MICHAKATO

Levis Rocky Ndekeno

This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Pages

Monday, May 9, 2016

Lady Jaydee kuwasha moto kwenye ‘Naamka Tena Concert’ May 20

Kwenye tamasha hilo litakalofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City, Jaydee atatumbuiza pamoja na bendi yake.
Hiyo itakuwa ni show yake kubwa zaidi tangia atumbuize June 2013 kwenye show ya kihistoria ya miaka 13 kwenye muziki kipindi ametoa album yake ‘Nothing But The Truth.’
Hivi karibuni Jaydee aliachia kazi mpya inayotamba kwa sasa, Ndindindi ambayo itakapatikana kwenye album yake mpya, Woman.

Gadner G Habash kwa hili umeteleza kaka

Huwa nakuwa mzito sana kumshauri mtu anayenizidi umri, uwezo, status na tena ninayemchukulia kama moja wa role models wangu. Pale ambapo nitahitajika kufanya hivyo kutokana na uzito wa jambo lenyewe, huamua kutumia keyboard ya computer kuyasema yale ambayo naamini kwa uelewa wangu yanaweza kumjenga pia lakini nikiyasema kwa staha ya hali ya juu.
Gadner G Habash ni miongoni mwa watangazaji wa redio ninaowaheshimu katika muda wote. Si tu kwasababu ni mtangazaji mkongwe, bali pia ni mtangazaji mwenye sauti ya pekee hewani na mwenye busara inayoweza kuhamisha milima. Anapokuwa anaongea jambo, mamlaka anayoyaweka kwenye sauti, hukufanya kila neno limtokalo mdomoni likuingie vyema masikioni.

Na kwa hakika tangu aachane na mke wake, Lady Jaydee, amekuwa akijibu maswali yanayowahusu kwa werevu mkubwa. Miongoni mwa interview yake iliyonivutia sana ni ile aliyofanya na Zamaradi Mketema kwenye kipindi cha Take One cha Clouds TV.
“Siwezi kusema najuta kwamba [Jaydee] alitokea kwenye maisha yangu na siwezi kusema kwamba najuta tuliachana. Lakini ninachoweza kusema tu kwamba kwa suala la Jaydee ni suala ambalo nilichagua sana lisiwe ni jambo ambalo nalizungumzia au kulitolea comment kwasababu yule ni public figure unaposema kitu kuhusu yeye tafsiri zinakuwa ni tofauti na vile unavyotarajia,” alisema Gardiner.
“Kwahiyo sina majuto yoyote, na sina aina yoyote ya chuki au uadui na nategemea hata yeye atakuwa anafeel the same,” alisisitiza.
Pia nilipenda majibu yake ya maswali kuwa Ndindindi ni wimbo alioandikiwa na ex wake huyo.
Hadi hapo niliendelea kuamini kuwa mtangazaji huyo ameufunga ukurasa wake na Lady Jaydee kwa amani na kila mmoja ameangalia hamsini zake, maisha yanaendelea. Sishangai kabisa kama ukweli halisi ni kwamba wawili hao wanachukiana baada ya kuachana kwasababu ni kitu cha kawaida. Na mara nyingi chuki huwa kubwa pale pendo linapochanganyikana na chuki na hasira ya kutendwa au kwasababu yoyote ile inayomfanya mmoja wapo kukatisha uhusiano kwa kosa la mwingine.
Lakini nashangaa sana kwa mtu smart kama Gardiner kutamka maneno ya kumdhalilisha ex wake mbele ya kadamnasi. Kuna video imesambaa na naamini itakuwa viral sana wiki hii inayomuonesha mtangazaji huyo akiwa jukwaani kama mshereheshaji wa tukio moja jijini Dar es Salaam akiongea maneno makali kumhusu ex wake ambaye licha ya kutomtaja inajulikana wazi alikuwa anamuongelea nani.
“My name is Captain Gardiner G Habash all the way from Clouds FM, Jahazi hatari sana,” anasikika akisema kwenye kipande hicho cha video. “Na sina neno na yule mtoto wa kike. Nimeshamkojoza kwa miaka kama 15 hivi,” anasema Gardiner na kisha Dj anaucheza wimbo wa Lady Jaydee, Ndindindi. Mtangazaji huyo anaonekana kuucheza pia wimbo huo jukwaani huku watu wakimshangilia.
Nimependa ujasiri wa Gardiner katika kulisema jambo hilo na kudhihirisha kwa mara nyingine tena kuwa hana tatizo na ex wake lakini sijapendezwa na uchaguzi wake wa maneno. Kimsingi ni clip ambayo kwa namna nyingi inamdhalilisha ex wake lakini pia inamuondolea Captain ile busara ambayo najua anayo.
Sijachachagua kuiweka clip hiyo hapa kutokana na kilichosemwa lakini ningemshauri kaka yangu Gardiner kuendelea kusimamia busara yake aliyonayo siku zote na kujiepusha na kauli tata kama hizi ambazo mara nyingi huwa zina madhara kwenye brand. Video hiyo haijamdhilisha Jide tu bali wanawake wote ambao kwa hakika kwa kauli yake inawaelezea kama ni vyombo vya starehe tu.
Na utashangaa jinsi ambavyo video fupi kama ile ikaondoa heshima ya Gardiner aliyoitengeneza kwa muda mfupi. Matusi anayotukanwa sasa kwenye ukurasa wake wa Instaram yanatoa jibu la ni kwa kiasi gani watu hawajapendezwa na kauli zake. Pia ni kauli mbaya katika kipindi hiki ambacho amerejea kwa kasi Clouds FM kukalia kiti chake kilichoshindikana kukaliwa na watangazaji wengi.
Bahati nzuri binadamu husahau mapema, yataisha tu lakini ni vyema Captain akawa mwangalifu na kauli zake katika siku za usoni sababu ‘kile kinachotokea au kusemwa kwenye starehe hakibaki hapo tu.’

