MICHAKATO

Levis Rocky Ndekeno

This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Pages

Friday, April 22, 2016

Mabasi yaendayo kasi yaanza safari zake Dar

Mabasi yaendayo kasi, yameanza kufanya safari zake katikati ya jiji la Dar es Salaam Ijumaa hii.
 Jumla ya mabasi 50 yameingia barabarani. Kwa wewe ambaye hujui njia mbalimbali za mabasi hayo, chini ni sehemu yanapopita.
1) RUTI YA KIMARA- KIVUKONI Mabasi Sita (6). Kati ya mabasi Hayo sita wakati wa Kutoka Jangwani matatu yataenda Kimara na Matatu Kivukoni.
2. RUTI YA KIMARA – KARIAKOO Mabasi Sita (6). Kati ya hayo Matatu yataelekea Kariakoo na Matatu Kimara.
3. RUTI YA UBUNGO – KIVUKONI Mabasi nane (8). Kati ya hayo Mabasi Manne yataelekea Ubungo na Manne Kivukoni.
4. RUTI YA UBUNGO – KARIAKOO Mabasi nane (8). Kati ya hayo Mabasi manne Yataenda Ubungo na Manne yataenda Kariakoo.
5. RUTI YA UBUNGO – MOROCCO Mabasi nane (8). Kati ya hayo Manne yataenda Ubungo Manne yataenda Morocco.
6. RUTI YA MOROCCO – KARIAKOO Mabasi sita (6). Kati ya hayo mabasi Matatu Morocco na Matatu Kariakoo.
7. RUTI YA MOROCCO – KIVUKONI Mabasi nane (8). Kati ya Hayo Mabasi Manne yataenda Moroco na mabasi manne Kivukoni.
DESPATCH PLAN SAA KUMI NA MBILI KAMILI. 1. Kimara Terminal Mabasi Sita (6) 2. Ubungo Terminal Mabasi kumi na mbili (12) 3. Morocco Termial Mabasi kumi na moja (11) 4. Kariakoo Terminal Mabasi kumi (10) 5. Kivukoni Terminal Mabasi kumi na moja (11) JUMLA NI MABASI HAMSINI (50)

Chanzo cha kifo cha Prince chabainika, alitumia madaya ya kulevya kumzidi

Muimbaji, Prince alikuwa akitibiwa kutokana na kutumia madawa ya kulevya kupitiliza siku sita kabla ya kifo chake, TMZ wameandika.Kwa mujibu wa tovuti hiyo, ndege binafsi ya Prince ilitua kwa dharura huko Moline, Illinois Ijumaa iliyopita, saa chache baada ya kutumbuiza Atlanta.
Kipindi hicho wawakilishi wake walidai kuwa alikuwa akisumbuliwa na mafua, kitu ambacho kilizua maswali kwasababu ndege yake ilikuwa imebakiza dakika 48 tu kufika nyumbani kabla ya kuamua kutua kwa dharura.
Vyanzo mbalimbali kutoka Moline vimeuambia mtandao huo kuwa Prince aliwahishwa hospitali na kupewe huduma ya haraka (save shot) kumsaidia.
Vyanzo hivyo vimedai kuwa madaktari walimshauri Prince akae hospitali hapo kwa saa 24. Watu wake walitaka chumba binafsi na walipoambiwa kuwa haiwezekani, Prince na wenzake waligoma.
Muimbaji huyo aliondoka saa tatu baada ya kufika hapo na kuelekea nyumbani. Vyanzo hivyo vimedai kuwa Prince aliondoka akiwa hajisikii vizuri.
Prince alikutwa hajitambui jana kwenye lifti kabla ya kutangazwa kuwa amefariki.

Director wa filamu za James Bond afariki akiwa na umri wa miaka 93

Muongazaji wa filamu ya James Bond Guy Hamilton amefariki akiwa na umri wa miaka 93.
Aliyekuwa nyota wa filamu hiyo ya 007 Roger Moore alituma ujumbe katika mtandao wake wa Twitter kwamba alihuzunishwa na kifo chake.

Hamilton alimuelekeza Roger Moore katika filamu ya Live and Let Die pamoja na The man with the Golden Gun.
Pia alifanya uelekezaji katika filamu za Sean Connery in GoldFinger na Diamond are Forever.
Hospitali moja katika kisiwa cha Uhispania cha Majorca ,ambapo Hamilton aliishi ilithibitisha kwa chombo cha habari cha AP kwamba amefariki sikju ya Jumatano.
Filamu nyengine zilizoelekezwa na Hamilton ni pamoja na The Battle in Britain,Force 10 from Navarone,Evil under the sun na The Mirror Crack’d.