MICHAKATO

Levis Rocky Ndekeno

This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Pages

Thursday, February 4, 2016

Upimaji wa ubikira wakosolewa Afrika Kusini

Waziri mmoja wa Afrika Kusini ameshtumu kuwa kinyume cha sheria ufadhili wa elimu ya wasichana wanaopita kipimo cha ubikira.
Mwezi Uliopita,Manispaa ya uthukela katika jimbo la Kwazulu Natal nchini Afrika Kusini ilisema itawapa zawadi wanafunzi 16 wa kike kwa masharti kwamba wasalie mabikira.
''Mpango huo ulilenga kupunguza maambukizi ya virusi vya HIV na mimba za mapema miongoni mwa wasichana'',alisema Meya Dudu Mazibuko.
Katika taarifa ya gazeti la Daily Maverick,waziri wa maendeleo ya kijamii Bathabile Dlamini alielezea upimaji wa ubikira kama usiowezekana,mchafu na ukiukaji mkubwa na haki za kibiniaadamu.
''Kujamiana kwa mara ya kwanza hakutakikani,licha ya hilo kuna unyanyapaa miongoni mwa wasichana ambao hufeli kipimo hicho'',alisema,akiutaja mpango huo kama ''kosa la kingono''.
Bi. Dlamini ,ambaye ni kiongozi wa chama tawala cha ANC upande wa wanawake ndio kiongozi mwenye hadhi ya juu kupinga kipimo hicho.

Wanaotuhumiwa kumvua nguo Mtanzania mbaroni India

Wanaume wanne wanaotuhumiwa kuhusika katika kumshambulia na kumvua nguo mwanafunzi wa kike kutoka Tanzania wamekamatwa, shirika la habari la AP limeripoti.
Waziri wa mashauri ya kigeni wa India Sushma Swaraj, aliandika kwenye Twitter kwamba amezikitishwa sana na “kisa hicho cha aibu” kilichotokea Jumapili eneo la Bangalore.
Bi Swaraj amesema polisi wamewakamata washukiwa wanne ambao watafunguliwa mashtaka.
Wanafunzi Waafrika mjini Bangalore wamesema wanaishi na hofu ya kushambuliwa.
Bw Bosco Kaweesi, mshauri wa kisheria wa Chama cha Wanafunzi kutoka Afrika, anasema wanafunzi wengine watatu wa kike kutoka Tanzania waliokuwa pamoja na mwanafunzi huyo garini pia walipigwa.
Gari lao liliteketezwa.
Kaweesi amesema huenda kisa hicho kilitendeka kimakosa, akisema gari la wanafunzi hao lilikuwa limefuata gari la mwanafunzi kutoka Sudan ambalo lilimgonga na kumuua mwanamke aliyekuwa amelala pembezoni mwa barabara.
Wanafunzi hao hawakumfahamu mwanafunzi huyo wa kiume aliyetoka Sudan, ambaye pia alipigwa na gari lake kuteketezwa.

Trump ataka mchujo wa Iowa urudiwe


Donald Trump anataka uchaguzi wa mchujo wa kuteua atakayegombea urais kupitia chama cha Republican katika jimbo la Iowa urudiwe, akisema mshindi Ted Cruz alitumia ulaghai.
Bw Trump anasema wakati wa kikao cha Iowa, maafisa wa kampeni wa Cruz waliwaambia wapiga kura kwamba mgombea mwingine Ben Carson alikuwa amejitoa kwenye kinyang’anyiro hicho, habari ambazo hazikuwa za kweli.
Maafisa wa kampeni wa Cruz baadaye walimuomba radhi Carson, wakisema lilikuwa kosa lisilokusudiwa.
Bw Trump alimaliza wa pili katika mchujo huo wa kwanza kufanyika nchini humo kwa ajili ya uchaguzi mkuu baadaye mwaka huu.
Mchujo utakaofuata utafanyika New Hampshire Jumanne ijayo.
"Ted Cruz hakushinda Iowa, aliiba. Hii ndiyo maana kura zote za maoni zilionekana kukosea na ndiyo sababi alipata kura nyingi kuliko ilivyotarajiwa. Ni vibaya!,” Bw Trump amesema.
Awali, alikuwa ameandika kwenye Twitter kwamba Bw Cruz alishinda mchujo wa Iowa kwa njia haramu, lakini baadaye akafuta ujumbe huo.
Matamshi ya Bw Trump ni kinyume na hotuba yake ya kukubali kushindwa ambayo aliitoa Jumatatu usiku baada ya matokeo kujulikana, jambo ambalo lilishangaza wengi ikizingatiwa ukali wake.
Kambi ya Cruz haijafurahishwa na madai ya sasa ya Bw Trump.
“Ukweli umemfika nyota huyu wa runingani – alishindwa Iowa na sasa hakuna anayezungumza kuhusu ubabe wake, kwa hivyo anachomoza kwenye Twitter,” afisa wa mawasiliano wa Bw Cruz Rick Tyler aliandikia Politico kupitia barua pepe.
“Kuna makundi yanayosaidia watu kudhibiti uraibu wa kutumia Twitter, labda anafaa kuwasiliana na tawi moja.”
Katika historia, haijatokea uchaguzi wa mchujo ukarudiwa.
Bw Carson alikubali ombi la msamaha kutoka kwa Bw Cruz lakini maafisa wake wa kampeni wamesema kambi ya Cruz ilitumia “mbinu chafu”.
Jumatano, seneta wa Kentucky Rand Paul na seneta wa zamani wa Pennsylvania Rick Santorum walijitoa kwenye kinyang’anyiro cha kutafuta tiketi ya chama cha Republican baada ya kutofanya vyema Iowa.

