MICHAKATO

Levis Rocky Ndekeno

This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Pages

Monday, January 27, 2014

JK aagiza JWTZ kujenga kambi ya muda Kilosa

RAIS Jakaya Kikwete, ameagiza Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), kujenga kambi ya muda ya mahema na mabati katika kijiji cha Magole mkoani Morogoro, ili waathirika wote wa mafuriko wasio na nyumba, waishi kwenye kambi hiyo. Mbali na agizo hilo, pia ameitaka Serikali kuandaa utaratibu wa kupata magodoro kutoka katika kampuni zinazotengeneza magodoro hayo na kuwagawia waathirika hao.
Ametoa maagizo hayo jana katika viwanja vya Shule ya Sekondari Magole, ambako kumewekwa kambi ya muda kwa waathirika wa mafuriko yaliyotokea Januari 22, mwaka huu.
Akiwa katika kambi hiyo, Rais Kikwete aliyewasili jana mchana kwa helkopta ya Polisi, alishuhudia idadi kubwa ya waathirika waliokumbwa na mafuriko wakiwemo watoto wadogo, wakilala chini na kuwa hatarini kupatwa na magonjwa ya vichomi na kuhara.
Kabla ya kutembelea waathirika na kuwahutubia, Rais Kikwete alitembelea daraja lililoathirika na mafuriko, maeneo yaliyoathirika vibaya na kupewa taarifa ya athari ya mafuriko kwa kata za Wilaya ya Kilosa, Gairo na Mvomero.
“Mafuriko haya ni makubwa na hayajawahi kutokea , watu wameathiriwa kwa nyumba zao kubomoka, kujaa maji na kuwafanya kukosa makazi na wengi wao wanalala chini.
“Serikali itatafuta magodoro kati ya siku mbili hizi na kuyaleta hapa kwa waathirika wa mafuriko ili kila mmoja alale kwenye godoro na si chini, lengo ni kuwaepusha kupatwa na magonjwa hasa ya vichomi na kwa watoto kuhara.
“Wenye viwanda hivi vya magodogo waendelee kuzalisha kwa wingi na waliyokuwa nayo stoo walete …hatuwezi kuwaacha watu waendelee kulala chini,” alisema Rais Kikwete.
Kwa upande wa chakula, alisema Serikali inacho cha kutosha kwenye maghala yake ambayo aliagiza yafunguliwe na chakula hususani maharage na mahindi, yasambazwe kwa waathirika.
Aliomba pia wadau wengine waendelee kujitokeza kusaidia kutoa chakula hasa mchele. Kuhusu huduma ya maji, alisema itaendelea kutolewa na magari ya JWTZ, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji pamoja na magari ya kampuni za ujenzi za China hadi huduma ya maji kwenye kijiji hicho na vingine itakapotengemaa.
Pia alizungumzia umuhimu wa kuwatafutia waathirika na wakazi wengine, maeneo mengine ya miiinuko yenye usalama kwa kujenga makazi yao ya kudumu.
Katika hatua nyingine, Rais Kikwete amewataka wakuu wa wilaya za Mkoa wa Morogoro pamoja na wakurugenzi watendaji wa halmashauri, kuwahudumia wananchi nyakati za matatizo, kwani uongozi wao utapimwa na wananchi kutokana na ushiriki wao wa moja kwa moja kwao.
Ametoa kauli hiyo, baada ya kutoridhishwa na takwimu za waathirika wa mafuriko zilizotolewa na uongozi wa Mkoa, kuhusu idadi ya kaya na watu waliokumbwa na mafuriko katika tarafa ya Magole, Wilaya ya Kilosa; Dakawa Wilaya ya Mvomero na Gairo kutoonesha mchanganuo halisia.
Kutokana na kasoro hizo, Rais alitoa siku moja ya jana kwa wakuu wa wilaya hizo na uongozi wa mkoa, wampatie takwimu kamili zikiwa na majina ya watu waliobomolewa nyumba ambao wanaishi kwa majirani na kambini, ili misaada inayotolewa iwafikie walengwa na si wajanja wachache ambao si walengwa.
“Uongozi unapimwa katika kipindi cha matatizo ya watu, sijaridhika na takwimu hizi, hazioneshi walengwa halisia... jipangeni vizuri mnipe taarifa kamili kesho (leo), ili Waziri William Lukuvi (Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge) na wengine wazifanyie kazi kuwezesha upatikanaji wa huduma bila kuachwa mtu aliyeathiriwa na mafuriko,” alisisitiza.
Awali Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera, alisema watu 12,472 walikumbwa na mafuriko hayo na kaya 2,759 zimeathiriwa, wakati nyumba 1,141 zilibomolewa na nyingine 2,922 kuzungukwa na maji.

