MICHAKATO

Levis Rocky Ndekeno

This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Pages

Wednesday, February 3, 2016

Wahamiaji wa Afrika wasiotakiwa na Israel

Kwa muda wa mwaka mmoja sasa Israel imekuwa ikiwapatia wahamiaji kutoka Afrika fedha ili kwenda kuishi vizuri katika taifa jengine.
Serikali ya Israel ina mktaba na matafa mawili ya Afrika ambayo yatawahifadhi wahamiaji hao wasiotakikana nchini humo.
Israel imekataa kuyataja mataifa hayo mawili ya Afrika,lakini BBC imezungumza na wahamiaji hao ambao wanasema walitumwa nchini Uganda na Rwanda.
Imeahidi kwamba wale watakaokubali mpango huo watapewa makaratasi wanapowasili ambayo yatawapa uraia katika taifa hilo.
Kama kiinua mgongo,wahamiaji hao hupewa dola 3,500 pesa taslimu ambazo hutolewa katika eneo la kusafiri katika uwanja wa ndege wa Tel Aviv.
Lakini BBC imezungumza na watu wawili ambao wanasema walitupiliwa mbali baada ya ndege yao kuondoka.
Mmoja wao aliuzwa huku aliyesalia akiamua kupigania maisha yake bila ya vibali.

Ushahidi dhidi ya Gbagbo waanza huko ICC

Shahidi wa kwanza katika kesi dhidi ya Rais wa zamani wa Ivory Coast, Laurent Gbagbo ametoa ushahidi wake mbele ya mahakama ya kimataifa ya jinai-ICC.
Bwana Gbagbo amekanusha tuhuma za kutekeleza uhalifu wa kivita na dhuluma dhidi ya binadamu. Uhalifu huo umedaiwa kutekelezwa wakati wa machafuko ya baada ya uchaguzi mkuu Ivory Coast mwaka wa 2010.
Shahidi huyo amesema kwamba alipigwa risasi kwa mguu na kisha akatandikwa na watu waliovalia sare za kijeshi wakati wa maandamano ya amani mji mkuu Abidjan.
Kuna taratibu zimewekwa kwa ajili ya usalama wa mashahidi japo shahidi wa leo alitaja jina lake bila kukusudia.

Milipuko ya guruneti yatokea Bujumbura

Watu kadhaa wameripotiwa kujeruhiwa vibaya katika mji mkuu wa Burundi, Bujumbura kufuatia milipuko 3 ya guruneti.
Duru zinasema kuwa takriban watu wanne wamejeruhiwa baada ya watu wasiojulikana kutupa gruneti nje ya jumba la posta mjini Bujumbura.
Mlipuko mwengine ulitokea nje ya afisi za kampuni inayotoa huduma za simu nchini humo Lumitel.
Mlipuko wa tatu ulisikika takriban nusu saa baadaye katika soko la zamani.
Hadi tulipochapisha taarifa hii hakuna maelezo kamili hayajatolewa kuhusu nani aliyetekeleza mashambulizi hayo na kwanini.
Machafuko nchini humo yalitibuka mwezi Aprili mwaka wa 2015 baada ya rais Pierre Nkurunziza kutangaza nia ya kuwania uchaguzi katika muhula wake wa tatu.
Wapinzani wake walisema Nkurunziza alikuwa anakiuka katiba ya taifa na kisha maandamano yakaanza kukotokea.
Kulitokea jaribio la mapinduzi ambayo ilizimwa na kisha rais huyo akaibuka mshindi katika uchaguzi ambao ulisusiwa na baadhi ya viongozi wa kisiasa wa upinzani.