Obama awakemea wanaoshtumu Waislamu


Rais Barrack Obama ameshtumu kile alichokitaja kuwa Matamshi machafu dhidi ya Uislamu,kufuatia tamko la hivi majuzi lililotolewa na mgombea wa urais kupitia tiketi ya Republican Donald Trump.
Katika ziara yake ya kwanza katika msikiti kama rais,Obama amesema kuwa matamshi machafu dhidi ya waislaumu hayakubaliki nchini Marekani.
Aliwapongeza Wamarekani Waislamu kama walio na heshima na uzalendo wa hali ya juu na taifa lao.Bwana Trump ametoa wito kwa waislamu kutoruhusiwa kuingia nchini Marekani.
Obama alikuwa akizungumza katika msikiti wa jamii ya waislamu mjini Baltimore Maryland.
Ametembelea misikiti katika maeneo mengine ya dunia katika ziara rasmi katika kipindi chake cha miaka saba akiwa rais.
Ikulu ya Whitehouse imesema kuwa ziara hiyo ni kutetea uhuru wa kidini na matamshi ya kutovumiliana dhidi ya jamii za walio wachache.
Obama amesema kuwa anajua kwamba Waislamu Wamarekani wanalengwa na kulaumiwa kwa vitendo vya wachache.
''Wamarekani wengi hawawajui Waislamu'',alisema.Wengi huwasikia Waislamu na Uislamu kutoka kwa vyombo vya habari baada ya tendo la ugaidi ama katika chombo cha habari kinachoouangazia Uislamu,TV ama hata katika filamu.
Rais Obama amekuwa na uhusiano wa kutatiza na Waislamu.Mapema katika uongozi wake aliapa kuimarisha uhusiano na waislamu katika mataifa ya kigeni baada ya vita vya Iraq.

Wednesday, February 3, 2016

Wahamiaji wa Afrika wasiotakiwa na Israel

Kwa muda wa mwaka mmoja sasa Israel imekuwa ikiwapatia wahamiaji kutoka Afrika fedha ili kwenda kuishi vizuri katika taifa jengine.
Serikali ya Israel ina mktaba na matafa mawili ya Afrika ambayo yatawahifadhi wahamiaji hao wasiotakikana nchini humo.
Israel imekataa kuyataja mataifa hayo mawili ya Afrika,lakini BBC imezungumza na wahamiaji hao ambao wanasema walitumwa nchini Uganda na Rwanda.
Imeahidi kwamba wale watakaokubali mpango huo watapewa makaratasi wanapowasili ambayo yatawapa uraia katika taifa hilo.
Kama kiinua mgongo,wahamiaji hao hupewa dola 3,500 pesa taslimu ambazo hutolewa katika eneo la kusafiri katika uwanja wa ndege wa Tel Aviv.
Lakini BBC imezungumza na watu wawili ambao wanasema walitupiliwa mbali baada ya ndege yao kuondoka.
Mmoja wao aliuzwa huku aliyesalia akiamua kupigania maisha yake bila ya vibali.

Ushahidi dhidi ya Gbagbo waanza huko ICC

Shahidi wa kwanza katika kesi dhidi ya Rais wa zamani wa Ivory Coast, Laurent Gbagbo ametoa ushahidi wake mbele ya mahakama ya kimataifa ya jinai-ICC.
Bwana Gbagbo amekanusha tuhuma za kutekeleza uhalifu wa kivita na dhuluma dhidi ya binadamu. Uhalifu huo umedaiwa kutekelezwa wakati wa machafuko ya baada ya uchaguzi mkuu Ivory Coast mwaka wa 2010.
Shahidi huyo amesema kwamba alipigwa risasi kwa mguu na kisha akatandikwa na watu waliovalia sare za kijeshi wakati wa maandamano ya amani mji mkuu Abidjan.
Kuna taratibu zimewekwa kwa ajili ya usalama wa mashahidi japo shahidi wa leo alitaja jina lake bila kukusudia.