Alisema kuna mahitaji ya tani 635.5 za chakula kwa miezi sita kuanzia sasa na Sh milioni 57 kwa ajili ya kujenga makazi ya muda.

Wizara za Fedha, Elimu kuwekwa ‘kitimoto’

Zitahojiwa na Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu matumizi ya marejesho ya fedha za radaDar es Salaam. Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali, PAC, imepanga kuzikutanisha kwa pamoja, Wizara za Fedha na Elimu wakati ikipokea taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) inayohusu matumizi ya fedha za marejesho ya rada jinsi zilivyotumiwa.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Deo Filikunjombe alisema kuwa wanatarajia kupokea taarifa hiyo kesho na watatumia fursa hiyo kujihakikishia kama matumizi hayo yalikuwapo au kama kulikuwa na ulaghai wa aina yoyote.
“Kwa sasa ni mapema kuanza kufikiri kwamba fedha hazikutumika inavyotakiwa, lakini kama kuna ujanja wowote ulifanyika tutabaini tu alisema na kuongeza:
“Ndiyo sababu katika kikao hiki tunakutana wote; CAG, Wizara ya Fedha na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ili kama kuna maswali basi kuwe na majibu yake papo hapo,” alisema Filikunjombe.
Alisema leo watapokea taarifa ya ukaguzi maalumu kuhusu mbolea ya ruzuku, pia shughuli nyingine ambazo kamati inatarajia kuzifanya katika kipindi cha wiki mbili zijazo ni pamoja na kutembelea bandari na kukagua mradi wa kuzalisha umeme kwa kutumia makaa ya mawe wilayani Ludewa.
Awali mwaka jana aliyekuwa Naibu Waziri wa Fedha, Janeth Mbene, aliliambia Bunge kwamba fedha za rada zilizorejeshwa Sh72.3 bilioni ziliingizwa katika bajeti ya serikali kwa mwaka 2012/13.
Mbene alisema kwamba fedha hizo ni marejesho kwa Serikali ya Muungano kutokana na udanganyifu uliofanywa na Kampuni ya BAE Systems ya Uingereza wakati wa kuiuzia Serikali ya Tanzania rada ya kuongozea vyombo vya usafiri angani.
Fedha zilizorudishwa na kampuni hiyo baada ya Taasisi ya Uchunguzi wa Makosa Makubwa ya Jinai (SFO) ya Uingereza kubaini kuwa, baadhi ya maofisa wa Serikali ya Tanzania na mawakala wa ununuzi kupandisha bei baada ya kushawishiwa na kampuni hiyo.
Novemba mwaka jana Serikali ilianza kusambaza vitabu milioni 19.4 kwa shule za msingi nchini, ambavyo ilielezwa kuwa vimenunuliwa kwa chenji ya rada na asilimia 75 ya fedha hizo zimetumika kununulia vitabu hivyo na asilimia 25 zitatumika kununulia madawati.