Mwandishi wa BBC aliyeko huko Prime Ndikumagenge, anasema kuwa mashambulizi haya leo ni ya kipekee kwa sababu ni mara ya kwanza kuwahi kutokea mchana.
''kumekuwa na mashambulizi mengi nchini ,lakini hii ndio mara ya kwanza kwa mashambulizi ya aina hii kutokea mchana''.
Takriban watu 439 wameuawa huku wengine 240,000 wakitoroka nchini kuwa wakimbizi nje ya nchi kwa mujibu wa takwimu za Umoja wa Mataifa.
Mwezi uliopita shirika linalopigania haki za kibinadamu Amnesty International walisema kuwa picha za setlaiti zinaonesha uwezekano wa kuweko kwa makaburi 5 ya halaiki nje ya Bujumbura.
Maafisa wa usalama wanalaumiwa kwa kuua watu mwezi desemba mwaka uliopita.

Makasha 18 ya sukari yakamatwa Mombasa

Makasha 18 ya sukari yaliokamatwa katika bandari ya Mombasa yakielekea Uganda yamefunguliwa na sukari hiyo kumwagwa baharini.
Mamlaka ya ushuru nchini Kenya imesema kuwa bidhaa hiyo haikulipiwa na kwamba haikuwa bora kwa afya ya binaadamu.
Kulingana na na taarifa iliotiwa saini na kamishna wa mamlaka hiyo John Njiraini, Mamlaka hiyo pia imekamata makasha mengine 63 yaliojaa mapipa ya Ethanol.
Njiraini amesema kuwa vita dhidi ya biashara haramu vitaimarishwa kwa lengo la kuhakikisha kuwa wenye biashara hizo wanashtakiwa.
Mwandishi wetu alishuhudia mapipa hayo ya Ethanol iliokuwa ikitoa harufu mbaya yakimwagwa baharini.
Wafanyikazi wanasema kuwa wana mpango wa kupunguza ukali wa mafuta hayo ya Ethanol kabla ya kuyamwaga baharini.
Ethanol hutumiwa kutengeneza pombe.

Muslim Brotherhood waponea kunyongwa

 Mahakama ya rufaa nchini Misri imebatilisha hukumu ya kifo dhidi ya wanachama 140 wa vuguvugu la Muslim Brotherhood.
Wafuasi hao walihukumiwa kunyongwa kwa kukishambulia kituo cha polisi mjini Cairo mwaka 2013. Mahakama hiyo imetaka kesi dhidi ya watu hao kufunguliwa upya ambapo walipatiakana na hatia ya mauaji ya watu 13 wengi wao wakiwa ni maafisa wa polisi.
Shambulio hilo lilifanyika siku moja ambapo mamia ya watu waliuawa baada ya polisi kuvunja kambi za waandamanaji wa Muslim Brotherhood.
Walikua wakipinga mapinduzi ya kijeshi dhidi ya utawala wa Rais Mohammed Morsi aliyeonekana kuunga mkono sera za kiisilamu.

Wataka viongozi wa mapinduzi wafungwe maisha Burundi

Mawakili wa upande wa mashtaka nchini Burundi wamekata rufaa dhidi ya uamuzi uliopewa viongozi wa jaribio la mapinduzi,wakitaka wote wapewe hukumu ya maisha jela,kulingana na chombo cha habari cha AFP.
Pia walipata orodha ya viongozi 34 wa upinzani waliokwenda mafichoni,wanaharakati na waandishi ambao wanataka kuwashtaki kwa jukumu lao katika jaribio la mapinduzi hayo ya mwezi May 2015.
Rufaa hiyo inajiri baada ya mahakama mwezi uliopita kuwahukumu kifungo cha miaka 21 jela kwa jukumu lao la mapinduzi hayo yaliofeli,ikimuhukumu waziri wa ulinzi Cyrille Ndayirukiye na majenerali wengine watatu kifungo cha maisha ,wengine tisa kifungo cha miaka 30 pamoja na wanajeshi wanane waliopewa kifungo cha miaka 5.
Waendesha mashtaka wamesema katika taarifa kwamba hawakuridhika na hukumu hiyo na watu saba walioachiliwa na mahakama hiyo ni sharti washtakiwe upya kulingana na ripoti za AFP.