Milipuko ya guruneti yatokea Bujumbura

Watu kadhaa wameripotiwa kujeruhiwa vibaya katika mji mkuu wa Burundi, Bujumbura kufuatia milipuko 3 ya guruneti.
Duru zinasema kuwa takriban watu wanne wamejeruhiwa baada ya watu wasiojulikana kutupa gruneti nje ya jumba la posta mjini Bujumbura.
Mlipuko mwengine ulitokea nje ya afisi za kampuni inayotoa huduma za simu nchini humo Lumitel.
Mlipuko wa tatu ulisikika takriban nusu saa baadaye katika soko la zamani.
Hadi tulipochapisha taarifa hii hakuna maelezo kamili hayajatolewa kuhusu nani aliyetekeleza mashambulizi hayo na kwanini.
Machafuko nchini humo yalitibuka mwezi Aprili mwaka wa 2015 baada ya rais Pierre Nkurunziza kutangaza nia ya kuwania uchaguzi katika muhula wake wa tatu.
Wapinzani wake walisema Nkurunziza alikuwa anakiuka katiba ya taifa na kisha maandamano yakaanza kukotokea.
Kulitokea jaribio la mapinduzi ambayo ilizimwa na kisha rais huyo akaibuka mshindi katika uchaguzi ambao ulisusiwa na baadhi ya viongozi wa kisiasa wa upinzani.

Mwandishi wa BBC aliyeko huko Prime Ndikumagenge, anasema kuwa mashambulizi haya leo ni ya kipekee kwa sababu ni mara ya kwanza kuwahi kutokea mchana.
''kumekuwa na mashambulizi mengi nchini ,lakini hii ndio mara ya kwanza kwa mashambulizi ya aina hii kutokea mchana''.
Takriban watu 439 wameuawa huku wengine 240,000 wakitoroka nchini kuwa wakimbizi nje ya nchi kwa mujibu wa takwimu za Umoja wa Mataifa.
Mwezi uliopita shirika linalopigania haki za kibinadamu Amnesty International walisema kuwa picha za setlaiti zinaonesha uwezekano wa kuweko kwa makaburi 5 ya halaiki nje ya Bujumbura.
Maafisa wa usalama wanalaumiwa kwa kuua watu mwezi desemba mwaka uliopita.

Makasha 18 ya sukari yakamatwa Mombasa

Makasha 18 ya sukari yaliokamatwa katika bandari ya Mombasa yakielekea Uganda yamefunguliwa na sukari hiyo kumwagwa baharini.
Mamlaka ya ushuru nchini Kenya imesema kuwa bidhaa hiyo haikulipiwa na kwamba haikuwa bora kwa afya ya binaadamu.
Kulingana na na taarifa iliotiwa saini na kamishna wa mamlaka hiyo John Njiraini, Mamlaka hiyo pia imekamata makasha mengine 63 yaliojaa mapipa ya Ethanol.
Njiraini amesema kuwa vita dhidi ya biashara haramu vitaimarishwa kwa lengo la kuhakikisha kuwa wenye biashara hizo wanashtakiwa.
Mwandishi wetu alishuhudia mapipa hayo ya Ethanol iliokuwa ikitoa harufu mbaya yakimwagwa baharini.
Wafanyikazi wanasema kuwa wana mpango wa kupunguza ukali wa mafuta hayo ya Ethanol kabla ya kuyamwaga baharini.
Ethanol hutumiwa kutengeneza pombe.

Muslim Brotherhood waponea kunyongwa

 Mahakama ya rufaa nchini Misri imebatilisha hukumu ya kifo dhidi ya wanachama 140 wa vuguvugu la Muslim Brotherhood.
Wafuasi hao walihukumiwa kunyongwa kwa kukishambulia kituo cha polisi mjini Cairo mwaka 2013. Mahakama hiyo imetaka kesi dhidi ya watu hao kufunguliwa upya ambapo walipatiakana na hatia ya mauaji ya watu 13 wengi wao wakiwa ni maafisa wa polisi.
Shambulio hilo lilifanyika siku moja ambapo mamia ya watu waliuawa baada ya polisi kuvunja kambi za waandamanaji wa Muslim Brotherhood.
Walikua wakipinga mapinduzi ya kijeshi dhidi ya utawala wa Rais Mohammed Morsi aliyeonekana kuunga mkono sera za kiisilamu.

Wataka viongozi wa mapinduzi wafungwe maisha Burundi

Mawakili wa upande wa mashtaka nchini Burundi wamekata rufaa dhidi ya uamuzi uliopewa viongozi wa jaribio la mapinduzi,wakitaka wote wapewe hukumu ya maisha jela,kulingana na chombo cha habari cha AFP.
Pia walipata orodha ya viongozi 34 wa upinzani waliokwenda mafichoni,wanaharakati na waandishi ambao wanataka kuwashtaki kwa jukumu lao katika jaribio la mapinduzi hayo ya mwezi May 2015.
Rufaa hiyo inajiri baada ya mahakama mwezi uliopita kuwahukumu kifungo cha miaka 21 jela kwa jukumu lao la mapinduzi hayo yaliofeli,ikimuhukumu waziri wa ulinzi Cyrille Ndayirukiye na majenerali wengine watatu kifungo cha maisha ,wengine tisa kifungo cha miaka 30 pamoja na wanajeshi wanane waliopewa kifungo cha miaka 5.
Waendesha mashtaka wamesema katika taarifa kwamba hawakuridhika na hukumu hiyo na watu saba walioachiliwa na mahakama hiyo ni sharti washtakiwe upya kulingana na ripoti za AFP.