Nauli za Mabasi yaendayo haraka ziko hapa, siku mbili bure

Baada ya Kampuni ya UDA-RT kuwasilisha maombi ya nauli zitakazotumika kwa mabasi yaendayo haraka kwa Mamlaka ya udhibiti usafiri wa nchi kavu na majini (SUMATRA) May 09 206 SUMATRA imetangaza nauli hizo.
SUMATRA imesema kuwa njia ya pembezoni (Freeder Route) nauli ya mtu mzima ni 400 na mwanafunzi 200 na njia kuu (Trunk Route) ni 650 na mwanafunzi 200 na kwa abiria atakayetumia kusafiri njia kuu (Freeder Route) na kuendelea na safari kwa njia ya pembezoni nauli yake itakuwa ni 800 na mwanafunzi 200. 
Huduma hiyo itatolewa kuanzia kesho bure kwa wananchi kwa siku mbili na May 12 2016 zitaanza kutozwa nauli zilizotajwa.
Msimamizi wa mradi kutoka DART, Eng Ronald Lwakatare amesema>>>‘Wakati huo tunafanya majaribio tutakuwa tunaangalia mfumo unavyofanya kazi kwa hiyo tutawabeba abiria kwa siku kadhaa bila kulipa nauli’

Rais Magufuli asema yeye siyo katili, anawatumikia Watanzania ili kurejesha nchi kwenye mstari

Rais John Magufuli amewataka Watanzania wasimuone katili kwa kuwafukuza kazi baadhi ya watendaji wa Serikali, kwakuwa anataka kuirejesha nchi kwenye mstari.Akizungumza katika misa ya Jumapili kwenye Kanisa Katoliki Parokia ya Tokeo la Bwana Burka jijini Arusha, Rais Magufuli alisema watu katili ni wale ambao walikuwa wanawaibia Watanzania na kuwanyonya wanyonge.
Dk Magufuli alisema analazimika kuchukua hatua ya kuwafukuza kazi si kwamba ni katili, bali lengo ni kuwatumikia Watanzania na kuirejesha nchi kwenye mstari.
Alisema Tanzania ni taifa tajiri, hakuna sababu ya wananchi kulalamika kila kona, kwani kuna ardhi ya kutosha, madini ya kila aina, wanyama wa aina mbalimbali ambao baadhi wameanza hadi kupelekwa nje.
“Ninapochukua hatua nataka kuweka Tanzania iliyonyooka, mimi tayari nimesema nimejitoa sadaka kwa Watanzania hasa wanyonge,” alisema.
Aliongeza kuwa hatawaangusha Watanzania na hatabadilika, ataendelea kusimama na kutetea haki za Watanzania maskini na siku zote atatembea na maskini.