Matrilioni ya dola yaliyoporwa yafichuliwa Nigeria

Kwa miaka 12 iliyopita Nigeria imeweza kufichua zaidi ya dola trilioni 2 zilizokua zimeporwa kutoka hazina ya taifa , amesema waziri wa sheria wa nchi hiyo Abubakar Malami .
Magenge ya wahalifu na wakuu wa ofisi za umma waliiba pesa, aliongeza kusema.
Mwaka 1998 pekee, mtawala wa kijeshi Sani Abacha alipora zaidi ya dola milioni 2, Bwana Malami amenukuliwa na gazeti la Nigeria-Vanguard akielezea.
Rais Muhammadu Buhari ameapa “kurejesha mali ambazo wahalifu walizipora kwa kurejesha kila pesa ambayo ni mali ya umma nchini Nigeria ”, Aliongeza kusema waziri Malami .

Bei za mafuta hapa nchini kuanzia 3/2/2016

Petroli
DPetroli
Dizeli
Mafuta Ya Taa
Dar es Salaam
1,842
1,600
1,699
Arusha
1,926
1,684
1,783
Arumeru (Usa West)
1,926
1,684
1,783
Karatu
1,945
1,702
1,801
Monduli
1,932
1,689
1,788
Ngorongoro (Loliondo)
1,983
1,740
1,839