Matrilioni ya dola yaliyoporwa yafichuliwa Nigeria

Kwa miaka 12 iliyopita Nigeria imeweza kufichua zaidi ya dola trilioni 2 zilizokua zimeporwa kutoka hazina ya taifa , amesema waziri wa sheria wa nchi hiyo Abubakar Malami .
Magenge ya wahalifu na wakuu wa ofisi za umma waliiba pesa, aliongeza kusema.
Mwaka 1998 pekee, mtawala wa kijeshi Sani Abacha alipora zaidi ya dola milioni 2, Bwana Malami amenukuliwa na gazeti la Nigeria-Vanguard akielezea.
Rais Muhammadu Buhari ameapa “kurejesha mali ambazo wahalifu walizipora kwa kurejesha kila pesa ambayo ni mali ya umma nchini Nigeria ”, Aliongeza kusema waziri Malami .

Bei za mafuta hapa nchini kuanzia 3/2/2016

Petroli
DPetroli
Dizeli
Mafuta Ya Taa
Dar es Salaam
1,842
1,600
1,699
Arusha
1,926
1,684
1,783
Arumeru (Usa West)
1,926
1,684
1,783
Karatu
1,945
1,702
1,801
Monduli
1,932
1,689
1,788
Ngorongoro (Loliondo)
1,983
1,740
1,839


Kibaha
1,847
1,604
1,704
Bagamoyo
1,853
1,611
1,710
Kisarawe
1,850
1,607
1,706
Mkuranga
1,852
1,610
1,709
Rufiji
1,870
1,627
1,727
Dodoma
1,901
1,658
1,758
Bahi
1,908
1,666
1,765
Chemba
1,927
1,685
1,784
Kondoa
1,934
1,691
1,790
Kongwa
1,898
1,656
1,755
Mpwapwa
1,902
1,660
1,759
Iringa
1,906
1,664
1,763
Kilolo
1,911
1,668
1,767
Mufindi (Mafinga)
1,916
1,674
1,773
Njombe
1,934
1,692
1,791
Ludewa
1,972
1,730
1,829
Makete
1,965
1,723
1,822
Wanging'ombe (Igwachanya)
1,932
1,690
1,789
Bukoba
2,057
1,815
1,914
Biharamulo
2,032
1,789
1,888
Karagwe (Kayanga)
2,074
1,831
1,930
Kyerwa (Ruberwa)
2,079
1,837
1,936
Muleba
2,057
1,815
1,914
Ngara
2,023
1,780
1,879
Misenyi
2,066
1,823
1,922
Geita
2,007
1,765
1,864
Bukombe
1,996
1,754
1,853
Chato
2,028
1,786
1,885
Mbogwe
2,045
1,803
1,902
Nyang'hwale
2,022
1,780
1,879
Kigoma
2,073
1,831
1,930
Uvinza (Lugufu)
2,085
1,843
1,942
Buhigwe
2,062
1,820
1,919
Kakonko
2,030
1,788
1,887
Kasulu
2,059
1,817
1,916
Kibondo
2,038
1,795
1,894
Moshi
1,916
1,673
1,773
Hai (Bomang'ombe)
1,919
1,677
1,776
Mwanga
1,909
1,667
1,766
Rombo (Mkuu)
1,937
1,694
1,794
Same
1,902
1,660
1,759
Siha (Sanya Juu)
1,922
1,680
1,779
Lindi
1,901
1,659
1,758
Kilwa Masoko
1,876
1,634
1,733
Liwale
1,922
1,680
1,779
Nachingwea
1,930
1,688
1,787
Ruangwa
1,928
1,686
1,785
Babati
1,964
1,722
1,821
Hanang (Katesh)
1,975
1,732
1,832
Kiteto (Kibaya)
1,975
1,733
1,832
Mbulu
1,977
1,735
1,834
Simanjiro (Orkasumet)
1,996
1,754
1,853
Musoma
2,020
1,778
1,877
Rorya (Ingirijuu)
2,029
1,787
1,886
Bunda
2,012
1,769
1,868
Butiama
2,017
1,775
1,874
Serengeti (Mugumu)
2,066
1,824
1,923
Tarime
2,032
1,789
1,888
Mbeya
1,949
1,707
1,806
Chunya
1,959
1,716
1,815
Ileje
1,962
1,720
1,819
Kyela
1,965
1,722
1,822
Mbarali (Rujewa)
1,933
1,691
1,790
Mbozi (Vwawa)
1,958
1,716
1,815
Momba (Chitete)
1,967
1,725
1,824
Rungwe (Tukuyu)
1,958
1,716
1,815
Morogoro
1,867
1,625
1,724
Mikumi
1,883
1,640
1,740
Kilombero (Ifakara)
1,905
1,663
1,762
Ulanga (Mahenge)
1,916
1,673
1,772
Kilosa
1,886
1,643
1,742
Gairo
1,886
1,643
1,742
Mvomero (Wami Sokoine)
1,878
1,635
1,734
Turian
1,892
1,650
1,749
Mtwara
1,915
1,672
1,771
Nanyumbu (Mangaka)
1,963
1,721
1,820
Masasi
1,940
1,698
1,797
Newala
1,947
1,704
1,803
Tandahimba
1,940
1,697
1,796
Mwanza
1,992
1,750
1,849
Kwimba
2,028
1,786
1,885
Magu
2,000
1,758
1,857
Misungwi
1,998
1,755
1,854
Sengerema
2,024
1,782
1,881
Ukerewe
2,051
1,809
1,908
Sumbawanga
2,015
1,772
1,872
Kalambo (Matai)
2,007
1,765
1,864
Nkasi (Namanyele)
2,028
1,786
1,885
Katavi (Mpanda)
2,050
1,807
1,906
Mlele (Inyonga)
2,028
1,786
1,885
Songea
1,965
1,723
1,822
Mbinga
1,999
1,756
1,856
Namtumbo
1,995
1,752
1,851
Nyasa (Mbamba Bay)
2,001
1,759
1,858
Tunduru
2,024
1,782
1,881
Shinyanga
1,971
1,728
1,828
Kahama
1,985
1,742
1,841
Kishapu
1,999
1,757
1,856
Simiyu (Bariadi)
2,012
1,770
1,869
Busega (Nyashimo)
2,005
1,763
1,862
Itilima (Lagangabilili)
2,015
1,773
1,872
Maswa
2,004
1,761
1,860
Meatu (Mwanhuzi)
2,011
1,768
1,867
Singida
1,933
1,690
1,790
Iramba
1,945
1,702
1,802
Manyoni
1,917
1,675
1,774
Ikungi
1,928
1,686
1,785
Mkalama (Nduguti)
1,957
1,715
1,814
Tabora
1,996
1,754
1,853
Igunga
1,950
1,708
1,807
Kaliua
2,014
1,772
1,871
Ulyankulu
2,008
1,766
1,865
Nzega
1,961
1,718
1,817
Sikonge
2,008
1,765
1,865
Urambo
2,009
1,767
1,866
Tanga
1,825
1,586
1,745
Handeni
1,846
1,607
1,725
Kilindi
1,861
1,622
1,759
Korogwe
1,838
1,598
1,738
Lushoto
1,847
1,608
1,748
Mkinga (Maramba)
1,832
1,593
1,759
Muheza
1,830
1,591
1,745
Pangani
1,832
1,593
1,752