Vita ya umeme

WAKATI Watanzania wakilia ugumu wa maisha pamoja na mambo mengine, kupanda kwa gharama za nishati ya umeme, imethibitishwa kuwa kuna wafanyabiashara wanapambana bei hiyo isishuke. Wafanyabiashara hao; wenye mitambo ya kufua umeme wa mafuta na waagizaji wa mafuta, wananufaika kwa kunyonya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), ambalo linalazimika kuwapa karibu Sh bilioni nne kila siku, ili lipate umeme huo wa mafuta kutoka kwao.
Akizungumza juzi katika siku ya mwisho ya ziara yake ya kutembelea ujenzi wa bomba la gesi na mitambo ya kuchakata gesi Mtwara na Lindi, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, alisema wafanyabiashara hao wanauzia Tanesco umeme uniti moja kwa kati ya senti 33 na 50 ya dola ya Marekani.
Bei hiyo ya umeme kwa Tanesco ni kubwa kuliko ambayo shirika hilo linauza kwa wateja wanaotumia umeme mdogo wa majumbani, wa kati kwa wafanyabiashara, wa kati viwandani na mkubwa kwa viwanda vikubwa, na kubwa kuliko bei ya umeme ya mashirika ya umeme ya nchi za Afrika Mashariki.
Tanzania kwa sasa inatumia megawati 1,850 ambazo asilimia 80 kwa mujibu wa Pinda, zinazalishwa kwa mafuta ya dizeli na mazito; wakati asilimia nyingine ndizo zinazotokana na vyanzo vingine vya maji na gesi ya Songosongo.
Bei ya umeme Kwa mujibu wa takwimu za Tanesco, wateja majumbani wananunua uniti moja kwa senti 19 ya dola, wateja wa biashara senti 13 na viwanda vya kati na vikubwa senti 10. Umeme wa taa za barabarani ni senti 19.
Kwa nchi za Afrika Mashariki, hasa Kenya, Uganda na Rwanda, wateja majumbani hununua uniti moja kwa senti 20, wa biashara ni kati ya senti 16 na 20.
Viwanda vya kati Uganda bei ni senti 17, Kenya 14 na Rwanda 19. Kwa umeme wa viwanda vikubwa, bei kwa Uganda ni senti 12, Kenya 15 na Rwanda 19. Tanzania inaongoza kwa kutoza bei kubwa kwa taa za barabarani ambayo ni senti 19 sawa na Rwanda huku Kenya na Uganda bei kwa umeme huo ni senti 18.
Hali hiyo inadhihirisha kuwa pamoja na kupandisha bei ya umeme mwezi huu, bado gharama za umeme kwa Tanesco ni kubwa kuliko bei ya kuuzia, na kusababisha shirika hilo muhimu katika uchumi wa nchi, kujiendesha kwa hasara.
Suluhisho Pinda alisema bomba la gesi kutoka Mtwara likimalizika kujengwa na uzalishaji kuanza, Tanesco itanunua umeme huo kwa senti 8 na kufanya nishati hiyo kushuka bei. Kauli hiyo ya kushusha bei ya umeme baada ya gesi kuanza kutumika Dar es Salaam, pia ilipata kutolewa na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.
“Hii bei ya umeme iliyopo sasa ni ya muda tu na itashuka sana bomba la gesi litakapokamilika, kwa sababu hata mitambo ya kufua umeme inayotumia mafuta nayo itatumia gesi na mitambo mipya ya gesi italetwa, nataka Watanzania wakubali hivyo.
“Serikali inataka umeme mwingi utokane na gesi, jua, upepo na joto ardhi, lakini wapo wanaokataa bomba kuja Dar es Salaam na hao hao wanalalamika umeme kuwa juu, mtu yeyote ambaye anajua dunia inakwendaje, hawezi kupinga kujengwa bomba la gesi.
"Miaka ijayo, chanzo kikubwa cha umeme nchini kitakuwa gesi asilia… nyie mtanitukana, mtanisema sana, lakini mimi nitabaki kwenye utaalamu na wala siwezi kuyumba, tatizo la umeme wa Tanzania litatatuliwa na gesi, kila kitu kikikamilika Tanesco na Ewura (Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji) hawawezi kuendelea kuweka bei juu," alisema Profesa Muhongo.