Kibaha
1,847
1,604
1,704
Bagamoyo
1,853
1,611
1,710
Kisarawe
1,850
1,607
1,706
Mkuranga
1,852
1,610
1,709
Rufiji
1,870
1,627
1,727
Dodoma
1,901
1,658
1,758
Bahi
1,908
1,666
1,765
Chemba
1,927
1,685
1,784
Kondoa
1,934
1,691
1,790
Kongwa
1,898
1,656
1,755
Mpwapwa
1,902
1,660
1,759
Iringa
1,906
1,664
1,763
Kilolo
1,911
1,668
1,767
Mufindi (Mafinga)
1,916
1,674
1,773
Njombe
1,934
1,692
1,791
Ludewa
1,972
1,730
1,829
Makete
1,965
1,723
1,822
Wanging'ombe (Igwachanya)
1,932
1,690
1,789
Bukoba
2,057
1,815
1,914
Biharamulo
2,032
1,789
1,888
Karagwe (Kayanga)
2,074
1,831
1,930
Kyerwa (Ruberwa)
2,079
1,837
1,936
Muleba
2,057
1,815
1,914
Ngara
2,023
1,780
1,879
Misenyi
2,066
1,823
1,922
Geita
2,007
1,765
1,864
Bukombe
1,996
1,754
1,853
Chato
2,028
1,786
1,885
Mbogwe
2,045
1,803
1,902
Nyang'hwale
2,022
1,780
1,879
Kigoma
2,073
1,831
1,930
Uvinza (Lugufu)
2,085
1,843
1,942
Buhigwe
2,062
1,820
1,919
Kakonko
2,030
1,788
1,887
Kasulu
2,059
1,817
1,916
Kibondo
2,038
1,795
1,894
Moshi
1,916
1,673
1,773
Hai (Bomang'ombe)
1,919
1,677
1,776
Mwanga
1,909
1,667
1,766
Rombo (Mkuu)
1,937
1,694
1,794
Same
1,902
1,660
1,759
Siha (Sanya Juu)
1,922
1,680
1,779
Lindi
1,901
1,659
1,758
Kilwa Masoko
1,876
1,634
1,733
Liwale
1,922
1,680
1,779
Nachingwea
1,930
1,688
1,787
Ruangwa
1,928
1,686
1,785
Babati
1,964
1,722
1,821
Hanang (Katesh)
1,975
1,732
1,832
Kiteto (Kibaya)
1,975
1,733
1,832
Mbulu
1,977
1,735
1,834
Simanjiro (Orkasumet)
1,996
1,754
1,853
Musoma
2,020
1,778
1,877
Rorya (Ingirijuu)
2,029
1,787
1,886
Bunda
2,012
1,769
1,868
Butiama
2,017
1,775
1,874
Serengeti (Mugumu)
2,066
1,824
1,923
Tarime
2,032
1,789
1,888
Mbeya
1,949
1,707
1,806
Chunya
1,959
1,716
1,815
Ileje
1,962
1,720
1,819
Kyela
1,965
1,722
1,822
Mbarali (Rujewa)
1,933
1,691
1,790
Mbozi (Vwawa)
1,958
1,716
1,815
Momba (Chitete)
1,967
1,725
1,824
Rungwe (Tukuyu)
1,958
1,716
1,815
Morogoro
1,867
1,625
1,724
Mikumi
1,883
1,640
1,740
Kilombero (Ifakara)
1,905
1,663
1,762
Ulanga (Mahenge)
1,916
1,673
1,772
Kilosa
1,886
1,643
1,742
Gairo
1,886
1,643
1,742
Mvomero (Wami Sokoine)
1,878
1,635
1,734
Turian
1,892
1,650
1,749
Mtwara
1,915
1,672
1,771
Nanyumbu (Mangaka)
1,963
1,721
1,820
Masasi
1,940
1,698
1,797
Newala
1,947
1,704
1,803
Tandahimba
1,940
1,697
1,796
Mwanza
1,992
1,750
1,849
Kwimba
2,028
1,786
1,885
Magu
2,000
1,758
1,857
Misungwi
1,998
1,755
1,854
Sengerema
2,024
1,782
1,881
Ukerewe
2,051
1,809
1,908
Sumbawanga
2,015
1,772
1,872
Kalambo (Matai)
2,007
1,765
1,864
Nkasi (Namanyele)
2,028
1,786
1,885
Katavi (Mpanda)
2,050
1,807
1,906
Mlele (Inyonga)
2,028
1,786
1,885
Songea
1,965
1,723
1,822
Mbinga
1,999
1,756
1,856
Namtumbo
1,995
1,752
1,851
Nyasa (Mbamba Bay)
2,001
1,759
1,858
Tunduru
2,024
1,782
1,881
Shinyanga
1,971
1,728
1,828
Kahama
1,985
1,742
1,841
Kishapu
1,999
1,757
1,856
Simiyu (Bariadi)
2,012
1,770
1,869
Busega (Nyashimo)
2,005
1,763
1,862
Itilima (Lagangabilili)
2,015
1,773
1,872
Maswa
2,004
1,761
1,860
Meatu (Mwanhuzi)
2,011
1,768
1,867
Singida
1,933
1,690
1,790
Iramba
1,945
1,702
1,802
Manyoni
1,917
1,675
1,774
Ikungi
1,928
1,686
1,785
Mkalama (Nduguti)
1,957
1,715
1,814
Tabora
1,996
1,754
1,853
Igunga
1,950
1,708
1,807
Kaliua
2,014
1,772
1,871
Ulyankulu
2,008
1,766
1,865
Nzega
1,961
1,718
1,817
Sikonge
2,008
1,765
1,865
Urambo
2,009
1,767
1,866
Tanga
1,825
1,586
1,745
Handeni
1,846
1,607
1,725
Kilindi
1,861
1,622
1,759
Korogwe
1,838
1,598
1,738
Lushoto
1,847
1,608
1,748
Mkinga (Maramba)
1,832
1,593
1,759
Muheza
1,830
1,591
1,745
Pangani
1,832
1,593
1,752


B: BEI ZA JUMLA


Bei za Jumla - DSM
Petroli (Sh/L)
Dizeli  (Sh/L)
Mafuta ya Taa (Sh/L)
Bei Kikomo
1,737.38
1,494.85
1,594.04

Bei za Jumla - TANGA
Petroli (Sh/L)
Dizeli  (Sh/L)
Bei Kikomo
1,720.47
1,481.29


Felix Ngamlagosi
MKURUGENZI MKUU
EWURA

Breaking News..Kabwe Zitto Kununua Timu Kubwa ya Mpira Nchini.