B: BEI ZA JUMLA


Bei za Jumla - DSM
Petroli (Sh/L)
Dizeli  (Sh/L)
Mafuta ya Taa (Sh/L)
Bei Kikomo
1,737.38
1,494.85
1,594.04

Bei za Jumla - TANGA
Petroli (Sh/L)
Dizeli  (Sh/L)
Bei Kikomo
1,720.47
1,481.29


Felix Ngamlagosi
MKURUGENZI MKUU
EWURA

Breaking News..Kabwe Zitto Kununua Timu Kubwa ya Mpira Nchini.

MBUNGE wa Kigoma Mjini, Kabwe Zitto (ACT), ametangaza azma ya kuinunua timu ya soka ya JKT Kanembwa inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara.

Akizungumza , mbunge huyo alisema kuwa tayari ameshaanza mazungumzo na uongozi wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) mkoani Kigoma kuona kama upo uwezekano wa kuinunua timu hiyo.

Alisema kuwa mpango wa kuinunua timu hiyo unakuja katika kutekeleza azma ya kuwa na timu ambayo itacheza Ligi Kuu Tanzania Bara na kurudisha hadhi ya michezo ya mkoa Kigoma kwenye soka.zitto-kabwe-facebook-frontKabwe alisema kuwa iwapo uwezekano wa kuinunua timu hiyo utafanikiwa mpango utafanywa kuunda kampuni ambayo itakuwa ikisimamia uendeshaji wa timu hiyo kama ilivyo kwa timu ya Azam.

Alisema ni jambo la aibu kuona mkoa wa Kigoma hauna timu hata moja katika Ligi Kuu wakati sehemu kubwa ya wachezaji wanaochezea timu zinazoshiriki ligi hiyo wanatoka Kigoma.

Pamoja na azma hiyo alisema kuwa kama itashindikana kwa timu hiyo kununuliwa kutokana na taratibu za jeshi atatafuta timu nyingine ambayo ataisimamia na kuiwezesha kufanya vizuri ili iweze kucheza Ligi Kuu.

Katika kauli yake Kabwe ametanabaisha kuwa pamoja na mpango wa kuwa na timu ya mpira wa miguu, mpango wake ni kuhakikisha wachezaji wakongwe waliowahi kuchezea timu za madaraja ya juu na timu ya Taifa wakiwemo Juma Kaseja na wengine wanarudi mkoani humo ili kusimamia timu za mkoa huo na kuzifanya ziweze kucheza mashindano ya ligi mbalimbali nchini kwa mafanikio.