Mrisho Mpoto apata shavu la ubalozi wa kampeni ya ‘Kili Challenge’

 Msanii wa muziki wa asili, Mrisho Mpoto amepata shavu jipya la kuwa balozi wa kampeni ya ‘Kili Challenge’ itayokuwa inaelimisha jamii kuhusu kuendeleza mapambano dhidi ya Ukimwi.
Kupitia instagram, Mpoto ameandika:


Mgodi wa dhahabu wa Geita (GGM) kwa kushirikiana na Tume ya kupambana na kudhibiti Ukimwi nchini (TACAIDS) imeniteua kama msanii na mtanzania kuwa Balozi wa Kampeni ya Kili Challenge.
Napenda kuwashukuru sana TACAIDS na GGM kwa kuniamini na kunipa fursa hii ya kipekee.
Naomba nitoe wito kwa watanzania na waafrika wote kuwa tuendelee na mapambano dhidi ya Ukimwi. Tuzungumze na tuchukue hatua dhidi Ukimwi ili tufikie lengo la Kampeni ikiwa kama lengo letu sote tuhakikishe tunafikia idadi ya Zero katika Maambukizi Mapya, Zero ya Unyanyapaa, Zero ya vifo vitokanavyo na Ukimwi.

Picha: Msichana asiye na mikono ashinda tuzo la muandiko bora


 Msichana wa miaka saba aliyezaliwa bila mikono ameshinda shindano la muandiko mzuri nchini Marekani.
Anaya Ellick kutoka Chesapeake, Virginia hatumii viungo vya kumsaidia wakati anapoandika.
Wakati anapoandika yeye husimama huku akishikilia kalamu yake katika mikono.
Mwalimu wake mkuu Tracy Cox kutoka shule ya Greenbrier Christian amemtaja kuwa mtu wa mfano mwema.
“Yeye uhakikisha kuwa hakuna kitu kinachomzuia kufanya atakalo”, alisema Cox.”Ni mkakamavu na ana muandiko mzuri katika darasa lake”.
Msichana huyo anadaiwa kuwashinda washindani wengine 50 ili kushinda taji hilo la kitaifa.
Orodha hiyo ya tuzo huwazawadi wanafunzi wenye akili, matatizo ya kimwili, au ulemavu endelevu




NE-YO kutumbuiza Mwanza May 21


Mwanamuziki nguli kutoka nchini Marekani NE-YO anayetamba kwa muziki wa kizazi kipya anatarajia kufanya ziara nchini mwezi huu kwa mwaliko wa kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania kwa kushirikiana na Jembe Media Limited.Akitangaza ujio wa mwanamuzi huyo, Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu alisema NE-YO atawasili nchini Mei 19 na Mei 21 atatoa burudani ya aina yake katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza kwenye tamasha la Jembeka na Vodacom 2016 liloandaliwa na kampuni ya Jembe chini ya udhamini mkuu wa Vodacom Tanzania.Nkurlu alisema kuwa Vodacom imedhamini ujio wa mwanamuziki huyu kwa ajili ya kuwapatia burudani ya kimataifa wateja wake na watanzania wote kwa ujumla kupitia tamasha lake la Jembeka na Vodacom 2016.“Vodacom tunaamini kuwa wateja wetu wanahitaji kupata burudani baada ya majukumu ya kazi ya kila siku ndio maana tumekuwa tukidhamini michezo na matamasha mbalimbali ya muziki kwa ajili ya kuwapatia burudani kama ambavyo tumefanikisha kumleta NE-YO nchini,” alisema Nkurlu.Aliongeza kuwa mbali na kukonga nyoyo za wapenzi wa muziki NE-YO anayetamba kwa vibao maarufu baadhi yake vikiwa ni Let Me Love You, Beautiful Monster, Coming With You na She Knows featuring Juicy J atashiriki katika shughuli za kusaidia jamii kupitia taasisi ya Vodacom Foundation pia atashiriki katika hafla ya uzinduzi wa duka la Vodacom lililopo kwenye Mall kubwa jijini Mwanza.Aliwataka wasanii wa hapa nchini na wananchi kwa jumla kujitokeza kwa tamasha hilo ili wapate burudani ambapo pia wasanii watapata fursa ya kujifunza mambo mbalimbali na kubadilishana uzoefu na mwanamuziki huyu wa kimataifa.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi wa Tamasha la Jembeka festival 2016, Costantine Magavilla,alisema kuwa wanayo furaha kumleta mwanamuziki NE-YO kwenye tamasha hili na wana imani kuwa wapenzi wa muziki nchini watapata burudani iliyokuwa na hadhi ya kimataifa kutoka kwa msanii huyo.Alisema tamasha la Jembeka na Vodacom litaendelea kufanyika kila mwaka na litakuwa linasambaza burudani za kila aina kwa wapenzi wa muziki na burudani katika kona zote za Tanzania “Wapenzi wa muziki tunawataka wakae mkao wa kula kwa kuwa tutazidi kuuwapatia burudani za muziki wa hapa nchini na wa kimataifa.