MBUNGE wa Kigoma Mjini, Kabwe Zitto (ACT), ametangaza azma ya kuinunua timu ya soka ya JKT Kanembwa inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara.

Akizungumza , mbunge huyo alisema kuwa tayari ameshaanza mazungumzo na uongozi wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) mkoani Kigoma kuona kama upo uwezekano wa kuinunua timu hiyo.

Alisema kuwa mpango wa kuinunua timu hiyo unakuja katika kutekeleza azma ya kuwa na timu ambayo itacheza Ligi Kuu Tanzania Bara na kurudisha hadhi ya michezo ya mkoa Kigoma kwenye soka.zitto-kabwe-facebook-frontKabwe alisema kuwa iwapo uwezekano wa kuinunua timu hiyo utafanikiwa mpango utafanywa kuunda kampuni ambayo itakuwa ikisimamia uendeshaji wa timu hiyo kama ilivyo kwa timu ya Azam.

Alisema ni jambo la aibu kuona mkoa wa Kigoma hauna timu hata moja katika Ligi Kuu wakati sehemu kubwa ya wachezaji wanaochezea timu zinazoshiriki ligi hiyo wanatoka Kigoma.

Pamoja na azma hiyo alisema kuwa kama itashindikana kwa timu hiyo kununuliwa kutokana na taratibu za jeshi atatafuta timu nyingine ambayo ataisimamia na kuiwezesha kufanya vizuri ili iweze kucheza Ligi Kuu.

Katika kauli yake Kabwe ametanabaisha kuwa pamoja na mpango wa kuwa na timu ya mpira wa miguu, mpango wake ni kuhakikisha wachezaji wakongwe waliowahi kuchezea timu za madaraja ya juu na timu ya Taifa wakiwemo Juma Kaseja na wengine wanarudi mkoani humo ili kusimamia timu za mkoa huo na kuzifanya ziweze kucheza mashindano ya ligi mbalimbali nchini kwa mafanikio.

Kauli hiyo ya Zitto inakuja siku moja baada ya kuutangazia umma mazungumzo ya awali kati yake na Mkurugenzi wa timu ya Azam FC, Abubakar Bakhresa kuhusu kuanzisha shule ya kuendeleza vipaji Kigoma.


Dr. Slaa Ajibu Mapigo....Akanusha Nyumba Yake Kupigwa Mnada Kisa Mkopo Aliochukua Mkewe Na Kumpa Mwanaume Mwingine

Katibu Mkuu wa Zamani wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbroad Slaa ametoa majibu kuhusu taarifa zinazoandikwa kwenye baadhi ya magazeti nchini pamoja na mitandao kuwa nyumba yake iliyoko Mbezi jijini Dar es Salaam inauzwa baada ya kushindwa kulipa mkopo wa Benki ikidaiwa kuwa mkewe aliuchukua na kumpa mwanaume mwingine.

Taarifa hizo zilieleza kuwa Mke wa Dk. Slaa, Josephine alichukua mkopo wa shilingi milioni 300 katika moja kati mabenki nchini na kushindwa kuirudisha fedha hiyo.

Dk. Slaa ambaye yuko nchini Canada akijiendeleza kimasomo, amekanusha taarifa hizo na kueleleza kuwa yeye na mkewe Josephine hawajawahi kuchukua mkopo katika benki yoyote nchini.

“Nataka nikuambie na uwajulishe Watanzania kwamba wala si mimi Dk. Slaa wala mke wangu, Josephine kwa wakati wowote ule hatujawahi kuchukua mkopo benki,”Dk. Slaa aliliambia gazeti la Mtanzania kwa njia ya simu.