Kauli hiyo ya Zitto inakuja siku moja baada ya kuutangazia umma mazungumzo ya awali kati yake na Mkurugenzi wa timu ya Azam FC, Abubakar Bakhresa kuhusu kuanzisha shule ya kuendeleza vipaji Kigoma.


Dr. Slaa Ajibu Mapigo....Akanusha Nyumba Yake Kupigwa Mnada Kisa Mkopo Aliochukua Mkewe Na Kumpa Mwanaume Mwingine

Katibu Mkuu wa Zamani wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbroad Slaa ametoa majibu kuhusu taarifa zinazoandikwa kwenye baadhi ya magazeti nchini pamoja na mitandao kuwa nyumba yake iliyoko Mbezi jijini Dar es Salaam inauzwa baada ya kushindwa kulipa mkopo wa Benki ikidaiwa kuwa mkewe aliuchukua na kumpa mwanaume mwingine.

Taarifa hizo zilieleza kuwa Mke wa Dk. Slaa, Josephine alichukua mkopo wa shilingi milioni 300 katika moja kati mabenki nchini na kushindwa kuirudisha fedha hiyo.

Dk. Slaa ambaye yuko nchini Canada akijiendeleza kimasomo, amekanusha taarifa hizo na kueleleza kuwa yeye na mkewe Josephine hawajawahi kuchukua mkopo katika benki yoyote nchini.

“Nataka nikuambie na uwajulishe Watanzania kwamba wala si mimi Dk. Slaa wala mke wangu, Josephine kwa wakati wowote ule hatujawahi kuchukua mkopo benki,”Dk. Slaa aliliambia gazeti la Mtanzania kwa njia ya simu.

“Tangu nitoke Bungeni sijawahi kuchukua hata senti moja benki, achilia mbali propaganda ya shilingi milioni 300.
" Hivyo, ni vizuri waliokupa taarifa wakupe undani ni benki ipi nilikopa au Josephine alikopa na ni shilingi ngapi na kwa nyaraka zipi. 
"Na ni vema ukafuatilia benki husika pia kama walikuwambia ni benki gani,”Mwanasiasa huyo mkongwe alieleza.

Dk. Slaa ambaye alitangaza mwaka jana kustaafu siasa, alisema kuwa anapanga kuchukua hatua za kisheria dhidi ya wote walioandika habari hizo.

Zuma kulipa fedha za ukarabati wa nyumba yake

Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amekubali kulipa kiasi cha dola milioni 23 ambazo serikali ilitumia kurekebisha nyumba yake iliopo mashambani.
Katika ripoti ya 2014,ripoti yake mlinzi wa umma imesema bw.Zuma alifaidi kinyume na sheria.
Bw.Zuma amesema kuwa mkaguzi mkuu na waziri wa fedha wanafaa kubaini ni kiasi gani anapaswa kulipa ili kumaliza mgogoro huo.
Tangazo hilo linajiri wiki moja kabla ya kusikilizwa kwa swala hilo.
Urekebishaji wa makao hayo katika kijiji cha Nklanda nyumbani kwa zuma katika mkoa wa kwa Zulu Natal umezua mgogoro mkubwa wa kisiasa nchini Afrika Kusini.
Baadhi ya fedha zilitumiwa kujenga ukumbi wa maonyesho,kidimbwi cha maji na zizi la ng'ombe.

US: Wagombea sasa waelekea New Hampshire

 
Wanachama wa Republican na Democrats nchini Marekani wanaopigania tiketi za vyama vyao tayari kwa uchaguzi wa urais nchini Marekani wameanza kuwasili katika jimbo la New Hampshire ambapo uchaguzi mwengine utafanyika.
Walioshinda katika kamati za wabunge za Iowa walikuwa Sineta Ted Cruz wa chama cha Republican na Hillary Clinton wa Democrats.
Bw.Cruz alishinda licha ya kuwa nyuma katika kura ya maoani huku Bi.Clinton akimshinda sineta Bernie Sanders kwa asilimia 0.2.
Jimbo la New Hampshire linaonekana kuwa na changamoto tofauti kwa vyama hivyo.Jimbo hilo lenye watu wa msimamo wa kadri na wasio na wasiofuata dini huenda likawa changamoto kubwa kwa bwana Cruz wakati mchujo huo utakapofanyika mnamo tarehe 9 mwezi Februari.
Donald Trump,ambaye amekuwa kifua mbele kwa upande wa chama cha Republican anatarajiwa kufanya vyema zaidi ya Iowa ambayo mchujo wa kwanza ulifanyika.
Upande wa Democrats,Bw.Sanders anaonekana kuwa na fursa ya kuwa nyumbani dhidi ya Bi Clinton,akiwa sineta wa jimbo jirani la Vermont.

