watu wavutiwe kuwekeza 
Aliitaka serikali kutozipuuza sekta kama ya kilimo na kueleza kuwa kinachotakiwa ni kuiboresha kwa kuanzisha viwanda ili kuongeza thamani ya mazao yenu.