Mapambano “Sisi tunaona kuwa suluhu ya kuondokana na gharama hizi ni gesi, lakini kuna watu wanajua watanyang’anywa tonge midomoni, vita hii tunaijua; lakini hatuwezi kurudi nyuma katika hili ni lazima tusonge mbele,” alisema Pinda.
Alisema nyuma ya mapambano ya kuzuia gesi kufika Dar es Salaam, wapo wafanyabiashara ambao wanahofia kuwa mwisho wa biashara yao ya kuuzia Tanesco umeme kwa bei ya juu umefika.
Alisema watu kwa sasa wananufaika na Tanesco kununua mafuta ya kuendeshea mitambo ya umeme. Katika hali hiyo, Pinda alisema uamuzi wa Serikali kuchimba gesi hiyo na kuisafirisha hadi Dar es Salaam si jambo jepesi, kwani utekelezaji wake unakabiliwa na mapambano na upinzani mkubwa kutoka kwa wenye mitambo ya kuzalisha umeme ambao kwa sasa wananufaika kutoka Tanesco.
Alisisitiza, kuwa Serikali imedhamiria kuachana na umeme huo wa mafuta na kama wafanyabiashara hao wanataka kuendelea na biashara hiyo, ni vema wabadilishe mitambo yao iwe ya gesi na si ya mafuta kama ilivyo sasa.
Mataifa, ushauri Pia alisema vita nyingine wanayokabiliana nayo ni ya nchi ambako kampuni za utafiti wa mafuta na gesi zinatoka, ambazo zinataka kampuni zao zipewe zabuni ya kutandaza bomba la gesi na kujenga mitambo ya kuchakata gesi.
“Wanalalamika gesi wametafuta na kugundua wao, halafu kandarasi anapewa China, sisi tumewajibu kuwa tumekimbilia China kwa sababu masharti yao ni nafuu kuliko yao,” alisema Pinda.
Katika hatua nyingine, Pinda alitaka wakazi wa Lindi na Mtwara kutambua kuwa gesi hiyo ni rasilimali ya Taifa na itanufaisha nchi nzima. Aliwataka wajiandae kwa uchumi huo kwa kuhakikisha wanatumia fursa zilizopo kufaidika. Aliwataka wasikubali fursa ya gesi ilete balaa nchini badala ya neema.
“Kama tunataka iwe neema tushirikiane na wadau wakubwa zaidi ili nchi yetu ipige hatua kimaendeleo.”
Kwa upande wake, Profesa Muhongo aliwataka wananchi wa mikoa ya Lindi na Mtwara kusomesha watoto wao hasa katika Sayansi, ili wafaidike na uwepo wa gesi na mafuta katika mikoa hiyo.
Alisema Serikali imejitahidi kusomesha vijana katika eneo la gesi na wamekuwa wanahamasisha vijana wa mikoa hiyo kuchukua masomo ya Sayansi kwa vile wizara inagharimia baadhi ya vijana kusoma masuala ya gesi vyuo vikuu vya ndani na nje ya nchi.

Pinda katika ziara hiyo alielezea kuridhika na kazi inayoendelea katika mradi huo na akasema upo uwezekano mradi huo ukakamilika kabla ya muda wake uliopangwa wa miezi 18.

Birdman aonyesha choo chake kilichotengenezwa na dhahabu, kichokadiriwa kuwa na thamani ya $1mil.

Birdman boss wa record label ya YMCMB ambaye mara nyingi huwa anajisifia kwa matumizi yake makubwa ya pesa kwenye vitu luxury, ameendeleza hivyo vitendo  vya kufanya matumizi makubwa ya pesa.
Hivi karibuni ame-share picha ya choo chake ambacho kime-kuwa covered na material ya dhahabu pande zote.
Mfuniko wake na sehemu ya juu ya choo hicho ni dhahabu tupu na sehemu nyingine yote hautaweza kukiona hicho choo kwasababu kimefunikwa na dhahabu.

Gharama yake inakadiriwa ni dola millioni moja.