Hata kabla ya ushindi mdogo wa Bi.Clinton kutangazwa rasmi,Bw.Sanders alikuwa amepanda katika lori moja akisalimiana na mashabiki katika mji wa Bow jimbo la New Hampshire.
Akiuambia umati huo kwamba kampeni yake imeushangaza ulimwengu huko Iowa,ameahidi kwamba itaushangaza tena ulimwengu katika Jimbo la New Hampshire.
Katika jimbo hilo,Bi Clinton alitangaza ushindi akisema kuwa anaamini kwamba anaelekea kupata ushindi mwengine katika jimbo la New Hampshire baada ya kuibuka mshindi Iowa.
''Nimeshinda na kupoteza huko, na ni vizuri kushinda'',alisema akiangazia alipopoteza katika jimbo hilo mwaka 2008.

Tuesday, February 2, 2016

Kisa nadra cha Zika charipotiwa Marekani

Kisa nadra sana cha virusi vya Zika kuambukizwa kupitia kushiriki ngono, badala ya kuumwa na mbu, kimeripotiwa nchini Marekani.
Mgonjwa aliyeambukizwa virusi hivyo Dallas, Texas, sana huenda aliambukizwa kupitia kufanya mapenzi, Kituo cha Udhibiti wa Maradhi (CDC) kimeambia BBC.
Mtu huyo hakuwa amesafiri maeneo ambayo yana virusi hivyo lakini mpenzi wake alirejea majuzi kutoka Venezuela.
Virusi vya Zika vinaenezwa sana na mbu na vimehusishwa na visa vya watoto kuzaliwa wakiwa na vichwa vidogo na ubongo kudumaa.
Vinaenea kwa kazi Amerika na Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza hali ya tahadhari duniani.
Shirika la msalaba mwekundu nchini Marekani limewahimisha watu waliotoka maeneo yaliyoathirika na Zika, na ambao wanataka kutoa damu, wasubiri angalau siku 28, kabla ya kutoa damu.
Ushauri huu umeelekezwa kwa watu waliorejea Marekani kutoka Mexico, visiwa vya Caribbean au Amerika ya Kati na Kusini katika kipindi cha wiki nne zilizopita, shirika hilo limesema kupitia taarifa.
Katika tukio jingine, visa viwili vya maambukizi ya Zika vimethibitishwa Australia.

Basi linalotumia umeme wa jua lazinduliwa Uganda

Basi linalotumia umeme wa nguvu za jua ambalo limedaiwa na watengezaji wake nchini Uganda kuwa la kwanza barani Afrika limeendeshwa hadharani.
Basi hilo la kielektroniki aina ya Kayoola linalomilikiwa na kampuni ya Kiira Motors lilionyeshwa katika uwanja wa Uganda mjini Kampala.
Mojawapo ya betri zake zinaweza kuwekwa chaji na vibamba vya umeme wa jua katika paa la nyumba ambavyo huongeza kasi ya gari hilo hadi kilomita 80 kwa saa.
Watengezaji wake sasa wanalenga kuwavutia wateja wataolitengeza basi hilo ili kuvutia soko kubwa la magari duniani.
Mkurugenzi mkuu wa Kiira Motors Paul Isaac Musasizi ameiambia BBC kwamba amefurahishwa na jaribio la gari hilo lilipoendeshwa.
Raia wamefurahishwa na wazo kwamba Uganda ina uwezo wa kutengeza mfano kama huu na bw. Musasizi anasema kwamba angependelea kulisaidia taifa hilo kushindana na kampuni nyengine za magari katika eneo hili.
Pia anatumai kwamba hatua hiyo itabuni ajira zifikiazo 7000 kufikia mwaka 2018.Hatahivyo mradi huo hauwezi kuanza bila ya usaidizi wa kampuni zinazotengeza vifaa vya magari.

Lengo ni kwamba kufikia 2039,kampuni hiyo itakuwa na uwezo wa kutengeza vifaa vya magari na kuviunganisha nchini Uganda bila kutegemea kampuni nyengine .
Basi hilo lenye viti 35 linalenga kufanya kazi katika miji midogo badala ya mji mkuu kutokana na masharti ya umbali linakoweza kusafiri.
Iwapo mabasi hayo yatazalishwa kwa wingi,kila basi litagharimu kiasi cha dola 58,000 ambacho bw,Musaizi anasema ni bei nzuri katika soko lenye ushindani mkubwa.
Kampuni ya Kiira Motors ilianzishwa kutokana na mradi uliofanyika katika chuo kikuu cha Makerere,ambacho ni mmoja wa mmiliki wa hisa katika kampuni hiyo na pia kimenufaika na ufadhili kutoka kwa hazina ya fedha ya serikali.

