MICHAKATO

Levis Rocky Ndekeno

This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Pages

Sunday, February 2, 2014

WAUMINI wa Kanisa la Break Through Assemblies lililoko eneo la Boko Magengeni nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam linadaiwa kuuza Sakramenti kwa Sh 100,000 kwa kila muumini. Hatua hiyo inadaiwa kuwanyima wasio na fedha chakula hicho cha Bwana hivyo kusababisha malalamiko dhidi ya uongozi wa Kanisa hilo la Walokole.

Habari za uhakika zilizolifikia gazeti hili, zilisema tukio hilo lililoshangaza waumini lilitokea Januari 19. Kanisa hilo linaongozwa na Mchungaji Godfrey Simtomvu.

Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti, na kwa masharti ya kutotajwa majina, waumini walisema kitendo hicho kiliwashangaza siku hiyo kanisani hapo walikokuwa wamekwenda kwa ajili ya Ibada kama siku zingine.

Akisimulia, mmoja wao alisema baada ya Mchungaji kuhubiri, vililetwa vikombe na mikate ambayo hutumiwa kanisani kama ishara ya kushiriki pamoja Chakula cha Bwana. Makanisa mengine hutambua ibada hiyo kama ya Sakramenti ya Chakula cha Bwana.

“Baada ya vifaa hivyo kufika kanisani hapo vilionekana kuwa vichache tofauti na waumini waliokuwa kanisani hapo…ndipo Mchungaji alipopaza sauti kuwa mwenye Sh 100,000 na zaidi ndiye atakayeshiriki,” alisema na kuongeza kuwa Januari 26, alishindwa kuabudu kutokana na kitendo hicho.

Alisema baada ya kutamka hivyo, waumini wengi walinywea wakashindwa kusogea na kupisha watu wapatao 10; lakini baada ya kuona idadi imekuwa ndogo zaidi ikatangazwa kuwa hata wenye Sh 50,000 wanaweza kusogea mbele kushiriki.

Aliongeza kuwa wakati wote huo waumini walikuwa wakitazamana, wakijiuliza juu ya utaratibu huo mpya, jambo ambalo ni kinyume na ilivyokuwa awali kanisani.

Alisema Mchungaji baada ya kuona idadi ya waumini inazidi kupungua, akawatangazia kuwa wasiokuwa na fedha wajiandikishe kisha wapokee chakula hicho kisha na kesho yake wapeleke kiwango hicho cha fedha. Muumini mwingine alisema jambo lililoshangaza wengi ni utaratibu huo mpya ambao awali haukuwapo kwani walikuwa wakitangaziwa wiki moja kabla na kutakiwa kujitayarisha kwa ajili ya ibada hiyo ya Chakula cha Bwana.

“Awali Mchungaji alikuwa akitupa taarifa wiki moja kabla, akiwataka waumini kujitayarisha na kusafisha nyoyo zao kabla ya kushiriki kitendo hicho ambacho tuliamini kuwa ni kitakatifu na chenye mafundisho makubwa kwa waumini,” alisema na kuongeza kuwa hilo la kununua chakula lilizuka ghafla na hakujua hatma yake.

Mwingine alisema mbali na kununua chakula hicho, pia jambo lililozusha mshangao kwa waumini ni Mchungaji huyo kuleta watu kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kuhubiri Neno la Mungu akidai kuwa ni wahubiri ambao nao husisitiza neno la kutoa tu.

“Waumini tunaamini kuwa Bwana Yesu alitoa chakula hicho bure…iweje leo waumini wauziwe tena kwa kupangiwa kiwango?” Alihoji.

Akizungumzia madai hayo, Mzee wa Kanisa hilo alisisitiza kuwa yeye si msemaji wa Kanisa hilo na kusema madai hayo hayana ukweli na kwamba siku hiyo, Mchungaji hakumaanisha kwamba utakuwa utaratibu, bali ilikuwa ni kuhamasisha utoaji kwa muumini mwenye nacho. Alisema kufanya hivyo halikuwa lengo la kutafuta fedha bali kupeleka Neno la Mungu mbele.

“Msemaji wa Kanisa ni Mchungaji mwenyewe, ukiniuliza sana mimi utakuwa unanionea, kama unamtafuta na ukamkosa atakuwa redioni katika kipindi,” alisema mzee huyo.

Akizungumzia malalamiko hayo, Mchungaji Simtomvu alisema kutokea kwa hali hiyo si imani ya Kanisa hilo bali ilitokana na mhubiri kutoka Kongo ambaye alifunuliwa na Mungu na kutaka waumini kuweka maagano yao na Mungu kwa mwaka huu.

Alisema hayo yalikuwa mafunuo ya mtu na si imani na ni kitu ambacho hutokea mara moja tu na kutolea mfano wa yai linapouzwa kwenye mnada kwa bei kubwa, ingawa bei yake halisi inajulikana.

“Laiti ningemfahamu aliyeleta taarifa hiyo ningemsaidia, kwani amekengeuka, mbona Mchungaji TB Joshua wa Nigeria huuza maji katika vichupa vidogo kwa gharama kubwa inayoweza kufikia Sh 75,000,” alisema Mchungaji Simtomvu.


Alisema tukio hilo ilikuwa ni kwa muumini anayetaka kuweka agano na Mungu wake, kwamba mwaka huu amtendee mambo gani na kuhoji kuwa zipo imani za ajabu ajabu lakini haziripotiwi.