“Tangu nitoke Bungeni sijawahi kuchukua hata senti moja benki, achilia mbali propaganda ya shilingi milioni 300.
" Hivyo, ni vizuri waliokupa taarifa wakupe undani ni benki ipi nilikopa au Josephine alikopa na ni shilingi ngapi na kwa nyaraka zipi. 
"Na ni vema ukafuatilia benki husika pia kama walikuwambia ni benki gani,”Mwanasiasa huyo mkongwe alieleza.

Dk. Slaa ambaye alitangaza mwaka jana kustaafu siasa, alisema kuwa anapanga kuchukua hatua za kisheria dhidi ya wote walioandika habari hizo.

Zuma kulipa fedha za ukarabati wa nyumba yake

Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amekubali kulipa kiasi cha dola milioni 23 ambazo serikali ilitumia kurekebisha nyumba yake iliopo mashambani.
Katika ripoti ya 2014,ripoti yake mlinzi wa umma imesema bw.Zuma alifaidi kinyume na sheria.
Bw.Zuma amesema kuwa mkaguzi mkuu na waziri wa fedha wanafaa kubaini ni kiasi gani anapaswa kulipa ili kumaliza mgogoro huo.
Tangazo hilo linajiri wiki moja kabla ya kusikilizwa kwa swala hilo.
Urekebishaji wa makao hayo katika kijiji cha Nklanda nyumbani kwa zuma katika mkoa wa kwa Zulu Natal umezua mgogoro mkubwa wa kisiasa nchini Afrika Kusini.
Baadhi ya fedha zilitumiwa kujenga ukumbi wa maonyesho,kidimbwi cha maji na zizi la ng'ombe.

US: Wagombea sasa waelekea New Hampshire

 
Wanachama wa Republican na Democrats nchini Marekani wanaopigania tiketi za vyama vyao tayari kwa uchaguzi wa urais nchini Marekani wameanza kuwasili katika jimbo la New Hampshire ambapo uchaguzi mwengine utafanyika.
Walioshinda katika kamati za wabunge za Iowa walikuwa Sineta Ted Cruz wa chama cha Republican na Hillary Clinton wa Democrats.
Bw.Cruz alishinda licha ya kuwa nyuma katika kura ya maoani huku Bi.Clinton akimshinda sineta Bernie Sanders kwa asilimia 0.2.
Jimbo la New Hampshire linaonekana kuwa na changamoto tofauti kwa vyama hivyo.Jimbo hilo lenye watu wa msimamo wa kadri na wasio na wasiofuata dini huenda likawa changamoto kubwa kwa bwana Cruz wakati mchujo huo utakapofanyika mnamo tarehe 9 mwezi Februari.
Donald Trump,ambaye amekuwa kifua mbele kwa upande wa chama cha Republican anatarajiwa kufanya vyema zaidi ya Iowa ambayo mchujo wa kwanza ulifanyika.
Upande wa Democrats,Bw.Sanders anaonekana kuwa na fursa ya kuwa nyumbani dhidi ya Bi Clinton,akiwa sineta wa jimbo jirani la Vermont.

Hata kabla ya ushindi mdogo wa Bi.Clinton kutangazwa rasmi,Bw.Sanders alikuwa amepanda katika lori moja akisalimiana na mashabiki katika mji wa Bow jimbo la New Hampshire.
Akiuambia umati huo kwamba kampeni yake imeushangaza ulimwengu huko Iowa,ameahidi kwamba itaushangaza tena ulimwengu katika Jimbo la New Hampshire.
Katika jimbo hilo,Bi Clinton alitangaza ushindi akisema kuwa anaamini kwamba anaelekea kupata ushindi mwengine katika jimbo la New Hampshire baada ya kuibuka mshindi Iowa.
''Nimeshinda na kupoteza huko, na ni vizuri kushinda'',alisema akiangazia alipopoteza katika jimbo hilo mwaka 2008.