Mfalme Abdullah wa Jordan anasema kuwa nchi yake iko kwenye hatari kubwa kufuatia wimbi la maelfu ya wakimbizi kutoka nchini Syria.
Kabla ya kufanyika kwa mkutano kuhusu utoaji misaada nchini Syria, mfalme Abdullah aliiambia BBC kuwa kuna shinikizo kubwa katika utoaji wa huduma za kijamii nchii Jordan, za miundo msingi na kwa uchumi.
Amesema kuwa jamii ya kimataifa inahitaji kutoa usaidizi zaidi ikiwa itahitaji Jordan iendelee kuwachukua wakimbizi zaidi.
Umoja wa Mataifa unatafuta dola billioni 7.7 kufadhili oparesheni za kutoa misaada kwa watu milioni 22.5 nchini Syria na nchi majirani mwaka ujao.
Jordan inawahifadfhi watu 635,000 kati ya watu millioni 4.6 ambao ni wakimbzi raia wa Syria waliosajiliwa na Umoja wa Mataifa. Serikali inasema kuwa zaid ya watu milioni moja raia wa Syria wanaoishi nchini humo wakiwemo wale waliowasilii kabla ya mzozo kuanza mwaka 2011.

Lubuva: Magufuli hafai kuingilia kati Zanzibar

Mwenyekiti wa tume ya taifa ya uchaguzi Tanzania Jaji Damian Lubuva amesema Rais John Magufuli hafai kuingilia kwenye mzozo wa uchaguzi unaoendelea visiwani Zanzibar.
Akizungumza alipokutana na Dkt Magufuli katika ikulu, Dar es Salaam Jumatatu, Jaji Lubuva amesema tume za uchaguzi zinafaa kuwa huru na hazifai kuingiliwa kimaamuzi na Rais wala kiongozi yeyote.
Amesema wanaosema Rais anapaswa kuingilia kati masuala ya uchaguzi iwe Tanzania bara ama Zanzibar wanafanya makosa, kwani Rais hana mamlaka hayo.
“Unaposikia kwamba Rais wa Jamhuri ya Muungano aingilie hilo suala la uchaguzi wa Zanzibar, yeye kwa kweli hana mamlaka kabisa. Pili ni kama kujikanganya, huku unasema tuwe na tume huru isiyoingiliwa halafu huku unasema aingilie kati maamuzi ya tume,” amesema Jaji Lubuva, kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa kutoka ikulu na kaimu mkurugenzi ya mawasiliano ya ikulu, Bw Gerson Msigwa.
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar Jecha Salim Jecha alitangaza kufutwa kwa matokeo ya uchaguzi uliofanyika visiwani humo tarehe 25 Oktoba mwaka uliopita akisema kulikuwa na kasoro nyingi.
Wiki iliyopita, Bw Jecha, kupitia tararifa, alitangaza kwamba uchaguzi utarudiwa Machi 20.
Chama cha Wananchi (CUF), ambacho kimekuwa kikisisitiza kwamba mshindi wa uchaguzi wa mwaka jana anafaa kutangazwa, kimesema hakitashiriki marudio hayo ya uchaguzi.

Meli iliyokuwa hatarini yarejeshwa baharini

Meli iliyokuwa ikielekea kwenye ufuo wa Ufaransa ikiwa imeinama imerejeshwa ndani ya bahari, maafisa wa baharini wanasema.
Meli ya kuvuta meli nyingine kutoka Uhispania imefanikiwa kuivuta meli hiyo na kuiingiza ndani ya baharini, msemaji wa chama cha mabaharia Ufaransa Louis-Xavier Renaux amesema.
Meli hizo mbili sasa zinaelekea magharibi ndani ya bahari ya Atlantic kwa kasi ya kilomita tano kwa saa, ameongeza.
Mabaharia 22 waliokuwa kwenye meli hiyo kwa jina Modern Express ambayo imesajiliwa Panama, waliondolewa salama kwa kutumia ndege kutoka kwenye meli hiyo Jumanne wiki iliyopita.
Maafisa walikuwa wamehofia kwamba meli hiyo, iliyokuwa kilomita 44 pekee kutoka ufuo wa Ufaransa eneo la Arcachon karibu na Bordeaux, ksuini magharibi mwa Ufaransa ingezama.
Lakini wataalamu wane walifanikiwa kushikisha mnyororo wa kuvuta meli hiyo na kuwezesha kuvutwa kwake.
Iwapo operesheni hiyo ingefeli, meli hiyo ingegonga ufuo wa kusini magharibi mwa Ufaransa kati ya Jumatatu usiku na Jumanne asubuhi.

Hali mbaya ya hewa ilitatiza juhudi za uokoaji Jumapili, siku mbili baada ya mnyororo mwingine wa kuivuta meli hiyo kukatika.

Meli hiyo ilikuwa imebeba tani 3,600 za mbao na mashine za kuchimba ardhini.
Ilikuwa imeinama kwa pembe ya nyuzi 40 hadi 50.

Maafisa wa baharini wamesema haiwezekani kuisimamisha.
AP
Meli hiyo ina mafuta tani 300 na kwa mujibu wa gazeti la Sud-Ouest, mipango ya dharura ilikuwa imeandaliwa kuhifadhi na kuyatoa mafuta hayo iwapo ingezama